kabla ya hapo mkuu watu walishaanza kujazwa kila kitu kipo yente mkuu
Una maana gani kusema walijazwa?
Hivi unafikiri watu kupinga uchaguzi ni 29 OCT pekee? Huko nyuma ilishatokea lakini haikuwa na nguvu..
Serikali ilikuwa imetofautina pakubwa na sehemu kubwa sana ya makundi...
Vyama pinzani
Taasisi za kidini -RC ,Kanisa la Gwajima, taasisi zingine...
Wanaharakati
Wananchi
Wanachama wa chama dola.
Watu kutoka vyombo vya ulinzi na usalama.
Hivi unategemea nini hapo?
Hayo makundi yote kwa mara ya kwanza katika historia waliungana kuipina serikali, kumbuka wafuasi wa Gwajima walivyofungiwa kanisa na kupigwa virungu kanisani, kumbuka wanachama wa CHADEMA waliopigwa mahakamani, kumbuka wanaharakati kutoka Ke na UG waliofanyiwa unyama baada ya kuja kusikiliza kesi ya Lissu.
Kumbuka pia wanachama wa CCM ambao walipinga kutofanyika kwa kura za maoni, kumbuka pia RC viongozi walichofanyiwa, kumbuka watu waliotekwa na kuuawa.... kumbuka kashafa za ufisadi na wizi... uonevu wa polisi n.k
Hayo matukio yote ndio yaliwapa hasira watu wakatoka 29 OCT, na hayo makundi yalikuwa na lengo moja... hivyo kila mmoja aliguswa kwa upande wake.
Kusema kwamba walijazwa si kweli... mtu kama hajaguswa hata umjaze vipi hawezi kuandamana, kama unasema Mange ndiye aliwajaza, unakumbuka alishaitisha maandamano wakati wa JPM, nani alitoka?
Hivyo raia walikuwa na hasira ndani kwa ndani, hivyo 29 OCT lazima tu kingenuka hata pasipo kujazwa...
Na kila kundi hapo kwa namna moja ama nyingine walichukizwa na muenendo wa serikali...
Na hilo suala halijaisha... ndio maana wanakuambia wafanye maridhiano, na watu hawataki maridhiano...