Nimekwisha na UKIMWI

Kama signature yako inavyo jieleza mkuu..."Pambana na hali yako"
Na kaa ukijua kuambukizwa virusi sio mwisho wa maisha, maisha lazima yaendelee.
Binafsi nina mfahamu mtu ambaye huu ni mwaka wa 15 toka athirike na ana dunda tu.
Man up usimtenge mkeo, fanyeni maisha.
 
Kwakweli najilaumu sana kuogopa ukimwi,matokeo yake mechi zote kasoro moja tu nilicheza nikiwa full metal jacket a.k.a full protected na condom,

yeah,sina ukimwi ndio na vilevile sina mtoto,,ha ha ha ha..

Sasa wewe mtu kazaliwa nao,hadi kafika umri wa kuolewa,kuna ugonjwa hapo au ni kuharibiana malengo tu?,
 
Kwakweli najilaumu sana kuogopa ukimwi,matokeo yake mechi zote kasoro moja tu nilicheza nikiwa full metal jacket a.k.a full protected na condom,

yeah,sina ukimwi ndio na vilevile sina mtoto,,ha ha ha ha..

Sasa wewe mtu kazaliwa nao,hadi kafika umri wa kuolewa,kuna ugonjwa hapo au ni kuharibiana malengo tu?,
 
Kwanza pole..pili huyo mwanamke ni muongo hakuzaliwa nao....eti alikua hajui?
Waliozaliwa nao mpk kufika umri wake lazma awe alishaanza kutumia dawa...dawa wanaanzishiwa wakiwa wadogo..sasa yeye hajui..alikua hanywi dawa..jibu ni big no...km alizaliwa nao ..basi anajua cz anakunywa dawa....la sivyo asinge survive mpk sasa hivi..unacheza na cd4??...
huyo kaupata ukubwani..na hapo alipo anajua..na anakunywa dawa...na ht km kazaliwa nao...dawa anaanzishiwa tangu akiwa mdogo...
Pole sana....
 
takwimu zinaonesha waathirika wa ukimwi wanaishi maisha sawa na ambao hawajaathirika na ukimwi (sikumbuki chanzo vizuri ila nahisi niliona hii habari bbc) hivyo usikate tamaa dunia imebadilika ukimwi hautishi tena..cha msingi ni kuikubali hali na kuwaza vitu chanya nakuhakikishia una miaka zaidi ya 50 mbele kama ukichagua kuishi maisha mazuri...maisha yako yapo mikononi mwako
 
Acha wenge ww, kwani ukikutwa umeathirika hutaishi? Unaweza ukaishi miaka 30 mbele kama utafuata masharti. Onyo, usimnyanyase huyo mwanamke wala mtoto, waleee, na ndoa ufunge
 
Mmmh!

Amezaliwa nao, na yeye hakujua kama anao..

Means hadi unakutana naye hakuwahi kuonesha dalili za kuwa mwathirika.

Anaonekana ana afya yake, na kinga yake iko poa, maana hata dawa hakuwahi kutumia..

Kumbe hata wewe unaweza ukawa na maisha marefu zaidi..

Jipe moyo.

Sent Using Nokia Torch
 
Mimi napata ukakasi kidogo kama mtaalam wa AFYA.

Kabla ya mama kuanza kliniki lazima mama mfuatane nae kwenda kupima afya kwa pamoja, kama imeshindikana wote kufuatana basi hata mama ni lazima apimwe VVU ili kama ameathirika ziweze kuchukuliwa hatua za kuzuia maambukizi kutoka kwa maama kwenda kwa mtoto, Prevention Of Mother To Child Transmission (PMTCT).


Huko mlipoenda na hamkupima au mama hakuambiwa hili ni wapi?


Kuna UJINGA umefanyika mahali.


Anyway nakupa pole sana
 
Pole sana mkuu , ktk maisha tunakutana na changamoto nyingi sana lkn muhimu nikutambua changamoto hazikuwepo Kwa ajili ya kutumaliza.

Wala suala ilo lisikufanye ukate tamaa namaisha wala kuona ukom wamaisha yako ,, usikae ukawaza juu ya ugumh utakaoupitia ktk maisha yako ..

Now days Life spam ya wanadam for those HIV + na HIV - ni inakaribiana tu , shukuran Kwa madaktar wanaoendelea kugundua protein ambazo zimekuja kua na positive effect ktk ARVs kwaiyo usiumie kabisaaa maisha bado yapo kabisaaa Kikubwa nikuepukana na Mawazo .

Kwanza sikushauri kupima kwasasa ,lkn pia usikae pekee yako jaribu kuongea sanaaa as much as you can , tembea tembea sana. Utakapoona sasa upon vzur kajisogeze kuchek dam .


Msamehe sana uyo Mdada , lkn pia Mwombe Mungu sanaaaa.

Nahisi kuna haja , siku moja nitatoa somo kuhusiana na HIV ,, litakua somo litakalosaidia kuweza kutambua HIV patient anayetumia dawa ,,na HIV patient asiyetumia dawa .

But guyz this issue nibora usiuze gem kavu kavu ,,,kuna watu kazi yao nikuua wenzao alafu kwenye mazishi hawaji
 
Wewe Kapime wala usiogope.

Majibu yatakuja mazuri tu
 
Pole mkuu, pasi na shaka huyo dada alikuwa anafahamu kila kitu, muhimu ni kusamehe, mlee mwanao maana naamini atakuwa amezaliwa salama. Naomba Mungu afanye miujiza mtoto asibaki yatima.

Sent using Jamii Forums mobile app
 

Hili jipya kwangu, wataalam ufafanuzi zaidi please.

Mleta mada usiwe na wasiwasi kipindupindu na malaria zinaua kuliko ukimwi
 
Pole sana Mkuu. Kuwa mpole tu usimjie juu mwenzio labda kweli hakujua. Washirikishe ndugu, jamaa na marafiki wa karibu na ambao unawaamini. Poleni sana.

 
Kwa nini huku pima kabla ya kuchovya?

Tamaa zako sasa zinakuua
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…