Nimekumbuka zamani

Chai sana hapa.
 
Nyie mlikuwa wajukuu wa kishua. Mambo ya CD na snacks.

Sisi michezo yetu ilikuwa kombolela, na kuiba kamba za bibi tunafunga bembea zile za kwenye mti . Halafu kuna kwenda kuogelea mtoni huko na kula vimatunda pori.
Hapo Pa kwenda kuogelea mtoni, umenikumbusha mbali mno.
 
😂😂😂😂
 
😂😂 Mkuu kwa bibi sio lazima kuwe bush haswa, babu na bibi walihamia kijiji kilichoendelea, barabara, maji , umeme havikua shida. Kwa bibi sio lazima kuwe na shida mkuu.

Hata mleta uzi kwa bibi yake kuna bonge ya geti, tv, movies kila mtu ana expirience yake nzuri anayokumbuka.

Na hata miaka hiyo ya 80 unayoisema wewe bado walikuwepo wenzio wanaenda kwa bibi na umeme sio bush.
 
Naona wengi story zenu zina ushua mwingi
 
bibi alikuwa anafungia ndani Tv zake zote hakuna kuangalia mpaka tuondoke,.

Sasa hapo ndio ile mikakati ilikuwa inaanza,. Ikikaribia likizo simu zinaanza kipigwa basi kila watu tunapangiana vitu vya kubeba

Awali ya yote zamani ina zama nyingi...

Leejay, hii zamani yenu inaonekana kama ni zamani ya Jakaya Kikwete hivi yenye kupigiana hadi simu ninyi wajukuu, maana nikikumbuka zamani ya simu za TTCL si kaya nyingi zilikuwa na huduma ya zile simu, na hata zikiwepo basi wazazi walikuwa wakizifungia kwenye kiboksi cha mbao chenye kikufuli au ile sehemu ya kuzungusha namba inawekwa lock...

Sisi wengine zamani zetu tulikuwa ni kwenda mtoni au mabwawani huko kuogelea na kuvua visamaki (hii tulikuwa tunapigwa marufuku sana sababu ya matukio ya kufa maji), kwenda porini kutafuta kuni, kwenda porini kuchunga mbuzi na ng'ombe lakini ukiwa mtoto lazima awepo mtu mzima sababu ya matukio ya kunyonya damu (tulikuwa tunaamini kuna nyonya damu 😅)...
 
Ndio maisha mkuu, Sasa Mimi ndio nilikaa kwa Bibi ,ndio nilikuwa nawapokea binamu zangu,dada zangu,wakiondoka kurudi Town nilikuwa napwaya kweli,ila nabaki na manguo kibao hadi nayagawa kwa wasiokuwa nazo!Hili
Ilaaa😂😂😂😂,. Ngoja wajuzi waje kukujibu mkuu
Nyeto zipo kitambo Mkuu,Tena wanyama walikuwa wanapiga nyeto balaa!
 
Sisi kwetu likizo ilikua kama camp ya mateso ni mwendo kwenda shamba hapo kulima, kuchimba mashimo ya kupanda migomba, kutifua & kupalilia pia kusomba majani hapo mpaka likizo iishe ushakua mweusi mweusi hivi
Lakini si ilikukomaza mkuu!
 
Nyie mlikuwa wa kishua
Sisi ukienda kwa bibi mtachota maji mtoni mtachanja kuni
Mtaenda shamba
Kukamua ng'ombe na kusafisha zizi
Michezo yetu ilikuwa rede,kombolela n.k
Mambo ya cd hatukuwa nayo ni mwendo wa VHS zile mnaangalia kwaya za kkkt Mkichoka mnaweka za kinaijeria au Neriaaa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…