Ukiona mwanamke mwenye umri kuanzia 18-50 analia njaa we tambua tuu amependa mwenyewe.
Hawa viumbe wana marafiki wengi bwana, leo akipata shida kwake sio tatizo kwani ana pa kukimbilia.
Nadhubutu kusema hawa wanawake wameteka utajiri wa hii dunia.
Leo katika ujasusi wa wangu nimefanikiwa kuchunguza inboxza mke wangu za facebook na insta nilichokiona huko sio vibaya ku share nanyi.
Pia mtambue hakuna urafiki mbele ya mwanamke na hapa ndio ule msemo wa hakuna ushemeji tunatulaga unatimia.
Wife kaenda shamba asubuhi nikasema ngoja niipekue simu yake.
Nilipata hili wazo jana baada ya kuona lock pattern yake na nikasema iko siku nitamcheki tuu na hatimaye leo nimeweza kuona.
Sio marafiki zangu, mashemeji zangu tunaosalimiana huko barabarani eti wanamtaka wife japo siku moja na ahadi nyingine kibao!
Nimekuta mi msg nyingi mno, fb nimekuta 720 na uzuri zote read so mimi sikuona shaka kufungua na kuona kilichomo.
Insta nimekuta msg 421 huko nako nimekuta mambo kibao.
Huyu mwanamke nashukuru sana Mungu kwa kunipa maana angekua ni kicheche basi nisinge ambulia chochote hapa.
Wanaume wenzangu kweli ukiona mwanamke kajitiolea kwa ajili yako maisha yake yote plz and plz naomba umuheshimu kwani kaona wanaume wa kila aina lakini amekuacha ili awe wako.
ONYO: Kwa mwanaume yoyote yule ambae hajajipanga kukabiliana na hali ya hatari hapa duniani basi usimpekue sana mkeo vinginevyo utakufa kwa kupata mshtuko kali au hata kuuwana na mahawara wako na mtagombana na wife na hatimaye na wale marafiki zako.
We usiamini mtu kabisa chukulia mambo easy. Ukiona umeoa mwanamke mwenye maadili mema na mvumilivo kwa kila baya unalomtendea plz mheshimu na ikiwezekana mpigie magoti umlilie kama mtoto kama unapenda penzi lako lidumu!
Hasira za wanawake zimewaingiza wengi kaburini hivyo hata akikisea usikasiirike sana wala kuweka kinyongo. Kuwa kama mwanaume bana hawa ni maua ya duniani kila mwanaume anayatamani.
Ila sijui kama wanawake na wao wanapendana kwa kweli maana kwa haya mambo mbona ni hatari sana.