Nimeipenda sana Sumbawanga

Nimeipenda sana Sumbawanga

Kwenye kati ya mwaka 2003 au 2005 kuna kijiji kinaitwa kalampanzite mwewe alibeba dume la ng'ombe alafu akawa anadondosha mifupa tu chini,

Mean while nina mwezi wa sita kikazi huku lakin sijawahi kutana wala kushuhudia hayo mambo, nadhani ilikua zamani
Duuuh!! Iyo ishu ilitutisha ata sisi wazawa wa huku aiseee
 
sumbawanga hakuna uchawi kama watu wanavyofikiria mimi nimezaliwa ngorotwa kijiji walichovumisha kuwa mwewe kabeba ng'ombe, s/m mpui maeneo ya stendi ss kaengesa seminari advance kantalamba sijawai sikia au kuona mtu kafa kwa kulogwa.
 
Tofauti na mikoa mingine huku maisha ni nafuu sana

Pia kuna fursa za aina tofauti hasa kilimo uvuvi na mifugo

Gharama za ujenzi ni nafuu.

Na hali ya hewa ni nzuri kupindukia

Nafikiri kustaafia Sumbawanga

Kuanzia Laela,Mpui,Tamasenga mpaka Luiche kila kitu ni kinono hasa kwa sisi tupendao chicha la asili.

Karibu mjionee hakuna taabu ya foleni,maji kelele wala uchafuzi wa mazingira.

Halafu tunapakana na nchi mbili Congo na Zambia

Kama kichwa yako haina mchanga mchanga na inawaza mema hii ndio sehemu ya kukimbilia.

Haiwezekani atoke binti Kenya anunue ardhi na kuwekeza na wewe umekaa hapo Dar unawaza mambo ya Dushe na papuchi.

Anatumia hati ya Ardhi yake kukopa ma bilioni
kijana amka hapo.

IMG_0543.jpg


Hakuna foleni
njoo huku.


Barabara%2BSumbawanga.jpg


Ukichelewa shauri zako.

57195139.jpg


Plot utapata kwa sh laki tatu..

Sasa unafanya nini huko mjini?

Majuto ni mjukuuu

Nzalendo UBARIKIWE Mkuu Kwa Uzalendo wako.Hiyo Ni habari nyeti halafu wako vijana wanaleta kejeli.
Asante sanaaaaa
 
nani anataka kulogwa wewe? kaa peke yako ushalogwa wewe, Jina lenye ni sumba alafu wanga uanjua maana yake wewe?

aujui kwa nini pinda hayupoo uko ameishia kuishi Kongowe DSM? jiulize waziri mkuu kukimbia kwao, wewe Mwalimu wa NASARY unajitia kutuita ebu risiti paper upande grade walau uwe mwalimu wa msingi alafu nitafte nikufanyie mpango uame uko

Mkuu, mimi nashida ya kufanya mpango wa kuhama Kituo cha Kazi..Nataka kuhamia DODOMA(RAS DODOMA).....
Naomba tuwasiliane( nimejaribu kukutafuta PM imegoma)
Thanks in Advance
 
Mkuu, mimi nashida ya kufanya mpango wa kuhama Kituo cha Kazi..Nataka kuhamia DODOMA(RAS DODOMA).....
Naomba tuwasiliane( nimejaribu kukutafuta PM imegoma)
Thanks in Advance
Umeamini biti alilompiga mwenzie hadi uombe akuunganishie uhamisho?
 
Mleta mada usipende kuwatoa wenzako toba. Kama umekula hela za wafipa tafadhali warudishie wenyewe usitake kutuuza kwa kutuambia tuje huko kutafuta maisha wakati wafipa wenyewe kina Mzindakaya, Pinda wamekukimbia kwao. Huko noma aisee, watu wanafanya shopping chini ya ziwa Tanganyika na kwenda juani (sayari ya jua) kununua radi ya kuwapigia adhabu wenzao, si hatari hii? Baki peke yako huko na roho yako ngumu.
Mzindakaya amewekeza ana Ranch kubwa..pia ana Export nyama mkuu
Pinda amewekeza sana kwenye kilimo
Huku kuna fursa sana mkuu,kimyakimya
Kuna mabinti wametoka Kenya na wamewekeza huku kwenye ardhi,
Changamka mkuu kabla hapajakucha.
 
Tatizo ni mbali sana na Tanzania(Dar)
Kuna watoto ,tena wa Kike wametoka Kenya na wanachangamkia fursa huko.....
Kati ya wajukuu zao na wajukuu wako.... nani atafanya kazi kwa mwenzake?
 
kiwanja laki 3... huko hasara tu sio kwa kuwekeza..

tanzania sehem ya kuishi ni dar tu.. kwingine kusogeza siku tu au kutafuta riziki tu.. hata mkuu wa kaya anaishi posta hapo
Mkuu Dhamani ya Ardhi hupanda kila mwaka.
 
Kuna watoto ,tena wa Kike wametoka Kenya na wanachangamkia fursa huko.....
Kati ya wajukuu zao na wajukuu wako.... nani atafanya kazi kwa mwenzake?
Kwani maisha yapo sumbawanga tu,hilo swali jiulize wewe unaokaa nao huko sumbawanga...
 
Nimezaliwa huko nikasima.hapo jangwani primary then nikaenda mazwi sec sumbawanga pazuri sana aisee kung'andaaaaa nimemiss migebukaaaaaa ile mbaya
 
Back
Top Bottom