Ndugu wana jamii natumaini mnaendelea vyema. Mimi ni mwanaume niliyetokea kupendwa sana na wanawake wawili ila mmoja sikuwa nampenda sana ingawa yeye alinipenda mno.
Kutokana na hilo nilimkatalia kwa nyakati tofauti kufanya mapenzi kabla sijaoa na alikuwa tayari kusubiri. Hivi karibuni alianza kunitambulisha kwa rafiki zake na ofisini kwao na alionyesha upendo wa hali ya juu kiasi cha kulia sana nisipopokea simu yake hasa usiku.
Ila nilijihadhari kumwambia kuwa simhitaji maana angeumia sana hivyo niliamua kumwomba Mungu ampe mtu atakaye mpenda na mimi nipate yule nitakaye mpenda. Siku moja baada ya maombi yule dada aliacha kabisa kupokea simu zangu na nimemtafuta mara nyingi hapokei wala kujibu meseji zangu hivyo yeye ameamini kuniacha ila kimsingi mimi ndio nimemwacha.
Pia sasa hivi nimeamua kuendelea na huyu mwingine ambaye pia ananipenda sana. Ushauri kwa vijana wenzangu tusifanye zinaa ni dhambi na pia utaumia zaidi ukiachana na mtu ambaye umefanya nae ngono maana nafsi yako inakuwa imeungana nae.
Hata huyu wa sasa sifanyi nae ngono mpaka nioe na hata akitaka kuniacha siwezi kuumia sana maana sijaunganishwa nae tumia maombi kumwacha mtu. Pia Mungu awasaidie kushinda zinaa na kupata wake na waume wema barikiweni sana pia samahani kwa maandishi mengi.
Kutokana na hilo nilimkatalia kwa nyakati tofauti kufanya mapenzi kabla sijaoa na alikuwa tayari kusubiri. Hivi karibuni alianza kunitambulisha kwa rafiki zake na ofisini kwao na alionyesha upendo wa hali ya juu kiasi cha kulia sana nisipopokea simu yake hasa usiku.
Ila nilijihadhari kumwambia kuwa simhitaji maana angeumia sana hivyo niliamua kumwomba Mungu ampe mtu atakaye mpenda na mimi nipate yule nitakaye mpenda. Siku moja baada ya maombi yule dada aliacha kabisa kupokea simu zangu na nimemtafuta mara nyingi hapokei wala kujibu meseji zangu hivyo yeye ameamini kuniacha ila kimsingi mimi ndio nimemwacha.
Pia sasa hivi nimeamua kuendelea na huyu mwingine ambaye pia ananipenda sana. Ushauri kwa vijana wenzangu tusifanye zinaa ni dhambi na pia utaumia zaidi ukiachana na mtu ambaye umefanya nae ngono maana nafsi yako inakuwa imeungana nae.
Hata huyu wa sasa sifanyi nae ngono mpaka nioe na hata akitaka kuniacha siwezi kuumia sana maana sijaunganishwa nae tumia maombi kumwacha mtu. Pia Mungu awasaidie kushinda zinaa na kupata wake na waume wema barikiweni sana pia samahani kwa maandishi mengi.