Nimeibiwa vitu vyote vya ndani

Jamani Mimi sio mganga! Nataka nimdirect sehemu,na uzuri atalipa baada ya kufanikiwa akichuna yatakayomkuta tusitafutane humu.
Muwekee huko unakomdirect hapa, au ni siri!?
😆😆😆😆
 
Habari wana jamvi,

Naandika nikiwa na jazba na hawa watu wanaoitwa wezi. Nimepanga geto langu nikajibana nikaeka vitu vyote vya ndani sasa hawa jamaa wamenilia time nimetoka wamenisafisha hadi kijiko ila kwenye vitu walivoiba wamebeba hadi king'amuzi.

Ila kuna mdau aliyeniambia king'amuzi kinatafutika kama ilivyo kwa simu.

Msaada jamani kwa mwenye ujuzi maana nikimpata mwenye king'amuzi ndio nitamtolea uvivu.

Nawasilisha
Daah pole mwamba usipanik nenda karipot mamlak husik watajua cha kukusaidia
 
Hii kitu ina ukwel , nikiwa Mwanza Mzee nilikuwa na gheto boss , siku moja nikaopoa manzi , nikamwingiza gheto mara ya Kwanza , nikarudia tena mara ya pili daah..... ma- Mae baada ya sku mbili Mzee nikachapwa deki , ....

Mwamba kuona hvyo nikaona isiwe tabu, nikahamisha kila kitu nikabakiza kitanda Tu , niliahrisha na kununua vitu vingine mpak nilipopata nyumba ya kueleweka a.k.a Geti Kali kuna mbwa mkali..... Nahs Yule manzi aliwaelekeza wajuba aisee
Inaweza ikawa mbaya zaidi ukasimikiwa hata madawa ya kulevya chief.
 
Muwekee huko unakomdirect hapa, au ni siri!?
😆😆😆😆
😂Ni kosa kuweka contact zake nimemcheki huyo Mzee hajapokea akikubali nitaweka.Nimekuelewa unachomanisha.
 
King'amuzi japo process ndefu kinatafutika,,nenda startime au dstv au azam,,tokana na ni cha kampuni gani,,
Wenyewe wanajua namba za simu zinazokilipia hicho king'amuzi..
 
Wezi wapo ila hii habari ya watu kubeba hadi vijiko huwa inatokea maeneo flani flani sasa kama mji wa kijanja kama Moshi una mambo hayo sijui.Au kuna demu wako kaamu kubeba vitu ahame navyo maana hali ni tete.
Sina demu mkuu nina mke
 
Nenda polisi kichukue RB,halafu wapatie namba ya king'amuzi chako watakupa mpelelezi mtaenda nae kama ni Azam,startimes nk mwisho wa siku watakifuatilia king'amuzi na mwizi wako utampata utasema ameiba na hata asivyoiba
 
Pole sana, hao wezi wanarudisha sana maendeleo ya watu nyuma
Habari wana jamvi,

Naandika nikiwa na jazba na hawa watu wanaoitwa wezi. Nimepanga geto langu nikajibana nikaeka vitu vyote vya ndani sasa hawa jamaa wamenilia time nimetoka wamenisafisha hadi kijiko ila kwenye vitu walivoiba wamebeba hadi king'amuzi.

Ila kuna mdau aliyeniambia king'amuzi kinatafutika kama ilivyo kwa simu.

Msaada jamani kwa mwenye ujuzi maana nikimpata mwenye king'amuzi ndio nitamtolea uvivu.

Nawasilisha
 
Waganga uwa mna wapata wapi. Maana nawatafta ila siwaoni
Waganga wa siku hizi matapeli tu kuna kipindi niliibiwa nikashauriwa nilete mtaalamu alichimbia kuku weusi kila kona ya uwanja na katikati ya uwanja hadi leo majizi yanaishi nilikuja kuwakamata kwa mfumo mwingine kabisa.
 
Pole sana Mkuu

Piga maombi Mungu atazungumza nao tuu... au kama vipi tafuta mtaalamu haswa awaguse kidogo tuu yatembee barabarani yakijikojolea.

Au yakilala yakose usingizi kazi iwe ni kujikuna hadi asubuhi.
Kuna mmoja huwa anasema hiyo ni kazi ndogo tu! Tunamfunga mkojo kwa wiki 1 tutaona ataenda kukojolea wapi!!!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom