Nimeamua Kulima kwa mara ya Pili kilimo cha mahindi

Hivi nikisema najitolea kwenda kuishi kijijini kwa makubaliano kwamba nitakuwa MTIIFU kufanya kazi zote za usimamizi wa shamba kuanzia kuandaa shamba mpaka kuvuna kwa makubaliano ya mimi kutumia nguvu,busara na hekima niliyopewa na Mungu na mtu mwingine ajitolee fedha ili kufanikisha hilo zoezi naweza kupata mtu wa kupiga naye kazi?

Makubaliano yanafanyika baada ya kila mmoja kiridhika na mwingine kwa kufahamu nyumbani na wazazi wa mwenziwe kama wapo, kisha sheria na taratibu nyingine kufuatwa.

Hili swala linawezekana?
ila siyo kilimo cha hekari kumi au ishirini(isiwe chini ya hekari 50), hapa nazungumzia shamba la ukweli maana hiyo ndiyo itakuwa ajira yangu.

Yaana kifupi naachana kabisa na mambao ya mwisho wa mwezi.
Huyo mtu yupo?

Mimi naweza ila hela yangu ndogo
 
Business gurus say it's always good to return to the basics when other business ideas fail. I am also attempting farming. Nataka kujaribu kufuga kuku wa kienyeji na samaki.
 
Mdogo wangu EL kama umeamua kulima basi iwe ni profession na siyo kubahatisha. Kilimo cha uhakika kinataka kitu kama "business plan" yaani kama vile unakwenda kuchukuwa credit bank.

Kilimo cha uhakika sio cha kuwachia vibarua na wewe unakwenda site mara nne kwa mwezi, kinataka full time committment. Tafadhali angalia wale wakulima wakubwa wa Zimbabwe na South Africa (mfano), pale ni ajira kamili na ni utajiri hasa pindi Mungu akikupa mafanikio. Hizo ekari ulizozitaja sio kidogo na ukizisimamia sawa sawa basi mwenzetu Inshalla utakuwa mbali sana ukiwa serious.

Vile vile usichukulie tu kama kila mtu anaweza kulima kama ilivyo kawaida yetu Watanzania. Nenda ukapate a, b, c za kilimo ili uweze kuondokana na kilimo cha mababu. Unaweza kufanya arrangements kupata tailor made courses pale SUA ili uweze kuelewa ni nini kinaendelea.

Hatua uliyochukuwa ni ya mfano kwa hivyo nakupongeza na kukutakia kila la kheri kwenye shughuli zako za kilimol.
 
Mdogo wangu EL kama umeamua kulima basi iwe ni profession na siyo kubahatisha. Kilimo cha uhakika kinataka kitu kama "business plan" yaani kama vile unakwenda kuchukuwa credit bank.

Kilimo cha uhakika sio cha kuwachia vibarua na wewe unakwenda site mara nne kwa mwezi, kinataka full time committment. Tafadhali angalia wale wakulima wakubwa wa Zimbabwe na South Africa (mfano), pale ni ajira kamili na ni utajiri hasa pindi Mungu akikupa mafanikio. Hizo ekari ulizozitaja sio kidogo na ukizisimamia sawa sawa basi mwenzetu Inshalla utakuwa mbali sana ukiwa serious.

Vile vile usichukulie tu kama kila mtu anaweza kulima kama ilivyo kawaida yetu Watanzania. Nenda ukapate a, b, c za kilimo ili uweze kuondokana na kilimo cha mababu. Unaweza kufanya arrangements kupata tailor made courses pale SUA ili uweze kuelewa ni nini kinaendelea.

Hatua uliyochukuwa ni ya mfano kwa hivyo nakupongeza na kukutakia kila la kheri kwenye shughuli zako za kilimol.


Hii imekaaje Mkuu, hizi kozi zipo kweli au ndio stury za kijiweni tu?
 
Heshima kwako ELNINO,

Mkuu wangu bei ya mbegu ni tsh 3500/= per kilo,utatakiwa kutumia kilo 10 kwa kila eka. 3500 x 10 x 50 = 1,750,000/=.kulima eka moja si chini ya tsh 20,000/= x 50 = 1,000,000/=.kupanda eka moja si chini ya tsh 5,000/= x 50 = 250,000/=,kupalilia eka moja si chini ya 10,000/= x 50 = 500,000/= kuvuna,kuhifadhi [magunia & dawa],kupukuchua na kusafirisha ni gharama inategemea na umbali wa masoko.Mkuu gharama za chini kabisa weka 8,000,000/= pembeni kwaajili ya hiyo shughuli yako.

Mkuu umesahau ghalama iliyo juu kuliko zote hapo-MBOLEA, unajua bei ya 50kg za CAN na UREA, minjingu imeliza watu mwaka huu ni majivu tu yale.
 
mkuu umesahau ghalama iliyo juu kuliko zote hapo-MBOLEA, unajua bei ya 50kg za CAN na UREA, minjingu imeliza watu mwaka huu ni majivu tu yale!!

Kijiji fulani huko Iringa,ukienda na Minjingu utarudi nayo ulikotoka. Kuwa makini,lakini bei ya CAN/UREA inatisha sana kwa wakulima wa Kibongo.
 
Kijiji fulani huko Iringa,ukienda na Minjingu utarudi nayo ulikotoka. Kuwa makini,lakini bei ya CAN/UREA inatisha sana kwa wakulima wa Kibongo.

Wanasema udongo wa mikoa ya kusini haukubali minjingu, lakini inasikitisha kuona bado inapelekwa kwa wingi! mimi naona serikali bado haina wataalamu wenye nia na moyo wa kuendeleza kilimo kwanza. na wafanyabiashara ndy wamepata nafasi ya kutengeneza mbolea feki kuibia wakulima!
 
Wakubwa hivi Tanzania hatuna kiwanda cha mbolea?? msaada tafadhali

Labda kama wamejenga jana usiku,nakumbuka mara baada ya kuzika kile cha Tanga,hakuna kilichoendelea zaidi ya kuwapa wahuni fulani tenda za kuingiza mbolea toka majuu kwa gharama za mkulima mdogo.

Sijui minjingu phosphates kama wataamua kuzalisha TSP,CAN au UREA and alike.
 
Heshima Mbele mkuu ELININO,

Tafadhali tupe maendeleo ya shamba.Mwanzako niko kwenye palizi kali sana majani na mahindi yanakimbizana kama wanariadha wa Kenya kwenye mbio za nyika Nimefurahi sana jinsi wanajamvi mlivyomtia moyo mkuu Elinino naamini wapo baadhi yenu mtajitosa kwenye kilimo muda si mrefu sana hasa baada ya kusoma maoni mbali mbali ya wanajamvi.
 
Labda kama wamejenga jana usiku,nakumbuka mara baada ya kuzika kile cha Tanga,hakuna kilichoendelea zaidi ya kuwapa wahuni fulani tenda za kuingiza mbolea toka majuu kwa gharama za mkulima mdogo.

Sijui minjingu phosphates kama wataamua kuzalisha TSP,CAN au UREA and alike.

Thanks bro.
 
Heshima Mbele mkuu ELININO,

Tafadhali tupe maendeleo ya shamba.Mwanzako niko kwenye palizi kali sana majani na mahindi yanakimbizana kama wanariadha wa Kenya kwenye mbio za nyika Nimefurahi sana jinsi wanajamvi mlivyomtia moyo mkuu Elinino naamini wapo baadhi yenu mtajitosa kwenye kilimo muda si mrefu sana hasa baada ya kusoma maoni mbali mbali ya wanajamvi.

Kama riadha za Kenya, I am in. Nitaleta matokeo tu, sisemi mengi.
 
Nipo dar mkuu,na kikazi niko Lindi mkuu wangu.Vp mambo safi nije?

Japo hujataja kiasi ila napenda sana mtazamo wako, inaelekea unamzuka kama mimi.

Kusema kweli lengo langu ilikuwa kama naamua kwenda shamba basi iwe ndiyo profession yangu kwa maana ya kwamba tunaanza kama wakulima wa kwaida kisha baadaye inakuwa kama uwekezaji fulani hivi so inabidi kujipanga vizuri maana siyo unaacha huku na kule kunakushinda...itakuwa DUUUUU. Target:..watu kamata huyoooo..
 
Japo hujataja kiasi ila napenda sana mtazamo wako, inaelekea unamzuka kama mimi.
Kusema kweli lengo langu ilikuwa kama naamua kwenda shamba basi iwe ndiyo profession yangu kwa maana ya kwamba tunaanza kama wakulima wa kwaida kisha baadaye inakuwa kama uwekezaji fulani hivi so inabidi kujipanga vizuri maana siyo unaacha huku na kule kunakushinda...itakuwa DUUUUU.......:target:..watu kamata huyoooo
Mpango wangu nataka nije niwe mkulima mkubwa,action plan yangu inaniongoza hivi,kwanza nichague mazao ya kulima, nichague mifugo ya kufuga na miti ya mbao ya kupata, pamoja na kufanya trial run za kila kimoja. nimeanza kujenga/kufanya project zitakazo-support kilimo changu huko mbele bila kukopa sana benki. Na la mwisho ninanunua ardhi sehemu ambazo maji yapo ya kuaminika, miundombinu na manpower.

Kwa hiyo utaona kwamba kuna project moja itaibeba project nyingine bila kuiathiri. Ukifaulu hilo bro, basi ktk kilimo ingia.
 
Japo hujataja kiasi ila napenda sana mtazamo wako, inaelekea unamzuka kama mimi. Kusema kweli lengo langu ilikuwa kama naamua kwenda shamba basi iwe ndiyo profession yangu kwa maana ya kwamba tunaanza kama wakulima wa kwaida kisha baadaye inakuwa kama uwekezaji fulani hivi so inabidi kujipanga vizuri maana siyo unaacha huku na kule kunakushinda...itakuwa DUUUUU.......:target:..watu kamata huyoooo..
Ni-pm nikutajie. Utacheka hadi uvunjike mbavu. Mkuu kilimo ni lazima tukifanye kama professionals wa kilimo hasa.
 
Mkuu Malila wala sijakusahau.

Nina kazi kuubwaa saaaana ya kuvuna, yaani mpaka nachnaganyikiwa. Inatia moyo mpaka basi. Wazee changamkieni dili. Mawazo nimeyatoa humu humu.

Elnino kaza buti mazee. You will never regret. Trust me
 
Mkuu Malila wala sijakusahau.

Nina kazi kuubwaa saaaana ya kuvuna, yaani mpaka nachnaganyikiwa. Inatia moyo mpaka basi. Wazee changamkieni dili. Mawazo nimeyatoa humu humu.

Elnino kaza buti mazee. You will never regret. Trust me

Asante kwa feedback yako. Usisahau kutoa sadaka mkuu. Mungu akujalie zaidi. Ipo siku tutaonana uso kwa uso.
 
Back
Top Bottom