Nimekutana na Mchina aliyekuja kama kibarua Tanzania ila sasa yeye ni Big Boss

Mhaya

JF-Expert Member
Aug 20, 2023
1,658
4,866
Jana kuna mchina nilikutanishwa nae ni CEO wa kiwanda cha uzalishaji wa marine boards, melamain boards, pliewoods na MDF ambacho wamekijenga pale Mafinga.

Nilimuuliza ABCs za maisha yake hapa Tanzania na akanambia yafuatayo.

1. Yeye alikuja Tanzania kipindi cha ujenzi wa uwanja wa mpira wa Benjamini Mkapa na alikuja kama kibarua wa kulipwa posho kwa siku.

2. ⁠Uwanja ulipoisha kwasababu alipokuwa kibarua alikua akijituma sana boss wake alimwamini na kumpa kazi ya kusimamia Makarasha Chalinze kama Foremen.

3. ⁠Walipomaliza mradi wa Chalinze yeye aliona kurudi china haiwezekani kwani kwa muda aliokaa TZ kaona fursa nyingi na utajiri mwingi.

4. ⁠Aliamua kumshawishi boss wake kwamba kama wao wanarudi china yeye anaomba abaki TZ aone fursa na ndipo alipoenda mafinga na kuona fursa iliyopo kwenye miti. Na akamwambia boss wake wafungue kiwanda yeye atakisimamia na atahakikisha mtaji unarudi na faida wanapata.

5. ⁠Boss Alikubali na sasa kile kiwanda ni kikubwa yeye ndo msimamizi na anamiliki billions of money .

NILIMUULIZA KWA MUDA ALIOKAA AMENIFUNZA NINI NDANI YA TANZANIA.

1. Alinambia nyie Watanzania ni watu wajinga sana kwasababu mnaamini kwenye miujiza kwakutumia muda mwingi kusali na kulala.

2. ⁠Fedha mlizotafuta kwa jasho mnachezea kamali/gulugulu alilotengeneza mchina mkiamini mtapata utajiri, akamalizia hakuna utajiri wa namna hiyo.

3. ⁠Hamjui matumizi ya simu, muda mwingi mnatumia simu kwa vitu vya kijinga akishangaa mtanzania anaweza kukupigia cm mara 20 mfululizo kama hupokei simu yake. Yeye Ana muda maalum wa kupiga cm na kupokea simu.

4. ⁠Mnaabudu na kuamini wanasiasa wanaweza tatua shida zenu kumbe wao ndo wanawategemea ninyi mtatue shida zao.

5. ⁠Mfumo wenu wa Elimu ni wa kijinga kwasababu haumuandai mtoto kuwa mbunifu na kutumia maarifa yake kubuni/ama kuzalisha bidhaa ili ziingie sokoni.
 
Ni ukweli usiopingika elimu ya kukariri haitufai na tumeona mpaka viongozi wakiongelea sayansi ya kukariri maana unasikia kabisa kakariri
Wanajituma sana hata kama hela zimeingizwa au mashine zimekuja kutoka kwa mafia hatujali mradi wanaajiri watu
Ila na sisi tupeleke hela kwao sasa
 
1.watanzania ni watu wajinga sana kwasababu mnaamini kwenye miujiza kwakutumia muda mwingi kusali na kulala.

2. ⁠Fedha mlizotafuta kwa jasho mnachezea kamali/gulugulu alilotengeneza mchina mkiamini mtapata utajiri, akamalizia hakuna utajiri wa namna hiyo.

3. ⁠Hamjui matumizi ya simu, muda mwingi mnatumia simu kwa vitu vya kijinga akishangaa mtanzania anaweza kukupigia cm mara 20 mfululizo kama hupokei simu yake. Yeye Ana muda maalum wa kupiga cm na kupokea simu.

4. ⁠Mnaabudu na kuamini wanasiasa wanaweza tatua shida zenu kumbe wao ndo wanawategemea ninyi mtatue shida zao.

5. ⁠Mfumo wenu wa Elimu ni wa kijinga kwasababu haumuandai mtoto kuwa mbunifu na kutumia maarifa yake kubuni/ama kuzalisha bidhaa ili ziingie sokoni.
 
1.watanzania ni watu wajinga sana kwasababu mnaamini kwenye miujiza kwakutumia muda mwingi kusali na kulala.

2. ⁠Fedha mlizotafuta kwa jasho mnachezea kamali/gulugulu alilotengeneza mchina mkiamini mtapata utajiri, akamalizia hakuna utajiri wa namna hiyo.

3. ⁠Hamjui matumizi ya simu, muda mwingi mnatumia simu kwa vitu vya kijinga akishangaa mtanzania anaweza kukupigia cm mara 20 mfululizo kama hupokei simu yake. Yeye Ana muda maalum wa kupiga cm na kupokea simu.

4. ⁠Mnaabudu na kuamini wanasiasa wanaweza tatua shida zenu kumbe wao ndo wanawategemea ninyi mtatue shida zao.

5. ⁠Mfumo wenu wa Elimu ni wa kijinga kwasababu haumuandai mtoto kuwa mbunifu na kutumia maarifa yake kubuni/ama kuzalisha bidhaa ili ziingie sokoni.
Kuna watu humu wanabisha ooh kila tajiri kapita kwa mganga
Sasa nataka mganga wa huyo Mchina wamlete hapa
Siamini pia upumbavu huo wa kwenda kwenye nyumba ya nyasi na mganga analala chini eti anipe utajiri over my dead?
 
Hapo kwenye kupiga piga simu bila mpangilio nakubaliana naye, unakuta jitu linapiga hata mara 10 na huna hata biashara yeyote nalo. Na mwisho wa siku linakuwa bifu kabisa et hujapokea simu, mi huwa najiuliza mbona kabla ya simu maisha yalikuwa yanaenda tu!
 
Hiv unaamin wakija Chadema au ACT watatutoa huku ?
Mkuu,

Hatuna uhakika kama kikija chama kingine kitatutoa huku. Ila kuna msemo unaosema "huwezi kufanya kitu kile kile miaka nenda rudi halafu utegemee matokeo tofauti..!"

Kwa mfano mtu ukisoma kwa mda mrefu ukaona kabisa wewe kitabu hakipandi, ni ujinga kuendelea kung'ang'ania kusoma, badala yake ni bora ukajaribu kitu kingine mfano biashara, kilimo, nk.. unaweza kushangaa kusoma kumekushinda ila biashara ukakimbiza mbaya...!

Sasa chama kilichopo kama kwa miaka 60 hakijaweza tuletea maendeleo, si bora tujaribu kingine kuliko kuendelea kuking'ang'ania hicho hicho miaka nenda rudi huku tukitegemea matokeo tofauti? Au we unaonaje kiongoz.
 
Back
Top Bottom