Nimefikia maamuzi magumu, lakini sahihi

Nimefikia maamuzi magumu, lakini sahihi

Mphamvu

JF-Expert Member
Joined
Jan 28, 2011
Posts
10,702
Reaction score
3,351
Kwema wapendwa? Kutokana na malalamiko ya baadhi ya members kuhusu avatar yangu, nimeamua kuchukua maamuzi ambayo ninadhani ni sahihi kwa mustakabali wangu na mustakabali wa JF kwa ujumla. Baadhi ya members ambao wamekuwa wakilalamika ni pamoja na Mpevu, FaizaFoxy na wengine wengi just to mention the few... Kumekuwa na malalamiko kuwa avatar yangu inadhalilisha utu wa mwanamke. Utetezi wangu kuhusu hoja hii ni kuwa mimi ni mfuasi wa Nadharia ya Mtazamo-Kike ya Kiafrika (African Feminism), hivyo avatar yangu ni sehemu ya yale ninayoyaamini. Nikilinganisha na hisia za walio wengi humu jamvini, nimeona kuwa utetezi huu si kitu na hivyo nimeamua kuutupilia mbali. Dai la pili ni kuwa kumekuwa na mkanganyiko kati ya jinsi yangu na picha iliyo kwenye avatar hiyo, wadau kadhaa wamekuwa wakihoji jinsi yangu, huku wengine wakidhani kuwa mimi ni msichana, kitu ambacho si kweli. Ili kuondoa mkanganyiko huo, nimeamua kutekeleza azma yangu ambayo nimeisema hapo juu...
Hoja hizi mbili, zimenisukuma kubadili avatar yangu na kuweka hii munayoiona sasa. Natumai wale niliowakwaza na avatar yangu ya mwanzo mmenisamehe...
Nawatakia msheherekeo mwema wa avatar yangu mpya!:welcome:
 
hata siijui avatar yako ya mwanzo. Ila umetenda lililo jema.
 
kweli kila faiza foxy wamejitahidi mpaka wakakuvua gamba
 
sasa unaongea na sisi sasa ukiwa umelala sio....Amka basi..au ndio mvinyooo?
 
so hiyo picha ni wewe......?

Ndio mdada, hiyo picha nilipigwa na Erick Gamba, wakati ule nasoma Azania Sekondari... Nilikuwa nimelala darasani, nimetokea kuipenda hata leo!
 
Mphamve ahsante, umeonesha ukomavu wa hali ya juu:

"Anaepewa ushauri akausikiliza na akautekeleza ni mtu kamili"

"Anaepewa ushauri akausikiliza na asiutekeleze ni mtu nusu"

"Anaepewa ushauri asiuzikilize na akautelekeza hakuna mtu kabisa hapo"
 
Mphamve ahsante, umeonesha ukomavu wa hali ya juu:

"Anaepewa ushauri akausikiliza na akautekeleza ni mtu kamili"

"Anaepewa ushauri akausikiliza na asiutekeleze ni mtu nusu"

"Anaepewa ushauri asiuzikilize na akautelekeza hakuna mtu kabisa hapo"

Ahsante dada FF. Ila nikuulize, hiyo picha kwenye avatar yako ni yako?
 
Dah umeizidi hata serikali ya tz.hongera kwa kufanya maamuzi magumu
 
natumia simu kwahiyo siioni hiyo avatar yako mpya. Unasema wewe si msichana? Nalog off
 
Dah umeizidi hata serikali ya tz.hongera kwa kufanya maamuzi magumu

Ahsante, tangu udogoni nilifunzwa kutoumiza hisia za wengine, ingawa kutekeleza kwa vitendo imekuwa si rahisi, najitahidi kwa lile dogo niwezalo... Ahsante tena!
 
natumia simu kwahiyo siioni hiyo avatar yako mpya. Unasema wewe si msichana? Nalog off

Rejea post za juu, nimeeleza wasifu wa ile niliyoitowa. Hii mpya nadhani ina mvuto wa kipekee...
 
hongera kaka kwakujali hisia za wengne na kukubali mabadiliko.
 
Back
Top Bottom