Nimekataa kumpongeza Mrisho Gambo

Nimekataa kumpongeza Mrisho Gambo

Kamwe Lowasa hatawatoka wana CCM kwenye vinywa vyao.Bila kumtaja Lowasa kikao au mkutano hauwezi kumalizika salama.Ni kwa nini?Mbona yeye hana habari nanyi kabisa.Naamini ataendelea kuwatesa kwa muda mrefu sana.Ni muda tu tusubiri.
 
gambo.JPG


Hivi umesema hii picha inatufundisha nini vileee?
 
MRISHO MASHAKA GAMBO,Kumbe uhasibu Arusha inatoa viongozi????? au ilikuwa ya zamani?
 
nasikitika kuona mbunge mzima una akili kama ya mtoto wa chekechea.

Sasa wewe mwenyewe umeshasema humjui vizuri alafu unammwagia sifa kibao na kumwamini kabisa ukksema hatakuangusha.

Hii imekaaje sasa

Ukiona hivi, tambua mara moja kuwa hizo ni porojo na uongo tu wa kufurahisha jamvi!!

Ninachoweza kusema kuhusu Juliana Shonza ni kuwa, she is good but not the best in propaganda!!

Amesahau kuwa ni huyu huyu Mrisho Gambo ndiye aliyewatukana wanawake wote wasomi wa sampuli yake Juliana kuwa vidigrii (shahada) zao hizo wamezipata kwa kuvua vyupi vyao!!.

Sina hakika kesi ilishaje dhidi ya huyu bwana maana alishitakiwagwa kwa kauli yake hii!!

Maana na tafsiri ya hiyo ni kuwa, hata shahada ya ...........aliyonayo Juliana Shonza hakuipata kwa halali bali kwa kuvua ovyo nanihi yake!!

Je,Juliana Shonza ana maana ya kuwa UJASIRI na UJEURI na KUJIAMINI (KUTOKUOGOPA) alionao huyu ndugu yake ni huu wa kutumia lugha chafu dhidi ya watu anaowaongoza na viongozi wenzake?...Hii ndiyo sifa bora ya kiongozi?
 
amesema "ameambiwa" kuhusu Gambo so probably atakuwa amepewa maelezo na akina lizaboni
 
Mnafiki saan huyu dada,eti anjiita Mlokole.Ukishaingia kwenye siasa za ulaghai na chuki pamoja na ufitini kama za CCM huwezi kujigamba kwa ulokole.

Ilikuwa ni kuchagua moja,utajili katka roho au fahari ya maisha katika mwili.Umechagua lililo moja na hakika huko ndio mahali pako.
Usitishike na neno Ulokole kiongozi maana hawa ndio wanaongoza kwa matendo machafu bora hata mtu asiye na dini lkn akaamini tu Mungu yupo
 
Na cha ajabu vijana hao hao wanaosifiwa kulelewa vizuri ndo waliouza Mali za chama kule iringa teh teh teh! Chama hiki hakiishi mikosi
Kati ya chama chako na CCM KIPI kina mkosi?!CCM ndiyo dume lako upende usipende na uukileta fyoko kina uwezo wa kukufanya kitakavyo chagadema ww!
 
Sijaelewa hata nini huyu dada anataka kukiwakilisha kwenye bandiko lake
Kwamba UVCCM na CCM kwa hujumla ndiyo inayotakiwa kupongezwa kwani imefanikisha kupatika kijana Gambo. Hata hivyo kama kweli Tume ya maadili kama inafaile lake la tuhuma na huyo mwanasheria amemfungulia kesi, hapo nadhani hilo ni doa kwa UVCCM na CCM kwa ujumla.
 
Kwa Katiba iliyopo tupo sahihi kwa kila jambo.
Kujitosheleza haitoshi je knaheshimiwa? Ndo maana nimekwambia ukaidadavuzi mkuu ili ikibidi iendane na kasi yenu kasi ya matamko, kila siku as if matamko yanaendeshe serikali badala ya katiba kuendesha serikali na nchi kiujumla
 
Kwamba UVCCM na CCM kwa hujumla ndiyo inayotakiwa kupongezwa kwani imefanikisha kupatika kijana Gambo. Hata hivyo kama kweli Tume ya maadili kama inafaile lake la tuhuma na huyo mwanasheria amemfungulia kesi, hapo nadhani hilo ni doa kwa UVCCM na CCM kwa ujumla.
Na iyo kesi haitokuja kwisha kama mapka leo ni miaka na hukumu yake bado inatafutwa!
 
Hakika,umenena kweli.CCM bado itaedelea kutoa viongozi mbalimbali wa nchi hii kwa karne nyingi zijazo...na hata kwa upande wa upinzani wataendelea kupata wagpmbea wa nafasi mbalimbali kuanzia mashinani hadi uraisi kutoka CCM...hili halina ubishi.

Kama CCM inajiamini mbona wanaiba kura? Wenye kujua viongozi mahiri ni wananchi na siyo CCM kujigamba yenyewe.
 
“TUNATAKA kuona taifa hili likiwa na vijana jeuri na wenye kujiamini, wasiwesi vijana waoga aina ya ‘ndiyo’ bwana, mkubwa; vijana wenye ujasiri wa kuhoji na kupiga vita mifumo ya jamii isiyoshabihiana na matakwa na matarajio ya jamii ya Kitanzania. Tunataka vijana wenye misimamo thabiti dhidi ya mifumo kandamizi, ubwana na ufisadi katika taifa,”

Haya ni maneno aliyopata kuyanena, Hayati Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.

Siku moja wakati nasoma Biblia nilikutana na ujumbe wa Mwanzo 45:5, ulisema “Yusufu akawaambia kaka zake, ingawa ninyi mliniuza ila Mungu alikusudia kunitanguliza ili niwasaidie”

Maendeleo ama mabadiliko katika nchi yoyote yanaletwa pale kunapokuwapo na watu walio tayari kuishi maisha ya kujitoa, watu ambao wanaamini kuwa wanao wajibu mkubwa kwa jamii yao.

gambo.JPG


Kimsingi mimi simfahamu sana na sina maelezo mengi kuhusu mtu niliyeamua kumzungumza leo mwenye jina la MRISHO MASHAKA GAMBO, maana yeye akiwa kwenye Umoja wa Vijana wa CCM kama mjumbe wa Baraza Kuu la UVCCM 2008 – 2012 kutoka Mkoa wa Arusha, mimi nilikuwa BAVICHA, wakati mimi nikijiunga na UVCCM na CCM mwaka 2013 mwanzoni yeye alikuwa ameshateuliwa kuwa DC wa Korogwe (akiwa DC wa Kwanza kwa wakati huo kubeba matofali na kushiriki kujenga shule na zahanati na Wananchi). Hivyo ni mtu ambaye nimekuta maneno yaliyovumisha sifa yake lakini sikupata bahati ya kumfahamu vizuri.

Lakini maneno niliyoyakuta ambayo yanamuelezea GAMBO yalishabihiana sana na maneno ya Mwalimu niliyoyanukuu, kuwa GAMBO ni Kijana JEURI, JASIRI na ANAYEJIAMINI.

Nimeambiwa katika historia ya maisha yake, halijawahi kutumika neno la MUOGA, kumuelezea juu ya wajihi wake na sifa yake…wala yeye mwenyewe hajawahi kusikika katika maisha yake akitamka neno NAOGOPA, ni Kijana anayehoji kwa HOJA.

Lakini hayo ni tisa, Kumi Mrisho Gambo ni Icon kamili ya Mwanamapinduzi anayechukia mifumo kandamizi, mifumo ya Ubwana na UFISADI. Historia yake inatueleza hivyo, alimkataa Mhe Lowassa ingawa alikuwa anatoka nae Mkoa mmoja tangu akiwa UVCCM kwa sababu moja kuu UFISADI.

Kwenye title ya andiko langu nimesema nimekataa kumpongeza Gambo, ni kweli nimekataa..!! Maana sio kwa juhudi za Mrisho pekee ndizo zilizomfikisha hapo bali malezi mazuri yanayotolewa na CCM na UVCCM kwa vijana wake ndio yaliyofanikisha kuwapata Mawaziri kama akina Makamba, Mavunde, Masauni na wengineo, ni mazao ya UVCCM yaliyotuletea wakuu wa Mikoa mahiri kama akina Makonda, Gambo, Mtaka na wengineo pamoja nao Ma-DC katika maeneo mbalimbali ya Nchi yetu. Kwa malezi haya nimeamua kuipongeza UVCCM na CCM na kukataa kumpongeza GAMBO.

Ni CCM pekee inayojenga Vijana majasiri wanaoweza kuwahoji Viongozi wao hadharani, katika historia yake GAMBO alipishana mawazo na kuhoji hadharani juu ya Lowassa, alihojiana na Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Tanga na wakubwa wengine pale alipoona wanaenda kinyume na matakwa na matarajio ya jamii yetu, Jamii yetu ina kiu ya Maendeleo, Kiongozi yeyote anayekwamisha maendeleo katika eneo ambalo GAMBO yupo basi huyo amejitangazia Vita na Uadui mkubwa na Kijana huyu. Daima alitaka kuona haki ikitendeka na wananchi wanahudumiwa. Hata hivi karibuni Yule jamaa wa M4C wa Arusha Mjini alipotaka kupima ubavu, alijikuta kadondokewa na kitu kizito chenye ncha kali (maana sasa hivi Serikali imepiga marufuku zile posho zao za kifisadi) Ni CCM na UVCCM sio CHADEMA, sio BAVICHA wenye uwezo wa kutoa Vijana makini na wasio waoga na mabwana ndio Mzee. Wao ni Vijana wa kusubiri maelekezo na kutumwa kubweka.

Mungu amemchagua na kumuinua GAMBO, akamtenga mbali na dhulma na wafitini. Ni kama ilivyo kwa Yusuph, MUNGU ameamua kumtanguliza Gambo ili awasaidie. Mkoa wa Arusha unakufa, biashara zimesimama, utalii unadorora, mahoteli yanafungwa kwa sababu za kipuuzu na upuuzi wa mtu mmoja na kijikikundi chake, MUNGU amemuinua GAMBO ili awasaidie kuirudisha heshima ya ARUSHA.

Nimekataa kumpongeza GAMBO lakini nitakuwa mchoyo wa fadhila nisipomshukuru na kumpongeza Mhe John Pombe Magufuli kwa kuendelea kuwaamini vijana na kuwapa nafasi, hakika mimi nachukua ahadi kwako kwa niaba yao kuwa HATUTOKUANGUSHA.
Hahahahah si kwa kujikomba huko lakin jitahidi anaweza kutenguliwa mwingine!!!!
 
Oneni majibu ya wana UKUTA! Eti haya wanayo jibu hapa ndio mawazo yao mbadala wa ccm.
Huo ni uono wako hafifu si kila anayekupinga ni mpinzani, kuna muda mwingine watanzania tuache unafiki wa kumng'ong'a mtu kisogo, akiwepo unamkubali akigeuza kichwa tu unaanza manung'uniko! Si kila anayechangia hapa ana interest na UKUTA jifunze kusema ukweli binafsi na sio ukweli wa chama
Nyie ndo kina Mkuu wa mkoa wa Rock city nyie
"Tutayafanyia kaz maagizo ya Rais hivyo hivyo yalivyo, hatutaongeza akili zetu" Aug.17,2016
 
Kati ya chama chako na CCM KIPI kina mkosi?!CCM ndiyo dume lako upende usipende na uukileta fyoko kina uwezo wa kukufanya kitakavyo chagadema ww!
Bahati mbaya umenielewa ndivyo sivyo! Aliyekwambia mimi Nina chama ni nani? Usikimbilie vitisho na kutukana jibu hoja hawajaiba? Kwaiyo tumuamini nani wewe au wale waliotangaza kuwa iringa kumeibiwa hahahaaa mimi sina chama ndugu yangu ni mbena kwa asili ya kabila langu naizungumzia iringa yangu sasa huko chagadema ndo wapi mkuu!?
 
Ni kweli Juliana Shonza, nakubaliana na wewe 100% CCM ni chama pekee cha kuzalisha viongozi bora nchini mwetu
Viongozi bora kwa kutumia vigezo au kipimo gani? Sio huyo RC wa Dar es Salaam aliyempiga mzee Warioba? Sio huyo mteule Rc wa Arusha aliyekuwa na kesi bwerere tume ya maadili ya umma ikiwemo ya kumtukana mwanasheria wa halmashauri kuwa ana digrii ya chupi? Mapungufu ya mamlaka ya uteuzi msiitumie kuhalalisha kuwa ndani ya CCM kunazalishwa viongozi bora. Na kwa uhakika, naomba hili ulichukue-kuna viongozi ndani ya CCM ambao wanatambulika kwa uadilifu wao, kama ndio wangekuwa na mamlaka ya uteuzi hao mnaoshangilia kuteuliwa kwao hata kwenye "reserve" wasingegusa! Endeleeni kushangilia staili hii ya uteuzi wa watu wasio na chembe hata ya maadili ila mjue CCM ndio inazidi kuizamisha nchi kwa habari ya maadili, muda utasema!
 
Huyu Binti nilifikiri matatzo yake yameisha kumbe bado..
 
Back
Top Bottom