Nimeikuta kwenye Facebook hii..

Nimeikuta kwenye Facebook hii..

supermario

Member
Joined
Dec 2, 2011
Posts
48
Reaction score
15
Status 1 ikiwa ndefu hawasomagi, ila mtu huyo huyo atasoma fupi fupi mia!:

Mnisamehe kama ntakuwa mkali kidogo, ni hivi, kama kilicho ndani ya nyumba thamani yake haifiki laki, nawe una milango miwili, huwezi enda nunua kufuli mbili za laki laki. Kimantiki, gharama ya ulinzi (laki mbili za kufuli) isizidi kinacholindwa nazo. Mfano Jakaya analindwa kwa mamilioni kila siku, kwa sababu mpuuzi akitokea na kumuua, Uchaguzi mpya utatakiwa na utatugharimu sana, gharama kubwa kuliko ulinzi wake, pia 'hadhi' ya jeshi na jina letu kimataifa litashuka, hata utalii utashuka, mtalii gani atapenda aende nchi ambayo wameshindwa hata kumlinda Rais wao? Itakula kwetu. Kimantiki, Msafara wa JK unastahili uwe wa askari wa hali ya juu na watumie kila zana kumlinda. Ni lazima. Hata kama mie ni Chadema, nasema JK alindwe na Makomandoo hasa, hapa ni uchumi na sio siasa ama vyama - maslahi ya Taifa.
.
Sasa iweje likampuni likubwaa liandae futari ya yatima 50, halafu waje waandishi wote wa habari -tv, radio hadi magazeti na magari yao spesheli, (ofkozi na wablogu pia - wa blogu aje mmoja tu wengine watapesti), polisi nao haooo kibao kulinda tukio la watoto 50 kulishwa futari ya nusu saa, wakati futari sahani buku2, sahani 50 ni laki tu. Gharama ya kuita waandishi ni mamilioni, futari laki, usaniii!
.
Hii nchi ni ya kisanii sana, ofisi ya sirikali ndani ina benchi na meza na kijifaili cabin tu, ila inalindwa na Kampuni Kubwa kabisa ya Ulinzi na inalipwa malilioni kwa mwezi, kisa kampuni anaimiliki Boss wa serikalini, ela inarudi kwake.
.
Tusiiseme serikali tu, na we dada kamshahara laki3 umehongwa gari umekubali, unaenda nalo job kila siku kutishia wenzio wajione si kitu, mafuta na service ya gari kwa mwezi ishapita hako kamshahara, unamudu vipi maisha kama sio msaniii na wewe? Na kaboyfriend chako nacho wala hakajashtukia kanachezewa game! Ila kiboy nacho si ni kisanii pia maana kina wengine mtaani. Usanii usanii tu ndo iliyobaki khabari ya mujini!
 
Status 1 ikiwa ndefu hawasomagi, ila mtu huyo huyo atasoma fupi fupi mia!:

Mnisamehe kama ntakuwa mkali kidogo, ni hivi, kama kilicho ndani ya nyumba thamani yake haifiki laki, nawe una milango miwili, huwezi enda nunua kufuli mbili za laki laki. Kimantiki, gharama ya ulinzi (laki mbili za kufuli) isizidi kinacholindwa nazo. Mfano Jakaya analindwa kwa mamilioni kila siku, kwa sababu mpuuzi akitokea na kumuua, Uchaguzi mpya utatakiwa na utatugharimu sana, gharama kubwa kuliko ulinzi wake, pia 'hadhi' ya jeshi na jina letu kimataifa litashuka, hata utalii utashuka, mtalii gani atapenda aende nchi ambayo wameshindwa hata kumlinda Rais wao? Itakula kwetu. Kimantiki, Msafara wa JK unastahili uwe wa askari wa hali ya juu na watumie kila zana kumlinda. Ni lazima. Hata kama mie ni Chadema, nasema JK alindwe na Makomandoo hasa, hapa ni uchumi na sio siasa ama vyama - maslahi ya Taifa.
.
Sasa iweje likampuni likubwaa liandae futari ya yatima 50, halafu wa
je waandishi wote wa habari -tv, radio hadi magazeti na magari yao spesheli, (ofkozi na wablogu pia - wa blogu aje mmoja tu wengine watapesti), polisi nao haooo kibao kulinda tukio la watoto 50 kulishwa futari ya nusu saa, wakati futari sahani buku2, sahani 50 ni laki tu. Gharama ya kuita waandishi ni mamilioni, futari laki, usaniii!
.
Hii nchi ni ya kisanii sana, ofisi ya sirikali ndani ina benchi na meza na kijifaili cabin tu, ila inalindwa na Kampuni Kubwa kabisa ya Ulinzi na inalipwa malilioni kwa mwezi, kisa kampuni anaimiliki Boss wa serikalini, ela inarudi kwake.
.
Tusiiseme serikali tu, na we dada kamshahara laki3 umehongwa gari umekubali, unaenda nalo job kila siku kutishia wenzio wajione si kitu, mafuta na service ya gari kwa mwezi ishapita hako kamshahara, unamudu vipi maisha kama sio msaniii na wewe? Na kaboyfriend chako nacho wala hakajashtukia kanachezewa game! Ila kiboy nacho si ni kisanii pia maana kina wengine mtaani. Usanii usanii tu ndo iliyobaki khabari ya mujini
!

Usanii ndio kazi iliyobakia kila kitu siku hizi usanii.....ila imekaa vizuri inshu ndogo waandishi wa habari na jamaa zetu wa blog....mimi huwa naumiza kichwa hawa wanaowadhamini hawa jamaa wenye blog hizo hela kwanini wasizipeleke kwenye misaada na kujitangaza kuliko kudhamini blog zilizokosa dira
 
Una mantiki ndani ya maneno haya ukiyatafakari kwa kina!
Haya ngoja tuwaache akina Kongosho, Mrembo by Nature, lara 1 na washirika wao waje maana nasikia hawa wote niliowataja wamehongwa magari ya rangiu nyekundu.
 
Last edited by a moderator:
mbona shirika la ndege la tanzania liko na ndege moja ya mkopo lakin wafanyakaz zaid ya 200 tena wana office kenya na uganda pia.
 
Back
Top Bottom