Nimefuta Biblia kwenye simu yangu

Nimefuta Biblia kwenye simu yangu

View attachment 2099557
Sasa nimeamini kuwa dini ni kwaajili ya maskini na waoga tu.

Mpaka leo hakuna mwanadamu au kitu chochote ikiwemo Mungu alitethibitisha kuwa Mungu yupo.

Kila mtu atakuthibitishia kwa maandiko ambayo yameandikwa kwa mkono wa mtu.

Ukiondoa maandiko hakuna mtu wa dini kukuthibitishia uwepo halisi wa Mungu.

Waislamu kwa kitabu chao watakuthibutishia uwepo wake, Wahindu, Wabudha, Waktisto n.k watakuthibutishia uwepo wa Mungu kwa maandiko na hadithi tu ila hawataweza kukuthibitishia kwa njia nyingine ya reality.

Kwa taabu wanazopata watu duniani ni kama nature ndio inatawala.

Haiwezekani Mungu ambaye wanasema aliupenda ulimwengu aruhusu vita, ubakaji, kuchinjana, kudhulumiana, ufukara, njaa n.k huku hivyo vitu ni vidogo kwake angevikomesha ndani ya sekunde.

Je, Mungu kazidiwa utu na upendo na mwanadamu?

Hii amani na hali ya maendeleo tunayoiona ni fikra na utu wa binadamu kwa ulimwengu.

Binadamu anaunda mabaraza ya kitaifa kupambana na majanga mbalimbali, pasipo na haya mabaraza Dunia isingekalika kabisa kwa idadi hii ya watu ilivyo kwa sasa.

Illusion ndizo zinatawala watu ndio maana kila dini na dhehebu wanajiona kuwa wako sahihi na wana ushahidi kuwa dhehebu lao ndilo sahihi mbele za Mungu na wao tu ndio wataingia mbinguni au peponi.
View attachment 2099556
Nimekunote sehem hapo unasema NATURE ndio inatawala? Unaweza kutuambia hiyo nature ninini? tuanzie hapo
You can not prove God physically that is spirit we nikikuuliza unaweza kuiona nafsi au roho yako tena mwogope Mungu maanake hujui unaloliongea kuna vitu vingi sana duniani vya kuvifanyia utafiti lkn achana na mambo ya Mungu kumbuka hujajiumba wala huna hiari ya kujipangia muda wa kuishi duniani wala huna hiari ya kuumwa au kutoumwa kufa au kutokufa sasa hiyo nguvu yenye mamlaka juu ya hayo ndo huyo Mungu unayesema hayupo
 
Vijana wa Siku hizi bangi na pombe zinawachanganya sana .huyu mtoa mada anasema akuna ushahidi wa reality ambao unaonyesha mungu (ALLAH) yupo.! Anafikiri kila kilichopo ni nature tu .duh hizi pombe vijana wangu ni mbaya sana. Vijan tuache stress .haya jua kutoka mashariki kwenda magharibi analipeleka Mwalimu wako wa physics au chemistry.......??? Au bibi yako wa kule kaliua.?? Kuna Vitu wala haviitaji akili kubwa kujua kama mungu yupo. Hata mtoto wa lasita b anaweza kukaa chini dk tano tu akajua huu ulimwengu Una muumba wake asie wakawaida wala binadamu.!
 
Kwa mamlaka ya Yesu natamka nguvu ikushikie.Na utakuwa MTU wa kwanza Ulipo kuona Ukuu wa Mungu.Tubu Leo mambo yako yote yatakuwa sawa futa kauli chafu
Acha ushamba wa kutisha tisha watu hauna mamlaka hayo.. kujaza watu uoga ili wasiulize wala kuhoji maswali ambayo haaana majibu yake???

Kama una hisi amekosea prove him wrong!!
 
Hujaelewa hoja

Kuna miungu 5,000

Katika hiyo miungu wewe umemchagua mmoja, hivyo hukubaliani na miungu 4,999

Miongoni mwa watu wanaoabudu hiyo miungu 4,999 ambayo wewe huikubali akakuambia anao uthibitisho unaoonesha ya kwamba mungu wako sio wa kweli ila wakwake tu

Akakuambia anaweza kukuthibitishia kua mungu wake huyo ni wa kweli, vigezo utavyotumia kuupima uthibitisho wa mtu huyo dhidi ya madai yake, ndivyo hivyo hivyo ambavyo naweza nikatumia mimi kupima uthibitisho wako utakaonipa
Wewe ndio hujaelewa.

Ni kwamba mimi nakubalia issue ya kuwepo Mungu na ndio maana ninamuamini Mungu mmoja wapo katika hiyo miungu yote, ila kwako wewe ni tofauti kwa sababu haukubali kabisa mtazamo wa uwepo wa Mungu na ndio maana katika hiyo miungu yote 5000 hakuna hata mmoja unayemkubali na kuona ni wa kweli kwa sababu haukubaliani kabisa na hizo issue sasa utaanzaje kutumia vigezo kama vyangu kujua Mungu wa kweli hali ya kuwa huna mtazamo wa uwepo wa Mungu kabisa?
 
Wewe ndio hujaelewa.

Ni kwamba mimi nakubalia issue ya kuwepo Mungu na ndio maana ninamuamini Mungu mmoja wapo katika hiyo miungu yote, ila kwako wewe ni tofauti kwa sababu haukubali kabisa mtazamo wa uwepo wa Mungu na ndio maana katika hiyo miungu yote 5000 hakuna hata mmoja unayemkubali na kuona ni wa kweli kwa sababu haukubaliani kabisa na hizo issue.
Hujaelewa bado

Katika miungu 5,000 ukamkubali mungu mmoja na kuwaacha miungu 4,999 hakukufanyi uwe karibu na ukweli kuhusu chaguo lako

Kwanini katika list ya miungu 5,000, mungu wako tu awe wa kweli na wengine wawe wauongo?

Na vipi kama spirit hiyo inashikiliwa na kila dini, kuwa hata hao wanaoabudu miungu hiyo 4,999 uliyoikataa nao pia wanasababu za kumfanya mungu wako aonekane potofu mbele ya miungu yao?

Utatumia kigezo kipi hapo kutaka kujua kati ya mungu wako na miungu yao nani ni mungu wa ukweli?
 
Hujaelewa bado

Katika miungu 5,000 ukamkubali mungu mmoja na kuwaacha miungu 4,999 hakukufanyi uwe karibu na ukweli kuhusu chaguo lako

Kwanini katika list ya miungu 5,000, mungu wako tu awe wa kweli na wengine wawe wauongo?

Na vipi kama spirit hiyo inashikiliwa na kila dini, kuwa hata hao wanaoabudu miungu hiyo 4,999 uliyoikataa nao pia wanasababu za kumfanya mungu wako aonekane potofu mbele ya miungu yao?

Utatumia kigezo kipi hapo kutaka kujua kati ya mungu wako na miungu yao nani ni mungu wa ukweli?
Scars
Una nondo nyingi kichwani.
Safi sana
 
You can not prove God physically that is spirit we nikikuuliza unaweza kuiona nafsi au roho yako tena mwogope Mungu maanake hujui unaloliongea kuna vitu vingi sana duniani vya kuvifanyia utafiti lkn achana na mambo ya Mungu kumbuka hujajiumba wala huna hiari ya kujipangia muda wa kuishi duniani wala huna hiari ya kuumwa au kutoumwa kufa au kutokufa sasa hiyo nguvu yenye mamlaka juu ya hayo ndo huyo Mungu unayesema hayupo
Save your energy for better things. Huyo kachagua upande tayari. Si kwa sababu ya ushahidi au kitu chochote. Wengi hupenda kuogelea kwenye maisha ya dhambi na wakikubali Mungu yupo itawalazimu kuyaacha hayo maisha. Hii kitu hawaitaki so only solution ni kujaribu kujiaminisha kuwa hakuna Mungu na kwa kuwa nafsi zao zinawasuta wanakuja huku nje kutafuta angalau consolation kuwa ah kumbe siko peke yangu.

Hakuna idadi ya ushahidi inamsaidia mtu wa aina hii kwa sababu shida yake sio ushahidi. Kwa hiyo tunza nguvu zako katumie kufanya kitu bora. Acha wafu wazikane kwa kutiana moyo. Ipo siku watajua ukweli na hawatahitaji kubishana na mtu kwa sababu hakutakuwa na mtu wa kubishana naye na watajua kwa hakika kama Mungu yupo au hayupo!
 
Hujaelewa bado

Katika miungu 5,000 ukamkubali mungu mmoja na kuwaacha miungu 4,999 hakukufanyi uwe karibu na ukweli kuhusu chaguo lako

Kwanini katika list ya miungu 5,000, mungu wako tu awe wa kweli na wengine wawe wauongo?

Na vipi kama spirit hiyo inashikiliwa na kila dini, kuwa hata hao wanaoabudu miungu hiyo 4,999 uliyoikataa nao pia wanasababu za kumfanya mungu wako aonekane potofu mbele ya miungu yao?

Utatumia kigezo kipi hapo kutaka kujua kati ya mungu wako na miungu yao nani ni mungu wa ukweli?
Nimeeleza kwamba vigezo nitakavyotumia mimi kuweza kumjua Mungu wa kweli ni tofauti na wewe ambaye hukubaliani kabisa na hoja ya kuwepo Mungu, kwahiyo mtazamo wangu wa uwepo wa Mungu ndipo vigezo vyangu vitapita humo kuweza kumjua Mungu wa kweli.

Kumbuka swali nililokuuliza kwamba utawezaje kujua kuwa huu kweli ni uthibitisho wa Mungu endapo ikitokea mtu akakupa huo uthibitisho?
 
Nimeeleza kwamba vigezo nitakavyotumia mimi kuweza kumjua Mungu wa kweli ni tofauti na wewe ambaye hukubaliani kabisa na hoja ya kuwepo Mungu, kwahiyo mtazamo wangu wa uwepo wa Mungu ndipo vigezo vyangu vitapita humo kuweza kumjua Mungu wa kweli.
Tufanye maelezo marefu yawe mafupi

Nipe hivyo vigezo ulivyotumia wewe ambavyo tukivipima hapa tutajua kua mungu wako ni mungu wa kweli
 
Tufanye maelezo marefu yawe mafupi

Nipe hivyo vigezo ulivyotumia wewe ambavyo tukivipima hapa tutajua kua mungu wako ni mungu wa kweli
Unakumbuka kwamba nilikuuliza swali?
 
Vipi shetani hayupo ambaye awali kabla hajaasi aliitwa Lucifer? yupo au hayupo?
Maana ukisema Mungu hayupo halafu ukatuambia shetani na malaika zake wapo tunashindwa kukuelewa.
 
Samahani Allah ni mungu wa jamii za Kiarabu. So unapomtaja Mungu usifanye hitimisho kuwa ni Allah.
mungu wako wengi. Ni zaidi ya 5000.
Huyo wako ni mungu kwa jamii zingine ingawa kwako ni Mungu
Vijana wa Siku hizi bangi na pombe zinawachanganya sana .huyu mtoa mada anasema akuna ushahidi wa reality ambao unaonyesha mungu (ALLAH) yupo.! Anafikiri kila kilichopo ni nature tu .duh hizi pombe vijana wangu ni mbaya sana. Vijan tuache stress .haya jua kutoka mashariki kwenda magharibi analipeleka Mwalimu wako wa physics au chemistry.......??? Au bibi yako wa kule kaliua.?? Kuna Vitu wala haviitaji akili kubwa kujua kama mungu yupo. Hata mtoto wa lasita b anaweza kukaa chini dk tano tu akajua huu ulimwengu Una muumba wake asie wakawaida wala binadamu.!
 
Wewe ACHA kuleta mashairi ya kiyahudi hapa narudia hakuna Mungu mkuu Wala
taka taka zake Hizo ni hekaya tu hakuna ukweli wowote Ulimwengu ulitokea tu Kwa formula maalumu na Mahesabu makali bila kuumbwa na kiumbe wa kufikirika anaitwa Mungu kama huyo Mungu wenu yupo basi ni mdogo Sana Hana nguvu yoyote na yeye anafungwa kwenye kanuni za ulimwengu maana anashindwa kuzikontrol huyo Mungu Gani kituko anaumba na kutengeneza vitu halafu vinamzidi nguvu na still mnaendelea kumwamini
Wake up dude huyo kikaragosi mliemtwngeneza Kwa mabichwa Yenu ni hekaya tu hayupo Katika uhalisia!
[emoji16][emoji16][emoji16]

Mkuu kwa jinsi nilivyokusoma na kukuelewa ni kwamba ulimwengu hakutokea tu wenyewe bali kulikuwa na chanzo kilichofanya mpaka ulimwengu ukstokea. Na kulingana na wewe uelewa na ufahamu wako ni kwamba chanzo chake ni mahesabu makali na formula maalumu. Je unaweza kunijuza aliyepiga hayo mahesabu makali ni nani? Na je hizo formula maalumu unaweza kuniwekea hapa kama ni ipi tujue kama ilitumika pie au ni formula ipi asa mpaka ulimwengu ukajitengeneza.
 
Unaelewa nilikujibu, na jibu langu hukuridhika nalo na ndio maana tumefika hapa?
Na ndio mimi nikakujibu kuwa huwezi kutumia vigezo vya kutaka kumjua Mungu wa kweli hali ya wewe hukubaliani kabisa na suala zima la kuwepo Mungu, sasa nashangaa bado unaendelea kuniuliza hivyo vigezo maana hata nikikutajia itasaidia kwenye swali nililokuuliza?
 
Na ndio mimi nikakujibu kuwa huwezi kutumia vigezo vya kutaka kumjua Mungu wa kweli hali ya wewe hukubaliani kabisa na suala zima la kuwepo Mungu, sasa nashangaa bado unaendelea kuniuliza hivyo vigezo maana hata nikikutajia itasaidia kwenye swali nililokuuliza?
Na ndio maana nikakuuliza hilo swali ambalo hujalijibu, ambalo lilikuwa na ufunguzi unaofafanua mantiki nzima ya hoja yangu
 
Na ndio maana nikakuuliza hilo swali ambalo hujalijibu, ambalo lilikuwa na ufunguzi unaofafanua mantiki nzima ya hoja yangu
Ndio ueleze hivyo vigezo vya kumtambua Mungu wa kweli vitakusaidia nini kwenye swali nililokuuliza? Hebu niambie ili nijue
 
Back
Top Bottom