Thibitisha kwa nini Mungu hayupo? Cc.
Kiranga
Kwanza kabisa, kisichopo hakithibitishiki kwamba hakipo.
Narudia tena, kisichopo, hakithibitishiki kuwa hakipo.
Kwa sanabu hakipo, na kama hakipo, hakithibitishiki kuwa hakipo, uthibitisho unaendana na kilichopo.
Tunaweza kujenga hoja kama za proof by contradiction kuonesha contradiction zinazoonesha kitu fulani hakiwezi kuwapo. Katika hii dhana ya Mungu (mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wote) hayupo, nimeelezea sana Epicurean Paradox mpaka michoro nimeiweka hapa. Google Epicurean Paradox, soma, ielewe, kama una swali kuhusiana an Epicurean Paradox lilete hapa.
Zaidi.
Mzigo wa uthibitisho unamuangukia yule anayesema kitu kipo.
Ndiyo maana Polisi wakija nyumbani kwako, wakisema una madawa ya kulevya, wao wanaosema una madawa ya kulevya wanatakiwa wafanye msako mpaka wayapate, wathibitishe yapo.
Hawakwambii wewe unayesema huna madawa ya kulevya uthibitishe huna madawa ya kulevya.
In principle, we cannot prove a negative, but we can show contradictions that shows the impossibility of a negative.
Swali la kuuliza hapa, ni kuwauliza wanaosema Mungu yupo, wathibitishe Mungu yupo.
Unasema Mungu yupo?
Kama unasema hivyo, thibitisha Mungu yupo.