Daah usimwache mkeo kwa ishu ndogo kama hiyo hapo ukiangalia Mkeo ashawahi kuta sms au chochote kwenye simu yako ndio maana kila unapokua offline yeye anajua upo kwa huyo pisi mwingine ingawaje hawa viumbe hasa wakiwa na mimba wanataka ukaribu wa hali ya juu wewe ndio unatakiwa ubadili utaratibu wa kuwasiliana nae mara kwa mara kutokana na hali yake hizo ndio changamoto za ndoa jaribuni wote kujishusha hakuna kombe la NBC mbele yenu hayo ni maisha yenu mjue na maisha ya mtoto wenu watoto wanapenda sana kuwa kwenye familia ya baba na mama pana madini mengi wanapata ingawaje vijana wengi hizi changamoto hamtaki kupitia kwa kuwa unaweza kuishi bila yeye life haipo hivyo huyo ni Mkeo mpigie simu mkauamalize wanawake wengi karibu tabia zinafanana wanatofautiana majina tuu kwa hiyo usihangaike na mwingine kutegemea eti yeye ni afadhali anakua kaficha makucha yake baadae mkizoeana anayatoa inakua majuto ni mjukuu .
Basi usimuache mkeo kwani kinachomfanya awe hivyo ni wivu tu na hiyo mimba inampa kisirani kwani anahisi kwamba wakati yupo kwenye situation hiyo pengine wewe upo na side chicks na hivyo upo mbali ndo kabisa unampa wakati mgumu maana kila muda anakuwazia wewe tu.Asantee mkuu
Nibaada ya kuamishwa ndo mambo yalipo badilika
Wabari wakuu na wanaJF, natumaini ni wazima wacha niende kwenye mkasa.
Mke wangu ni mjamzito, sasa mwezi huu wa 11 nilipata safari ya kikazi Dodoma sasa inaenda wiki ya 3, lakini baada ya kuondoka nyumbani kwaajili ya safari hii ya kazi kiukweli hakuna amani kabisa juu ya mimi na mke wangu. Ni ugomvi, kulumbana na kugombana kila siku.
Mke wangu amekuwa na magomvi yasiyoisha sijui kwanini, lakini kila siku ni maugomvi. Kiukweli hii hali nimejitahidi sana kuiweka sawa lakini imeshindikana sababu mke wangu amekuwa kama Hakimu Mfawidhi wa Mahakama ya Taifa kila siku kesi zisizo na msingi bila sababu.
Kutokana na hayo kiukweli ikafika hatua dada yake ikabidi aingie kati na kutuweka sawa lakini wapi, jitihada zake hazikuzaa matunda kabisa, moto ukawa ni uleule. Lakini nimejitahidi sana kuhakikisha nayakabili haya lakini ikashindikana, kila nikiwaza na kutafuta tatizo ni nini sipati jibu.
Nikimuuliza mwenzangu unataka nini ili tuyaepushe haya maisha ya kugombana hana kitu cha maana na hana sababu, kwasababu mpaka dada yake kashakaa naye na kumuuliza nini shida lakini hakuna cha maana alichosema.
Kiukweli ikafika kipindi dada yake akaamua kutuacha wenyewe na kushindwa kabisa, lakini kila nikiwaza au labda ni mimba ndiyo inamsumbua, lakini dada yake aliniambia kuwa ni wivu tu ndiyo unamsumbua kwasababu anajua upo mbali ndiyo maana kila siku anaanzisha ugomvi.
Juzi nilikuwa kazini na tulikuwa tuna kikao akapiga simu, kiukweli nilishindwa kupokea nikamtumia ujumbe kuwa nitakupigia baadae niko kwa kikao lakini hakutaka kunielewa kabisa, na kuanzisha ugomvi usiyokuwa na sababu na kusema eti namdharau sipokei simu zake.
Hivi kweli wakuu hii iko sawa, na ukizingatia niko kwa kikao na viongozi wangu? Kiukweli hii hali ikafikia hatua nikashindwa wakuu kila siku ugomvi.
Wikiendi hii nikaamua kwenda nyumbani nikaongee naye vizuri anieleze kwanini anakuwa kama mtoto kila siku ugomvi ukizingatia hata hajihurumii na hali yake, nikataka anieleze nini shida na anataka tuishije? Wakuu nilijuta kurudi nyumbani, kiukweli tuligombana sana kupita amelezo na kufikia uamuzi wa kuchana!
Kiukweli naona tumeshindwana, nimeamua kuondoka na kurudi kazini tena kuendelea na kazi nikabeba nguo zangu zote na sidhani kama nitarudi nyumbani tena. Nimeamua kuanzisha maisha mapya hukuhuku nilipoletwa kikazi, nimetafuta nyumba ya 'apartment', nimeichukua nakaa mwenyewe na nimeamua kumuachia kila kitu.
Na kuna hela kwenye akaunti ambazo nimemuekea kama akiba ya dharura kutokana na hali yake, na nimeshamtaarifu dada yake kwa maangalizi, lakini kama kuna changamoto yoyote itatokea anijulishe nitampatia pesa.
Lakini sitaki amwambie mdogo wake kuwa nimempatia hela, na ninafanya hayo kwaajili ya kiumbe changu alichobeba mpaka pale atakapojifungua halafu baada ya hapo nafikiri ndiyo mengine yatafuta, kama ni talaka au vipi lakini mpaka sasa uamuzi ni kwamba kila mtu aangalie maisha yake.
Wakuu ni hayo yaliojiri, kama nitakuwa nimekosea wakuu mtanisamehe lakini nimeshindwa hayo maisha ya ugomvi kila siku. Hapana wakuu kama mtoto nitatimiza majukumu yangu kama baba.
Shukrani wakuu.
Bahna eh hutulipi fupisha maelezo hata wewe inaonesha unakera waihWabari wakuu na wanaJF, natumaini ni wazima wacha niende kwenye mkasa.
Mke wangu ni mjamzito, sasa mwezi huu wa 11 nilipata safari ya kikazi Dodoma sasa inaenda wiki ya 3, lakini baada ya kuondoka nyumbani kwaajili ya safari hii ya kazi kiukweli hakuna amani kabisa juu ya mimi na mke wangu. Ni ugomvi, kulumbana na kugombana kila siku.
Mke wangu amekuwa na magomvi yasiyoisha sijui kwanini, lakini kila siku ni maugomvi. Kiukweli hii hali nimejitahidi sana kuiweka sawa lakini imeshindikana sababu mke wangu amekuwa kama Hakimu Mfawidhi wa Mahakama ya Taifa kila siku kesi zisizo na msingi bila sababu.
Kutokana na hayo kiukweli ikafika hatua dada yake ikabidi aingie kati na kutuweka sawa lakini wapi, jitihada zake hazikuzaa matunda kabisa, moto ukawa ni uleule. Lakini nimejitahidi sana kuhakikisha nayakabili haya lakini ikashindikana, kila nikiwaza na kutafuta tatizo ni nini sipati jibu.
Nikimuuliza mwenzangu unataka nini ili tuyaepushe haya maisha ya kugombana hana kitu cha maana na hana sababu, kwasababu mpaka dada yake kashakaa naye na kumuuliza nini shida lakini hakuna cha maana alichosema.
Kiukweli ikafika kipindi dada yake akaamua kutuacha wenyewe na kushindwa kabisa, lakini kila nikiwaza au labda ni mimba ndiyo inamsumbua, lakini dada yake aliniambia kuwa ni wivu tu ndiyo unamsumbua kwasababu anajua upo mbali ndiyo maana kila siku anaanzisha ugomvi.
Juzi nilikuwa kazini na tulikuwa tuna kikao akapiga simu, kiukweli nilishindwa kupokea nikamtumia ujumbe kuwa nitakupigia baadae niko kwa kikao lakini hakutaka kunielewa kabisa, na kuanzisha ugomvi usiyokuwa na sababu na kusema eti namdharau sipokei simu zake.
Hivi kweli wakuu hii iko sawa, na ukizingatia niko kwa kikao na viongozi wangu? Kiukweli hii hali ikafikia hatua nikashindwa wakuu kila siku ugomvi.
Wikiendi hii nikaamua kwenda nyumbani nikaongee naye vizuri anieleze kwanini anakuwa kama mtoto kila siku ugomvi ukizingatia hata hajihurumii na hali yake, nikataka anieleze nini shida na anataka tuishije? Wakuu nilijuta kurudi nyumbani, kiukweli tuligombana sana kupita amelezo na kufikia uamuzi wa kuchana!
Kiukweli naona tumeshindwana, nimeamua kuondoka na kurudi kazini tena kuendelea na kazi nikabeba nguo zangu zote na sidhani kama nitarudi nyumbani tena. Nimeamua kuanzisha maisha mapya hukuhuku nilipoletwa kikazi, nimetafuta nyumba ya 'apartment', nimeichukua nakaa mwenyewe na nimeamua kumuachia kila kitu.
Na kuna hela kwenye akaunti ambazo nimemuekea kama akiba ya dharura kutokana na hali yake, na nimeshamtaarifu dada yake kwa maangalizi, lakini kama kuna changamoto yoyote itatokea anijulishe nitampatia pesa.
Lakini sitaki amwambie mdogo wake kuwa nimempatia hela, na ninafanya hayo kwaajili ya kiumbe changu alichobeba mpaka pale atakapojifungua halafu baada ya hapo nafikiri ndiyo mengine yatafuta, kama ni talaka au vipi lakini mpaka sasa uamuzi ni kwamba kila mtu aangalie maisha yake.
Wakuu ni hayo yaliojiri, kama nitakuwa nimekosea wakuu mtanisamehe lakini nimeshindwa hayo maisha ya ugomvi kila siku. Hapana wakuu kama mtoto nitatimiza majukumu yangu kama baba.
Shukrani wakuu.
Kusema kweli hili mi binafsi japo wanawake wenzangu watanipopoa ila tuseme tu ukweli.Wengi watasema ni hangover ya mimba lakini umewah jiuliza house girl akipata mimba huo mvurugiko mbona huwa haupo? Mdogo wangu akipata mimba akiwa kwangu Wala sikugundua na alijitahidi kufichaa hakuna kuchagua chakula au kudeka kama hivyo, nikagundua kumbe wanafanyaga makusudi kupima upepo, kuanza hapo nikasema make wangu haji kuniletea hivyo vitimbwili, akijizima data inakula kwake
Hizo mimba ni kisingizio tu hamna kitu hapo, yaanii mimba haiwezi sababisha mtunga mimba akachukiwa, unaweza Kuta hata mimba sio ya jamaaKusema kweli hili mi binafsi japo wanawake wenzangu watanipopoa ila tuseme tu ukweli.
Mbonq kama mimba zinatofautiana kulingana na status ya mtu????? Maana kuna watu wa matabaka flani wakiwaga na mimba hujui Wadada wa kazi, mtu ambae bwana kaikataa mimba au hana hela unakua zako normal tu!
Ila hawa zake za wenyewe hawa eeeeweh!!!! Ni hatari niko hapa na mke wa mtu naishi nae ananinyanyasa kama hakai kwangu kwanza unamfulia, anajifanya akivaa nguo dakika 0 imechafuka, mara unanuka mara niketee sijui upupu gani!!! Hapo hajaanza kulalamika oooh mimba kazi ooooh mimba fyoko yani mambo ya hovyo tu
Kusema kweli mi Mleta mada namuelewa sana! Hapa msijifanye mnajua sana kuishi na mimba ila hawa so called Wifes wenye mimba wanakera mno MNOOOOO! hata mimi ningeondoka manake maisha yenyewe ya saivi ni mimba tosha bado na mmama wa mtu akuvuruge aaah
Braza ajichimbie uko akijifungua akamwone amuulize kaacha utoto ?? Kama kaaacha waendelee na maisha.
Mimba imekua kama sehemu ya kujiendekezea ili kutimiza mambo ambayo wazazi hawajakufanyia kwenuHizo mimba ni kisingizio tu hamna kitu hapo, yaanii mimba haiwezi sababisha mtunga mimba akachukiwa, unaweza Kuta hata mimba sio ya jamaa