Mmasai Wangu
Member
- Jul 22, 2021
- 19
- 77
Habarini wana Jamii Forums!
Kwa wanao fahamu maisha ya Dar ... kumkutaa mwanamke mwenye mtoto stendi pamoja na mabegi yake na hana pa kwenda ni jambo la kawaida!
Kuna mwamba hapa alitokea zake kwenye mizunguko akafika rangi tatu pale ( mbagala zakiem ) kutokana na uhaba wa usafiri hasa kwa wakaazi wa kisemvule na vikundii jamaa aliamua kuvuta vuta mdaa kwa kuzunguka kidogo huku akisubiria kupungua kwa watu kugombania gari kwa ajili ya usafiri
Basi katika pita pita zake kakutana na mdada yeye alikua mfanyakazi wa ndani ... katiwa mimba na mpenzi ! mwishowe alipokuwa anafanyia kazi zake za ndani wakamtimua ! Yule dada alikua anahangaika kumtafta yule mpenzi wake ila hakupatikana ! Na alipopanga kakuta mshikaji kashahama na kukimbia.
Yule dada kutokana na msongo wa mawazo alikua stendi ana lia hajui cha kufanya ! Sasa yule mwamba katika kupita akaona isiwe kesi ngoja ajaribu kuuliza huenda atapata mkasa zaidi ya kinachofanya binti alie !
Baada ya jamaa kupata mkasa akaona isiwe tabu akamchukua akampeleka kwake ! Hawakufanya chochote ndani ya siku 4 ... walipika na kupakua na walilala kitanda hicho hicho.
Yule jamaa akawa anajifikiria sana maana tabia za yule binti zilionyesha ni mwema ! Ila ikumbukwe ndani ya hizo siku 4 jamaa alikua anawasiliana na ndugu upande wa mwanamke ili kujichanga kupata nauli maana yule dada ni mtu wa bukoba!
Basi baada ya siku ya nne yule dada kutokana na aibu zake akaona ampee jamaa tunda ili iwe kama shukrani ! Basi ikawa hivo pika pakua na siku zikaenda. Baada ya siku tatu hivi yule dada aliondoka kwa shangazi yake yupo tanga !ila kutokana na maisha ya kijijini magumu alimuomba jamaa arudii maana alikuwa na njaa kali na yeye ni mjaa mzito. Wale ndugu kwa kuwa walipata taarifa kuwa kuna mtu alijitokeza kumsaidia basi walimruhusu maana hali zao zilikua duni.
Basi yule jamaa kalea mimba mpaka binti kajifungua hapo ndo shida ilipoanzia Yule binti akaondoka kwa shangazi zake na alipofika alikua anadai yule jamaa ni katili hafai na ashapata mwanamke mwingine ! Maneno kibao akaongea ! Ila jamaa upande wa pili hajui ! Sasa kama unavojua mhaya ni mhaya tu na siku zote unaambiwa usimwamini mwanamke ! Yule binti kumbe siku zile alivokua analia pale stendi yule jamaa hakuwa wakwanza kujitokeza kusaidia kuna mwamba pia alijitokeza kabla na kumpaa yule dada elfu 50 na namba za siku
Yule dada alichokifanya akatoroka kutoka kwa shangazi yake mpaka kwa yule mwamba wa kwanza ! Sasa alipofika akaelezea kwamba siku zote alikuwa kwa shangazi yake. Basi wakapika wakapakua na jamaa akawa anakula mzigo kama kawaida ila baada ya mudaa yule binti akamtafta yule jamaa alie lea mimba na kumwambia yupo kwa shangazi anateseka hali ngumu na mtoto anaumwa kila siku kutokana na jamaa hajui chochote basi akamrushia nauli aje mpaka kwake vikundu.
Pika pakua jamaa akawa anakula nayeye mzigo ! Ila baada ya mdaa kwenye kukosana ambalo ni jambo la kawaida yule mwanamke alisomba vitu vyote vya jamaa na kuondoka huku jamaa akiwa kazini !
Jama alivorudii kufika vikindu akakuta chumba empty na deki kapigiwa ! Hapo jamaa alijifunza usimwamini mwanamke usie mjua na usije ukapenda mwanamke kwasababu ety ana hali ngumu kwao ndo atatulia
Jamaa yupo ila anahitaji arudishee vitu vyake vya ndani jee afanyeje maana huyo binti bado yupo huku huku dar anahangaika nyumba baada ya nyumba ?
Na ndugu zake wamedai wataftafta na watamkamata ili arudishe vitu jee jamaa akitoa taarifa polisi itafaa ?
Au kuna mbinu gani ya kuvirudisha ??kwa ambao washawai kupitia matatizo kama haya??
Kwa wanao fahamu maisha ya Dar ... kumkutaa mwanamke mwenye mtoto stendi pamoja na mabegi yake na hana pa kwenda ni jambo la kawaida!
Kuna mwamba hapa alitokea zake kwenye mizunguko akafika rangi tatu pale ( mbagala zakiem ) kutokana na uhaba wa usafiri hasa kwa wakaazi wa kisemvule na vikundii jamaa aliamua kuvuta vuta mdaa kwa kuzunguka kidogo huku akisubiria kupungua kwa watu kugombania gari kwa ajili ya usafiri
Basi katika pita pita zake kakutana na mdada yeye alikua mfanyakazi wa ndani ... katiwa mimba na mpenzi ! mwishowe alipokuwa anafanyia kazi zake za ndani wakamtimua ! Yule dada alikua anahangaika kumtafta yule mpenzi wake ila hakupatikana ! Na alipopanga kakuta mshikaji kashahama na kukimbia.
Yule dada kutokana na msongo wa mawazo alikua stendi ana lia hajui cha kufanya ! Sasa yule mwamba katika kupita akaona isiwe kesi ngoja ajaribu kuuliza huenda atapata mkasa zaidi ya kinachofanya binti alie !
Baada ya jamaa kupata mkasa akaona isiwe tabu akamchukua akampeleka kwake ! Hawakufanya chochote ndani ya siku 4 ... walipika na kupakua na walilala kitanda hicho hicho.
Yule jamaa akawa anajifikiria sana maana tabia za yule binti zilionyesha ni mwema ! Ila ikumbukwe ndani ya hizo siku 4 jamaa alikua anawasiliana na ndugu upande wa mwanamke ili kujichanga kupata nauli maana yule dada ni mtu wa bukoba!
Basi baada ya siku ya nne yule dada kutokana na aibu zake akaona ampee jamaa tunda ili iwe kama shukrani ! Basi ikawa hivo pika pakua na siku zikaenda. Baada ya siku tatu hivi yule dada aliondoka kwa shangazi yake yupo tanga !ila kutokana na maisha ya kijijini magumu alimuomba jamaa arudii maana alikuwa na njaa kali na yeye ni mjaa mzito. Wale ndugu kwa kuwa walipata taarifa kuwa kuna mtu alijitokeza kumsaidia basi walimruhusu maana hali zao zilikua duni.
Basi yule jamaa kalea mimba mpaka binti kajifungua hapo ndo shida ilipoanzia Yule binti akaondoka kwa shangazi zake na alipofika alikua anadai yule jamaa ni katili hafai na ashapata mwanamke mwingine ! Maneno kibao akaongea ! Ila jamaa upande wa pili hajui ! Sasa kama unavojua mhaya ni mhaya tu na siku zote unaambiwa usimwamini mwanamke ! Yule binti kumbe siku zile alivokua analia pale stendi yule jamaa hakuwa wakwanza kujitokeza kusaidia kuna mwamba pia alijitokeza kabla na kumpaa yule dada elfu 50 na namba za siku
Yule dada alichokifanya akatoroka kutoka kwa shangazi yake mpaka kwa yule mwamba wa kwanza ! Sasa alipofika akaelezea kwamba siku zote alikuwa kwa shangazi yake. Basi wakapika wakapakua na jamaa akawa anakula mzigo kama kawaida ila baada ya mudaa yule binti akamtafta yule jamaa alie lea mimba na kumwambia yupo kwa shangazi anateseka hali ngumu na mtoto anaumwa kila siku kutokana na jamaa hajui chochote basi akamrushia nauli aje mpaka kwake vikundu.
Pika pakua jamaa akawa anakula nayeye mzigo ! Ila baada ya mdaa kwenye kukosana ambalo ni jambo la kawaida yule mwanamke alisomba vitu vyote vya jamaa na kuondoka huku jamaa akiwa kazini !
Jama alivorudii kufika vikindu akakuta chumba empty na deki kapigiwa ! Hapo jamaa alijifunza usimwamini mwanamke usie mjua na usije ukapenda mwanamke kwasababu ety ana hali ngumu kwao ndo atatulia
Jamaa yupo ila anahitaji arudishee vitu vyake vya ndani jee afanyeje maana huyo binti bado yupo huku huku dar anahangaika nyumba baada ya nyumba ?
Na ndugu zake wamedai wataftafta na watamkamata ili arudishe vitu jee jamaa akitoa taarifa polisi itafaa ?
Au kuna mbinu gani ya kuvirudisha ??kwa ambao washawai kupitia matatizo kama haya??