Wala usihangaike tafuta mpemba mwambie afanye Mambo...na hapo waliokuibia ni watu wanaokujua
Kaa Kwanza utulie ndo urudiHabari wana jamvi,
Naandika nikiwa na jazba na hawa watu wanaoitwa wezi. Nimepanga geto langu nikajibana nikaeka vitu vyote vya ndani sasa hawa jamaa wamenilia time nimetoka wamenisafisha hadi kijiko ila kwenye vitu walivoiba wamebeba hadi king'amuzi.
Ila kuna mdau aliyeniambia king'amuzi kinatafutika kama ilivyo kwa simu.
Msaada jamani kwa mwenye ujuzi maana nikimpata mwenye king'amuzi ndio nitamtolea uvivu.
Nawasilisha
Duh....Njoo nikupeleke handeni sehemu moja inaitwa kwamsisi,hivyo vitu vinarudi ndani ya saa 24 na wezi wakishavirudisha vyote wanasahau njia wanawashwa mwili mzima wanajikuna mpaka wanatoka damu,watazunguka eneo Hilo hapo kwako huku wanajikuna na kulia kwa uchungu mpka wewe useme either waondoke lakini umewasamehe au waondoke ila hujawasamehe.Mimi binafsi nilisema waondoke ila sijawasamehe,haikupita wiki wakaugua uchizi,ndani ya mwezi kila mmoja alikufa kwa kifo chake(walikua wanne)
Itakua njoro au pasuaPole sana runtown
Moshi sehemu gani?
Report hicho king'amuzi watakamatwa tuu
moshi
Wezi wapo ila hii habari ya watu kubeba hadi vijiko huwa inatokea maeneo flani flani sasa kama mji wa kijanja kama Moshi una mambo hayo sijui.Au kuna demu wako kaamu kubeba vitu ahame navyo maana hali ni tete.
Imeongezeka Rau siku hizi, saa 12 jioni mtu analizwa
Buza hakufaiHabari wana jamvi,
Naandika nikiwa na jazba na hawa watu wanaoitwa wezi. Nimepanga geto langu nikajibana nikaeka vitu vyote vya ndani sasa hawa jamaa wamenilia time nimetoka wamenisafisha hadi kijiko ila kwenye vitu walivoiba wamebeba hadi king'amuzi.
Ila kuna mdau aliyeniambia king'amuzi kinatafutika kama ilivyo kwa simu.
Msaada jamani kwa mwenye ujuzi maana nikimpata mwenye king'amuzi ndio nitamtolea uvivu.
Nawasilisha
Umeulizwa maeneo gani.moshi
Pole sana mkuu,
Huu ni wakati mgumu ambao ni wewe ndio unajua uchungu wake kuliko yeyote.
Usiache kutoa taarifa kwa mamlaka za kisheria kuanzia ngazi ya mtaa hadi Polisi.
Utaambiwa mengi,Lakini baada ya taratibu hizo Usiache kumshukuru Mungu kwa mtihani aliokupa.
Naamini wameiba vitu,Ila hawajaiba Akili,nguvu na uthubutu uliokufanya kupambana na kujikusanya hata ukajipongeza kwa kuwa na vitu vyako mwenyewe.
Kuna siku maisha baada ya mtihani uliokupata.
dawa ya Moto ni Moto hata huyo alieiba Hadi nzi ni mshirikinaHuu ushirikina sasa!