Nimchague nani?

Nimchague nani?

Hizi ndio athar za kua na mwanamke zaidi ya mmoja maskini asiependwa amepotezewa muda bure

Ndoa inahitaj uwe na mtu uliempenda kidhat i mean mmependana na kuridhiana, sio kua na mapenz ya upande mmoja itafikia hatua utachoka na kuamua kuacha

Wewe umempenda huyo mwanasheria sababu anakufurahisha kwenye tendo means huyu kama angekua hakufurahish kwenye tendo asingekua na nafas moyoni mwako?

Nasema hakuna uliempenda hapo we umewatamani tu mapenzi ya kweli hayaaangalii sababu ya kumpendea mtu unampenda tu unaona kila anachofanya ni sahihi kwake

Usimpotezee muda binti wa watu mcha Mungu mwambie ukweli huwez kua nae alie apate wake wa kumfuta machozi

Baki na mtu ambae unaona moyo wako umeamua
huyu jamaa anateswa na pesa za mwanasheria...upuuzi mtu, mimi siangalii elimu au alicho nacho bali nitautii moyo wangu utakaoangukia
 
Kwa miaka hii ya leo vijana nawashauri walau ufikishe miaka 30 na kuendelea ili ubongo upanuke zaidi uwe na fikra pevu. Ni ushauri tu lakini, sio sheria
Kawaida ni kama sheria boss. hata Bwana Yesu alianza rasmi utume wake baada ya kufikisha miaka 30. Na Mapadre wengi hupata upadre wakiwa na miaka kuanzia 30+. Nadhani kuna logic fulan ndan ya miaka 30+
 
Kawaida ni kama sheria boss. hata Bwana Yesu alianza rasmi utume wake baada ya kufikisha miaka 30. Na Mapadre wengi hupata upadre wakiwa na miaka kuanzia 30+. Nadhani kuna logic fulan ndan ya miaka 30+
Kimsingi huo ni umri ambao kwa binadamu yyt yule akifikisha miaka hiyo hata yy mwenyewe hujiona kbs kuwa kuna namna fulani amebadilika hasa ktk uwezo wa kufikiri, kuchambua na kuamua mambo kwa usahihi. Ile hali ya u- kiddish hutoweka

BTW ndoa tamu sana hasa kwa siku za mwanzoni
 
Kimsingi huo ni umri ambao kwa binadamu yyt yule akifikisha miaka hiyo hata yy mwenyewe hujiona kbs kuwa kuna namna fulani amebadilika hasa ktk uwezo wa kufikiri, kuchambua na kuamua mambo kwa usahihi. Ile hali ya u- kiddish hutoweka

BTW ndoa tamu sana hasa kwa siku za mwanzoni
Huko kwenye BTW...... mzee umetishia aman siooa.
 
Miaka 25 bado ni umri mdogo kuoa kwa miaka ya sasa, walau ujivutevute ufikishe hata 30 na kuendelea
Usimdanganye mwenzio wewe kama hutaki kuoa au umeoa ukiwa na 30 ni wewe mimi namshauri aoe ndoa nikitu kizuri na yeye hatachelewa kulea sio wengine sabini 70 ndio anamtoto mchanga kisa alitaka aoe malaika akakosa
 
Usimdanganye mwenzio wewe kama hutaki kuoa au umeoa ukiwa na 30 ni wewe mimi namshauri aoe ndoa nikitu kizuri na yeye hatachelewa kulea sio wengine sabini 70 ndio anamtoto mchanga kisa alitaka aoe malaika akakosa
Aaaaah wap
 
Kabla hujaoa ni waz una vigezo vyako japo s vyote vutatekelezeka lakin uko na vile muhim, sema na moyo wako angalia vigezo ulivyonavyo na wanawake yupi mizani imepanda chekecha shirikisha akili ako utapata jibu

Unaoa sababu wazazi wanakushinikiza?

Kwa sababu mjomba wake katika ukoo alioa miaka kama yake.. Too childish
 
Shida iko kwa nani?? Ni dini gan huyo baba?? Wapi anatimiziwa mahitaji hake kkmwili?
Ni wakristo. Yule mama(mkewe) anaonekana hana shida ingawa kisaikolojia ni kama anajikaza tu. Sijamdadisi kwa undani sana huyu Mzee japo anaonekana kbs kakata tamaa sana.

Unajua ikifikia hatua ya mwanandoa kutotamani masaa ya kutoka kazini yaishe sababu tu hana hamu ya kurudi nyumbani kwake ni mbaya sana
 
Ni wakristo. Yule mama(mkewe) anaonekana hana shida ingawa kisaikolojia ni kama anajikaza tu. Sijamdadisi kwa undani sana huyu Mzee japo anaonekana kbs kakata tamaa sana.

Unajua ikifikia hatua ya mwanandoa kutotamani masaa ya kutoka kazini yaishe sababu tu hana hamu ya kurudi nyumbani kwake ni mbaya sana
hiyo ni hatari naamini katika nguvu ya kukaa chini na kujadili tofauti zinazojitokeza kuliko kupuuza wakae chini wayaongee kils mtu ateme nyongo yake maisha yaendelee wawe wapya asee miaka nane mhhhhhh hapa wanaishi kimazoea tu maskin ndoa hiz
 
Huko kwenye BTW...... mzee umetishia aman siooa.
Hutakiwi kuogopa ila ndio uhalisia wenyewe huo ndugu

Mwanzoni mahaba huwa motomoto haswaaaa, kila lisaa likikatika unahesabu ili tu muda wa kazi uishe upesi uwahi nyumbani - shida inaanza-ga kikishaingia kimeta ohoooooo unatamani masaa yarudi nyuma ili tu usisogee mitaa ya home pale pale ulipokuwa unapakimbilia. Na kama hivo ukaingia kwenye mikono ya mwanasheria mbona mtanange!
 
Tafuta daftari.

Orodhesha sifa za mke unaemuhitaji zote.

Then tengeneza line column 3.
1. Sifa unazohitaji hata zfike 50
2. Mwanasheria
3. Mcha Mungu

Uwe unatiki na kukata kwa 2 au 3.

Rate percentage kutokana na unavovalue sifa husika.

Jibu kaa chini ns Mungu muombe akuongoze ktk uamuzi.

Ila swala kubwa hapa ni mke . Sawa tendo lachangia ila sio pekee. Kuna vitu zaidi ya hivyo. Vingine ni hisia tu.

Pia inawezekana kwa sababu unao wote wawili ndiyo maa a unaona huyu kuliko huyu ila nakuambia mbakize mmoja utaona.

Mwisho wapeleke kwa mama wote wawili siku tofauti. Mama atakuambia live.

Ila kwa msisitizo ukitulia na kujiweka karibu na Mungu atakujibu Live Live Live. Hata hutababaika
 
hiyo ni hatari naamini katika nguvu ya kukaa chini na kujadili tofauti zinazojitokeza kuliko kupuuza wakae chini wayaongee kils mtu ateme nyongo yake maisha yaendelee wawe wapya asee miaka nane mhhhhhh hapa wanaishi kimazoea tu maskin ndoa hiz
Mzee anakwambia yupo pale sababu tu ya watoto wake ambao bado wapo shule wanasoma vinginevyo sijui angekuwa Wapi. Na ukiangalia ni kweli maana kila wanae wakija likizo baba yao huwa ana amani sana issue shule zikifunguliwa kama hivi wanabaki yy na mkewe tu ni horrible kbs!

Kwa maelezo yake ameshafanya kila awezalo kuwekana sawa lkn holaaa. Yule mama hataki ukubwa, anajiona bado msichana mbiiiichiiii( hata namna anavyovaa na kubehave) ni shida
 
Hutakiwi kuogopa ila ndio uhalisia wenyewe huo ndugu

Mwanzoni mahaba huwa motomoto haswaaaa, kila lisaa likikatika unahesabu ili tu muda wa kazi uishe upesi uwahi nyumbani - shida inaanza-ga kikishaingia kimeta ohoooooo unatamani masaa yarudi nyuma ili tu usisogee mitaa ya home pale pale ulipokuwa unapakimbilia. Na kama hivo ukaingia kwenye mikono ya mwanasheria mbona mtanange!
Sawa mkuu.
 
Back
Top Bottom