Salaam wote!
Katika hangaika zangu za hapa na pale nilipata fulsa ya kushiriki katika mbio za mwenge kwa baadhi ya mikoa ya Tanzania mwaka huu Na kama tunavyojua Mwenge hukimbizwa Wilayani mpk vijijini na unapokesha basi Mwenge hukesha sehem iliyochangamka na Mara nyingi inakuwa kwenye Kata.
Nilipata bahati ya kuwa kwenye mbio za Mwenge Mikoa ya Arusha, Kilimanjaro, D'salaam, Iringa, Njombe, Ruvuma, Mtwara na kisha Lindi hii ikiwa ni mkoa mzima mpk vijijini kunapokuwa na Miradi ya maendeleo inayozinduliwa au kukaguliwa.
Katika Mikoa yote niliyopita Mikoa ya kusini ina umasikini wa kupindukia mno, nikianza na Iringa na Njombe pamoja na kwamba ni wazalishaji wa chakula na mbao kwa wingi lakini huko vijijini ni tabu tupu, bado watoto kwenda shule bila viatu na nguo zilizochanika ni kawaida sana, watoto kukaa kwenye mawe dalasani ni kawaida pia, huko Ludewa na Makete maisha ni magumu sn, ukiwatizama wananchi unawahurumia wamekata tamaa na hawajui kesho yao japokuwa ni maisha ya kawaida kwao.
Maisha ya wananchi wa Mikoa ya Ruvuma, Mtwara na Lindi yanafanana na ht tamaduni zao ni kama zinafanana kwa kiasi kikubwa, Ruvuma ni Mikoa Mkubwa na km tujuavyo ni wazalishaji wa chakula lakini huko Nyasa, Mbinga vijijini ni shida sn, kuna umasikini wa kutupwa, watu wa kusini wanapenda ngoma mno, ukifika mgeni ambae sio mwenyeji utashangaa kuazia wakubwa mpk watoto, wanaume kwa wanawake wanapenda ngoma na mdundiko, wasichana wa Mikoa ya Kusini kukupa papuchi sio kitu kwao.
Kiwango cha maambikizi ya Ukimwi kiko juu sana, japo kuwa kwasasa Iringa, Njombe na Mbeya inaongoza kwa maambukizi lakini nakwambia wanawake wa Mikoa ya Kusini hawatakunyima ukiwaomba kwa kulinganisha na Mikoa ya Kaskazini niliyopita. Ruvuma, Mtwara na Lindi kumkuta binti Mdogo ana mtoto ni kawaida kabisa, Wenyeji wa Mtwara na Lindi elimu kwa mtoto wa kike sio kipaumbele kabisa!
Nikiwa Ruvuma,Lindi na Mtwara nilijaribu kutembelea mabanda ya kupima HIV na kujaribu kuwauliza wahudumu wa Yale mabanda kuhusiana na maambukizi, nilijibiwa maambukizi kwa vijana yako juu na hawajali kuambiwa ana maambukizi.
Mtwara na Lindi wanampenda sana Ndugu yao harmonize, hata km wanacheza ngoma ikipigwa nyimbo yake wote wanaacha kucheza ngoma wanakimbilia inakopigwa nyimbo yake. Huko Tandahimba kuna shida ya Maji kupita kiasi, wamama asubuhi wanapishana wakiwa na baskeli na madumu ya Maji huku wamebeba watoto mgongoni. Masasi maisha yako juu sn km hapa Dar vyakula mpk nyumba ni km hapa Dar.
Mikoa ya Mtwara na Lindi wadada wanaojiuza wanakuwa ni wale wahudumu wa bar, hii nimeikuta Masasi, Newala, Nanyumbu, Tandahimba na sehem za Mijini za hiyo Mikoa so ukimtaka mda wowote unamchukua unaenda kupiga Ila utamlipa pesa yake na utamlipa meneja wa bar kwa mda ambao hayupo kazini.
Wakauu wa Mikoa, Wilaya na Wakurugenzi wanaogopa sana mbio za Mwenge, Mwenge unapokuwa kwenye eneo lake wanakuwa wenye hofu wakiogopa miradi yao kukataliwa na wanamnyenyekea sn Kiongozi wa mbio za Mwenge ambae anapofika anakuwa na taarifa zote kupitia usalama wa taifa mkoa au wilaya.
Yako mengi nimejifunza kupitia mbio za Mwenge mwaka huu niishie hapa kwanza!