Niliyoyaona inbox za mke wangu

Niliyoyaona inbox za mke wangu

hakika mkuu, maisha haya sio yakukagua kagua simu ya mwenza wako, hivi ukimwamini tu bila papara zakuchokonoa hautakua safe??
[HASHTAG]#unaambiwa[/HASHTAG] nyoka hana miguu bt ukimchunguza sana utaiona tu

Hiyo statement huwa siielewi kabisa.
Kuweka ratiba ya kukagua simu ya mwenza ni ushamba nakubali.
Lakini kuna instance lazima ujiaminishe. Chukulia hiki kisa changu.

KE daily tukiwa wote alikuwa anapigiwa simu na namba ngeni. Kila siku akipigiwa nikiwa nae haipokei. Sijawahi mgusia kuhusu hiyo namba. One day ikapigwa tena. Nikamwambia hii namba iliyoishia na 28 kwanini huwa hauipokei? ?akajing'atang'ata nikamkazia then akanisimulia kila kitu.

Je nisingechunguza ningelijua nililofanikiwa kujua? Kuna wapenzi wengine hata ukiishiwa salio ukitaka kutumia simu yake yeye ndiye ana kulockia password. Huu ni wizi na uchawi mkuu kwangu. Mambo yawe wazi..ila kila mtu awe na simu yake.
 
Mkuu unamaanisha ulichokikuta kwacm yamke wako upo salama ila upo vitani?
 
big gitf umeoa lini wewe? yaani na utaalamu wako jana ndio umegundua pattern za simu ya mkeo, kwa taarifa yako ukute anapigiwa simu anaenda kupigwa miti na kurudi wewe unabaki unakenua meno eti hujaona meseji chafu
 
Uharamia niliuacha zamani maana mwisho wa siku wajikuta wewe ndio unaumia na si mwenziwako.

Nilishawahi kuhack email ya mchumba enzi hizo kwa kutumia keylogger sijui kama bado zipo hizo software. Niliyoyakuta yakikuwa mazito labda niweke bandiko mahusui la kueleza mkasa mzima.

Pia nilishafanya backup ya simu yake hapo hata kama anatumia pin au pattern au password hua haja ya kuzijua ila unatumia ti usb cable connect simu yake kwenye pc then watumia software matata za backup mzee kama file scavenger nk hizo zinarudisha hata kama ujumbe alifuta au picha vinarudi.

Nilichojionea duh sikutake endela tena, na hizi kazi.

Sababi zinachukua muda wako mwingi kumpekua pia ukishapona ukweli unaomia waweza jiumbia magonjw ya ajabu ajabu ya akili na mwili.

Kisa kimoja tu nishirikiana na ninyi;:
Paja jamaa yangu alikuwa na demu wako miaka ya zamani kidogo, basi binti alichukua kamare ya mr wake akenda nayo kwa muda wa wiki mbili hivi. Kumbe binti alikuwa na kajamaa tena walikuwa na kajipati flani so akachukua kamera ili wajifotoe za ukumbusho.
Binti alivyomaliza kuitumia kamera akafuta picha zoote na kumrudishia jamaa yangu.

Jamaa naona alihisi kitu ila hakuw na uhakika ndipo akanipatie hiyo kamera yake mzee nikaito memory card yake na kuitumia kwenye deep scan ya scavenger mapicha yoote yakarudi na video kama ndio zimepigwa upya jamaa akajionea usaliti wa demu wake.

Ndio maana sishauri mtu kufanyia mtu wako vetting mwisho huwaga mbaya sana.

Mtoa posti haimaanishi upo salama,

Na mke au mume ngumu wachunga wakiamua fanya yao watafanya tu...aidha kazini au njiani nk na usipate ushahidi wowote ktk simu au mitandao.
Noted mkuu ngoja nizicheki hizo app najua zitakua updated na ziko kwenye ubora wa hali ya juu.

Hizi hard disk zetu na imani hazipo sala inshor tuko uchi sana. Manufacture wakiamua kutufatilia watatupata tuu.
 
NIPE NAMBA YAKE NIMJARIBU KAMA SHETANI ALIVYOMJARIBU EVA
 
Noted mkuu ngoja nizicheki hizo app najua zitakua updated na ziko kwenye ubora wa hali ya juu.

Hizi hard disk zetu na imani hazipo sala inshor tuko uchi sana. Manufacture wakiamua kutufatilia watatupata tuu.
Duuh unamoyo wa kishujaa bado unakiu ya kumpekua mwenzi wako haha??

Hivi bongo huduma za private investigator zipo kweli?!

Kama katika Riwaya ya MIFUPA 206?!
 
Hiyo statement huwa siielewi kabisa.
Kuweka ratiba ya kukagua simu ya mwenza ni ushamba nakubali.
Lakini kuna instance lazima ujiaminishe. Chukulia hiki kisa changu.

KE daily tukiwa wote alikuwa anapigiwa simu na namba ngeni. Kila siku akipigiwa nikiwa nae haipokei. Sijawahi mgusia kuhusu hiyo namba. One day ikapigwa tena. Nikamwambia hii namba iliyoishia na 28 kwanini huwa hauipokei? ?akajing'atang'ata nikamkazia then akanisimulia kila kitu.

Je nisingechunguza ningelijua nililofanikiwa kujua? Kuna wapenzi wengine hata ukiishiwa salio ukitaka kutumia simu yake yeye ndiye ana kulockia password. Huu ni wizi na uchawi mkuu kwangu. Mambo yawe wazi..ila kila mtu awe na simu yake.
kila kamba inakula urefu wa mbuzi yake aisee, bt hapo hukuchunguza bali ulihoji kwa kile ulichokua na hofu nacho,,basi maana yake nikua,hukatazwi kuhoji pindi uonapo uozo maana huo utakua ni woga, bali kushinda kukagua simu ndio ufala-lization, wengine hushinda kuangalia namba ngeni mpesa ili wajue tu ni mwanaume alipiga,au mwanamke...
 
Unachokitafuta utakipata siku moja kwenye simu za hao watu. ......naona peace of mind imekuzidia mwenzetu kiasi sasa umeanza kusahau mateso ya stress. ....endelea kudeal na simu za mkeo siku si nyingi utatuletea thread hapa.....Mungu akutangulie katika udukuzi wako
 
kila kamba inakula urefu wa mbuzi yake aisee, bt hapo hukuchunguza bali ulihoji kwa kile ulichokua na hofu nacho,,basi maana yake nikua,hukatazwi kuhoji pindi uonapo uozo maana huo utakua ni woga, bali kushinda kukagua simu ndio ufala-lization, wengine hushinda kuangalia namba ngeni mpesa ili wajue tu ni mwanaume alipiga,au mwanamke...
Nimekupata.
Kushinda kukagua ni ushamba na kukosa kazi. Ila unapoona sintofahamu kwa mwenza wako lazima ujiridhishe aseeh. Ila naamini kujiamini ni kuzuri saana mtu anakuwa hana mashaka na wewe hata kama unacheat.

Mtu pattern ngumu kama utandu wa buibui..ukiingia tena ndani kila app ina password yake. Hawa watu ni majipu. Ukiona mtu anajificha ficha ujue kuna madudu tuu
 
Usimuamini mwanamke hata siku moja. Hawa dada zetu wana akili na utashi wa kupita kiasi. Unaweza kukuta hiyo scenario yote aliitengeneza wewe halafu wewe unajiona sherlock holmes kumbe alikuonyesha pattern kwa makusudi. Hakikisha unatimiza majukumu yako na misimamo yako iwe wazi. Ajue kuwa siku ukigundua kimenuka. Lakini ujinga wa kupekua simu yake ni kujipa pressure tu. Never ever trust these beings.
 
Hapo sawa...

Nilidhani ulikuwa na lengo la kujustify 100% kuwa mkeo ni mwaminifu.

Mi naamini mwanamke anakuwa wako ukiwa naye. Ndio maana sipotezagi kumfuatilia sana mai waifu kwakuwa najua mwanadamu hachungiki, na kifo cha presha si kizuri... nitawapa wezi wangu wigo mpana zaidi wa kumtafuna kwa uhuru.

Ukiona mwanamke mwenye umri kuanzia 18-50 analia njaa we tambua tuu amependa mwenyewe.
Hawa viumbe wana marafiki wengi bwana, leo akipata shida kwake sio tatizo kwani ana pa kukimbilia.
Nadhubutu kusema hawa wanawake wameteka utajiri wa hii dunia.


Leo katika ujasusi wa wangu nimefanikiwa kuchunguza inboxza mke wangu za facebook na insta nilichokiona huko sio vibaya ku share nanyi.

Pia mtambue hakuna urafiki mbele ya mwanamke na hapa ndio ule msemo wa hakuna ushemeji tunatulaga unatimia.

Wife kaenda shamba asubuhi nikasema ngoja niipekue simu yake.
Nilipata hili wazo jana baada ya kuona lock pattern yake na nikasema iko siku nitamcheki tuu na hatimaye leo nimeweza kuona.

Sio marafiki zangu, mashemeji zangu tunaosalimiana huko barabarani eti wanamtaka wife japo siku moja na ahadi nyingine kibao!

Nimekuta mi msg nyingi mno, fb nimekuta 720 na uzuri zote read so mimi sikuona shaka kufungua na kuona kilichomo.
Insta nimekuta msg 421 huko nako nimekuta mambo kibao.

Huyu mwanamke nashukuru sana Mungu kwa kunipa maana angekua ni kicheche basi nisinge ambulia chochote hapa.

Wanaume wenzangu kweli ukiona mwanamke kajitiolea kwa ajili yako maisha yake yote plz and plz naomba umuheshimu kwani kaona wanaume wa kila aina lakini amekuacha ili awe wako.


ONYO: Kwa mwanaume yoyote yule ambae hajajipanga kukabiliana na hali ya hatari hapa duniani basi usimpekue sana mkeo vinginevyo utakufa kwa kupata mshtuko kali au hata kuuwana na mahawara wako na mtagombana na wife na hatimaye na wale marafiki zako.

We usiamini mtu kabisa chukulia mambo easy. Ukiona umeoa mwanamke mwenye maadili mema na mvumilivo kwa kila baya unalomtendea plz mheshimu na ikiwezekana mpigie magoti umlilie kama mtoto kama unapenda penzi lako lidumu!

Hasira za wanawake zimewaingiza wengi kaburini hivyo hata akikisea usikasiirike sana wala kuweka kinyongo. Kuwa kama mwanaume bana hawa ni maua ya duniani kila mwanaume anayatamani.
Ila sijui kama wanawake na wao wanapendana kwa kweli maana kwa haya mambo mbona ni hatari sana.
 
We ushaliwa.. Hiyo patern ndio uthibitisho
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom