Ethos
JF-Expert Member
- Aug 1, 2015
- 2,294
- 2,090
Juliana Shonza
Unataka kutuaminisha kuwa '' mfumo '' sasa hivi ni msafi.. Inawezekana. Ila tatizo ni kuwa Kuna '' mfumo '' mwingine unajengeka ambao unaweza kuwa hatari zaidi ya ule wa kwanza.
Unataka kutuaminisha kuwa '' mfumo '' sasa hivi ni msafi.. Inawezekana. Ila tatizo ni kuwa Kuna '' mfumo '' mwingine unajengeka ambao unaweza kuwa hatari zaidi ya ule wa kwanza.
Ni kweli Juliana Shonza
Humfahamu Mrisho Gambo,na nashangaa unatowaje sifa kwa mtu usiyemfahamu.Mrisho kweli ni jeuri,ana kiburi na matusi ya nguoni.Hata wewe ukikaa vibaya lazima akutukanie hata mzazi wako.
Ingekuwa vema ungekaa kimya kuliko kujipendekeza wakati humjui Gambo.Wewe unayejiita mwanamke mpambanaji inabidi ujipambambanue,maana wanawake wenzako alikopita Gambo kama kiongozi wamedharirishwa sana,kuanzia Korogwe mpaka Uvinza.
Nilidhani utamuonyaa aachane na tabia za matusi....Hapa chini ni ushahidi wa wanawake wenzake,wenye kuzunguka round about kila mwezi walivyoshuhudia tabia mbovu za huyo unayemsifia.
"Mhe. Gambo analalamikiwa na Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma kwa Matumizi mabaya ya uongozi yakiwemo matumizi ya lugha chafu, kukiuka sheria mbalimbali pamoja na ubabe wakati wa kutekeleza majukumu yake kama Mkuu wa Wilaya ya Korogwe
Pia Shahidi huyo alidai kuwa Mkuu huyo wa Wilaya aliwahi kumtukana hadharani matusi ya nguoni Mtumishi mmoja wa kike wa Halmashauri ya Mji wa Korogwe ambaye alikuwa ni Mwanasheria wa Halmashauri hiyo na kupelekea mtumishi huyo kufungua kesi Mahakamani dhidi ya Mkuu huyo wa Wilaya, kesi ambayo alidai bado inaendelea mpaka sasa
Kwa mujibu wa Mhandisi Mwahalende, katika kipindi hicho utendaji wa Mkuu huyo wa Wilaya haukuwa mzuri kwa mambo ambayo yeye mwenyewe ameshuhudia ambayo ni pamoja na lugha chafu ambayo haistahili kuzungumzwa na Kiongozi, Utawala wa mabavu na amekuwa ni kikwazo cha maendeleo ya Halmashauri ya Wilaya ya Korogwe kwa kukwamisha miradi mbalimbali ya maendeleo"