Ila wageni wanaoenda Njombe,Iringa na Mbeya ambako maambukiz yako juu hawatumii mipira? Sababu dhaifu sana hii.
Ama kuhusu mtoa mada,amezungumzia umaskini wa Mikoa ya kusini hasa vijijini kwamba ni wa kutupwa. Bahati nzuri Tanzania tunafahamiana vizuri tu. Ukiondoa mkoa wa Kilimanjaro,hali ya maisha vijijini kwa kila mkoa ni mbaya sana na inafanana.
Hivi,vijiji vya mkoa wa Dodoma,Singida,Tabora,Mara,Manyara,Arusha,Mwanza,Shinyanga,Geita,Simiyu kutaja michache vina nini hasa kuweza kusema vina unafuu kuliko vijiji vya Walima korosho wa Mtwara,Walima Chai wa Njombe,Iringa?
Mtoa mada anaandika kana kwamba vijiji vya mikoa mingine vina utajiri. Ukweli ni kwamba vijiji vya mikoa ya Kusini vina unafuu mkubwa kuliko kule kwenye matembe ya wafugaji.
Itoshe tu kusema mtoa mada kaamua kuiponda mikoa husika kwa sababu anazozijua yeye,lakini kama kwa umaskini wa vijijini,Mikoa ya kusini ina unafuu kuliko hata vijiji vya mikoa mingine,ila yote kwa yote,vijijini maeneo yote,hali ya maisha bado hairidhishi,na karibia viko sawa kwa sawa.