Nimefiwa...

Poleni sana Mkuu!
Tunamwomba Mungu amlaze Marehemu Pahala Pema na nyinyi wafiwa Mungu awape nguvu na subira.
R.I.P. Nelasi
 
Pole sana bwana Mphavu kwa yaliyokukuta. najua ni jinsi gani unaumia kwa hayo yalitokea lakini yote ni mipango ya Mola na kazi ya Mungu haina makosa, cha kufanya tumuombee kwa Mola ili apate kupumzika kwa Amani. Pole sana bwana Mphavu.
 
...na mtoto wa dada yangu, yaani mjomba'angu, if you know what am I saying. Marehemu aliitwa Nelasi, binti wa miaka 10, mwanafunzi wa Shule ya Msingi Elu, Morogoro, aliumwa ghafla ugonjwa kama degedege (nina hakika sio), akalazwa zahanati ya Chuo Kikuu Mzumbe kwa siku kadhaa, jana akahamishiwa Hospitali ya Manispaa Morogoro, ambako mauti yalimfika majira ya saa 10 jioni, takribani saa moja baada ya kufikishwa hapo. Msiba uko Chuo Kikuu Mzumbe, nyumbani kwa wazazi wa marehemu.
Alfajiri nitaanza safari ya kwenda huko... BWANA AMETOA, BWANA AMETWAA. JINA LAKE LIHIMIDIWE!
Pole sana ndugu yetu!
Huo ni mtihani so unapaswa kuushinda kwa kumshukuru mungu!
 
@Wote.
Nashukuru kwa pole zenu, nimefika hapa msibani kama masaa mawili yaliyopita, mwili bado uko hospitali, leo ndo tutaaga na kusafirisha kuelekea Mbeya kwa maziko.
 
Pole Mphamvu,
Bwana ametoa na Bwana ametwaa jina lake lihimidiwe.
Tunawatakia mazishi na maziko mema, na Mungu akusimamie kwa kila kitu,
Ameeen.
R.I.P NELASI,Tuko nyuma yako.
 
...na mtoto wa dada yangu, yaani mjomba'angu, if you know what am I saying. Marehemu aliitwa Nelasi, binti wa miaka 10, mwanafunzi wa Shule ya Msingi Elu, Morogoro, aliumwa ghafla ugonjwa kama degedege (nina hakika sio), akalazwa zahanati ya Chuo Kikuu Mzumbe kwa siku kadhaa, jana akahamishiwa Hospitali ya Manispaa Morogoro, ambako mauti yalimfika majira ya saa 10 jioni, takribani saa moja baada ya kufikishwa hapo. Msiba uko Chuo Kikuu Mzumbe, nyumbani kwa wazazi wa marehemu.
Alfajiri nitaanza safari ya kwenda huko... BWANA AMETOA, BWANA AMETWAA. JINA LAKE LIHIMIDIWE!

hii ni CHIT Chat?

Pole kwa msiba. nafikiri iende kwenye jukwaa jingine kama sio chit chat
 
Kama nilivyowajuza awali, msafara umeondoka kuelekea Chuo Kikuu Kishiriki cha Mkwawa (anakofanyia kazi baba mzazi wa marehemu), nako wametoa heshima zao za mwisho, kisha ukaelekea Ihanda, Mbozi kwa ajili ya maziko. Msafara umetoka Iringa majira ya saa mbili usiku, hii ni kwa mujibu wa babake marehemu. Mimi, sikusafiri na maiti, bali nimebaki Morogoro kwa ajili ya kuweka mambo sawa wakati huu ambako wenye mji hawapo.
 
Pole sana mjamvi mwenzetu, fikisha pole zote hizi za JF pale msibani, endelea kujiliwaza na JF wakati huu wa msiba hasa chitchat na jokes. Tafadhali sana usiingie kwenye jukwaa la siasa.
 
Back
Top Bottom