Nimekutana na matapeli leo asubuhi

Nimekutana na matapeli leo asubuhi

nimekutana na wale matapeli wa pesa wakazania wataniibia kumbe mm mtoto wa mjini yani nimezaliwa moshi mjini nikasoma mpaka advance nkaja Dar Chuo na ni mtu ambaye ni mtundu sana wa mitandao ya kijamii

Scenario ipo hivi,

Nlikuwa nimesimama kituo cha daladala magomen mwembechai ile sehemu wanapaita kanisani maana kuna kanisa nazani ni la wasabato, akaja mzee akaniuliza Posta ferry ni wap nikamwambia panda daladala za posta kabla cjamaliza Akaja mtu wa pili akanza kumwambia huyu mzeee kwa nn usipande mwendo kasi Mara mzee akatoa pochi inadollar kwa juu i guess ni feki pia akaanza kuniambia anataka kuexchange zipo Dollar 3000.

mimi nimesoma stories nyingi mtandaoni najua kabisa Nkiwa naongea na mtu ambaye simjui naavoid anishike mkono au Bega maana wanatumiaga dawa anavyokushika ana kupossess anakuibia sasa Baada ya yule mzeee kutoa hizo dollar akatwambia tumuonyeshe sehemu pakuexchange atatupa laki mbili na hamsini kila mmoja nkasema oyaaa.


Mara yule jamaaa aliyetukuta akasemaje hata Sheli wanaexchange na ukiangalia hivi kuna sheli mbele yetu , mzee akanisisitiza nsimuache ananiamini , lakini kichwani kitu kinaniambia siunajua kuna matapeli eeeee nkasema wacha niwaangalie watafika wapi. basi tukaenda pale sheli...

Heti tumefika jamaaa akajifanya anapiga simu akamuuliza jamaaa wa kwenye simu upo Wap jamaaa akamwambia nipo hapa , tukakutana na huyo mtu wa pili akiwa kwenye Gari huyo ambaye alipigiwa simu , akaniuliza naitwa nani nkamwambia naitwa XXX nina ukoo wakichaga...

Jamaa akatwambia tuingie kwenye gari twende Sinza tukaexchange nkamwambiaje sinza mbona Mbali Kuna bureau exchange hapo Cha manzese akasema tupande gari basi nikapanda nikasema sikai mbele Hivyo kwenye gari tuwaka watu wanne.

Mara jamaa mwenye gari akashuka akaniambia njoo nje tuongeeee Nkatoka nae tukawa kwa nyuma akanifata akaniambiaje hizi hela nimewaambia ukiexchange ni milion 7 na laki tano ila ni milion 7 na laki sita kwa hyo Tutagawana hyo laki moja Siunajua udalali tena Nikamwambia sawa Nikaavoid yeye kunipa Mkono tukarudi kwenye gari safari ikaanza...

Sasa kwenye gari nyuma nimekaaa mimi na mzee , mzee akaanza kuniaidisia kuwa ana mtoto wake wakike aliyepo Oman ndo Kampa hizo pesa , anaongea huku anatetemeka kiukwel nakuniambia kijana wangu ww ndo nakuamini hapa , mm nipo makini muda huo.

Mara tumefika manzese wakawa wote wawili wananisisitiza kwanza nishike hizo hela za mzeee lakini mzee anasemaje hawaamini hawa watu wa mbele hivyo Tumuachie pesa zetu laki mbili mbili hili zifike milion atugaie dollar zake then niingie kwenye bureau exchange mimi na dereva ... Wale wawili wakasema wanazo so ikawa bado mimi

Huku Mzee wananisisitiza wewe kwenye account milion ngap ili mnipe milion mbili halafu niwape hizi dollar maana siwez kutoa tu bila kupewa chakushika... Mimi nikamwambiaje kwenye benki sina hata mia

Kwahyo hela yake ikiingia haitakutana na hela nyingi maana walianza kusema kwamba pesa zikitolewa niwekewe kwenye account yangu ili Mzee asiibiwe...

Mimi ikawa siongei nkawaambiaje pakini hapo Tiptop ili nitoe hela niwape si wakapaki heti wakawa wananiambiaje pokea pesa zile dollar nkawaambia wacha Mzee azishike...

Nkashuka Nkaanza kucheka nkawaambia wajaribu kwa wengine wakasepa Zao nikaenda chuo

Funzo:
Ukikutana na mtu humjui husimpe Mkono, Kama ni usiku usiongee na mtu humjui Wanatumia Dawa kuibiwa watu, especially anavyoongea na wewe huku anakushika shika mabega anakupoteza unaibiwa kila kitu nina Marafiki na ndugu in ameibiwa kwa hivi halafu pia tusiwe na tamaa na pesa za watu au pesa ya kirahisi.
Mzee wangu aliibiwa mafao yake namna hii inahudhunisha sana, binafsi nikishaona mtu simfahamu mara ghafra bin vuu anaanza kunipigisha story za pesa huwa inanikumbusha scenario ya Mzee mara namzingua.

Ila kuwa makini mkuu usipende kudandia magari ya wanaume usiowajua siku nyingine utakuja kubakwa mjini hapa!
 
hao tayari walishakuwin kaka... wamekutoa magomeni mpaka sinza unazunguka nao tu!! Wangekuteka je!?
hawakuniwin maana Hawakuchukua hata Simu maana Nina simu ya Kama laki tano hivi , Hatukufika sinza tumetoka mwembechai mpaka tiptop manzese
 
Pole sana na hongera kwa kufanikiwa kutoka salama. Ila next time usifanye kosa la kupanda gari la watu uliotilia shaka kuwa ni matapeli.

Kwa wengine kitendo cha kupanda tu gari lao ni tayari unawapa ushindi wa kukuibia kila ulicho nacho kwa 'upigaji wa kubwaga'.

Ova
ahsante mkuu Next time sitarudia , masiahara yangu yanaweza kunicost kwel kabisa
 
Hapokwenye kushikana mkono au kukushika Bega nitakuelleza kitu
Wewe shika mkono mwache akushike hafi bega
Hakuna uchawi mkubwa ama lolote
Isipokuwa kinachofanyika ni KUWIN mind yako
wnafanya vipikaa kwa kutulia nikueleze
sijaelewa
 
Mtoto wa mjini asingevunja safari yake na kuanza kuzulura na wezi, hivi pale sheli mngeitiwa wezi kwa kushitukiwa mpaka saa hii ungekuwepo? Hivi dereva angeendesha gari kuelekea anakokutaka bila kukusikiliza wewe ungefanyaje, haudhani muda huo Hulikuwa umejiweka mateka!
Mwisho, ni sehemu gani ya Moshi mjini utasema kunawajanja zaidi ya ubabe, Majengo au Kiboloroni! Moshi mjini hakuna watoto wa mjini labda Njiapanda nako si kivile. Wewe ulijiingiza kwenye kundi wa wezi ila bahati hakutokea mtu wa kusema anamtafuta yule mzee kwa kumuibia, usirudie kuvunja safari yako na kuanza kuongozana na watu usio wajua, usirudie.
Sawa
 
Wakazania = wakadhania
Heti = Eti
Kuniadisia = Kunihadithia....

Makosa ya kisarufi ni mengi mno na bado unasisitiza ni mwanachuo kumbe ndo tapeli mwenyewe
hamna ni lafudhi yangu ipo hvyo .
 
Waligundua hana pesa wakampotezea, Mimi hapa mjini sisikiliza mtu nisiemjua. Labda mtu akija akaniuliza nimuelekeze mahala ndio ntamuelekeza. Lakini eti sijui nauza simu, sijui Kuna ela yaan ukileta story za pesa najua wewe nitapeli Moja kwa moja kwahio sikupi nafasi ya kukusikiliza.
nilikuwa nina laki nne kwenye simu , na simu ni ya zaidi ya laki tano.
 
Siku nyingine usirudie tena.
1. Kosa la kwanza kuanza kuwasikiliza na kupiga nao stori
2.Kosa la pili kuvuka barabara eti unaenda nao sheli kubadilisha pesa.
3.Kosa la tatu ambalo ni baya zaidi ni kuingia kwenye gari. Yaani hapa ulishaingia kwenye mfumo wao walikuwa na uwezo wa kukufanya chochote kile basi tu shukuru Mungu upo hai mpaka leo na hawajakudhuru popote.

Hivi hata wangekupeleka tu polisi na kukugeuzia kibao kuwa ulitaka kuwauzia dola feki japo hizo dola ni za kwao ungechomokaje? Kuna vitu vya kujaribu lakini hili jaribio ulilofanya hakuna tofauti na kujaribu kuonja sumu. Kama una masikio na usikie ila ukiwa mbishi ipo siku yatakukuta makubwa.

Na usipende sana kuwalinganisha watu eti siju nawamudu, ooh sijui yule alikuwa mzee. Kumbuka kuwa hata wahuni wanazeeka na uhuni wao na hata hao unawaona kuwa unawamudu jua kuwa wametangulizwa mbele wenye kazi yao walikuwa wanafuatilia nyuma mwanzo mwisho sema tu walibaini kuwa huna kitu wakakuachia na wala usijisifu hata kidogo kuwa eti emewachomoka..
kilichotaka kuniponza ni huruma.
 
Hao matapeli ufaulu wao ilikua ni wewe kupanda gari lao, wangekufanya watakacho.

In short na wewe uliingia tamaa tayari. Mtu humjui, unakubalije kishamba kuungana nao mpk unapanda gari?

Next time never associate with foreigners in name of cash!
niliona watamtapeli mzee kumbe walitaka kunitapeli mimi, yani huruma yangu ndo ilinisababisha niingie kwenye gari
 
We bado mshamba huna ujanja wowote, yaani kukubali tu kupanda gari nimekuona wenge sana na mshukuru sana Mungu kwa kukuepusha na janga, kwani wangeweza kukupulizia dawa ya usingizi, kukutolea bastola au kitu kingine ili watimize haja yao

Na wengine wakikukuta huna hela, wanachukua simu etc na unaweza kuta marinda yako hayapo, kuwa makini sana mjini hapa


Usilete mazoea na mtu yoyote yule kiasi cha kupanda gari lao, kuna wengine kukukomoa wanaweza hata kukuitia mwizi ndio ujue binadamu jinsi walivyo washenzi
halafu watu unajua hamjafahamu kuwa dawa wanazotumia ni dawa ambazo tunafundishwa Darasani kama Scopolamine , dawa wanaweka kwenye pesa Pamoja na wakikushika mimi niliavoid hvyo vyote
 
Kulingana na maelezo kilichokunusuru ni kutokuwa na cash tofauti na hapo huwezi kuja na coclusion ya kwamba watu wasipaene mikono wala kugusana mabega. kitendo cha kuacha kazi zako na kuingia kwenye gari tayari ulishakuwa kwenye kumi na nane zao.
Hapana bhana na nlikuwa nimeshika simu Si wangenitapeli simu?
 
Back
Top Bottom