Niliwashauri ATC wasiende China kupitia Bangkok, hawatapata faida njia ina ushindani sana, naona hawakusikia

Synthesizer

JF-Expert Member
Feb 15, 2010
11,143
18,774
Naona ATCL wameamua kwamba wataenda China kupitia Bangkok, Thailand Bangkok. Njia hii ina ushindani sana, haitakuwa na faida kwao kupitia Bangkok na kushindana na mashirika makubwa ambayo yameweka mizizi sana kwenda au kupitia Bangkok pamoja na Ethiopian Airways and Kenya Airways.

Ninawashauri kwamba wawe innovative katika kubuni njia ambapo wanaweza kuvuta abiria hata kutoka nchi jirani badala ya mentality ya Kitanzania ambapo jirani yako akifungua genge la nyanya mtaani kwenu na wewe unaenda kufungua genge la kuuza nyanya pembeni yake badala ya kuuza bidhaa ambayo wale wanaonunua nyanya kwa jirani yako wataitaka kwako!

ATCL wafikirie route kama kwenda China kupitia Hong Kong, au Mumbai, au Delhi au Bangalore badala ya kufuata mkumbo wa kila shirika linaloenda China kupitia Bangkok. Hatuhitaji kuuza nyanya kwa kuwa jirani anauza nyanya. Tuuze vitunguu na chumvi.

Wakienda China kupitia Hongkong, Bangalore, Delhi kwa mfano, unaweza kukuta wanavuta abiria kutoka nchi kama Kenya, Uganda, Rwanda Zambia nk ambazo watapeleka regional flight kwa ajili ya hiyo connection, na kupata pia abiria wanaoenda huko ambao labda inabidi waende hadi South Africa au Addis Ababa kupata hiyo connection.

ATCL kwenda China kupitia Bangkok unajiweka katika wigo wa kukosa abiria pale Bangkok kwa kuwa wana options nyingi sana. Jiulize, kwa nini abiria watumie ATCL na sio Kenya Airways au Ethiopian Airways? Anzisha route kwa namna ambayo unawa-compel abiria kutumia ATCL, sio unawapa ATCL kama option nyingine kati ya nyingi zilizopo.
 
Labda kama walivyosema wahenga
"Sikio la kufa halisikii dawa "
Mkuu tatizo ni kufanya kazi kwa mazoea na kuogopa kuwa wabunifu - unafanya kile ambacho wenzako wanafanya ili tatizo likitokea ukwepe lawama na ionekane kama ni kifo cha wengi ni harusi.

Watu wengi sana katika uongozi wanaogopa kufanya kitu original kwa kuwa kikifeli wataonekana hawajui kazi! Hivyo hawako tayari kuchukua risk ya kufeli katika original thinking, hata kama decision katika routine thinking ina risk kubwa zaidi
 
Naona ATC wameamua kwamba wataenda China kupitia Bangkok, Thailand, tofauti na kile nilichowashauri kwamba njia ya Bangkok ina ushindani sana, haitakuwa na faida kwao kupitia Bangkok na kushindana na mashirika makubwa ambayo yameweka mizizi sana kwenda au kupitia Bangkok pamoja na Ethiopian Airways and Kenya Airways.

Niliwashauri kwamba wawe innovative katika kubuni njia ambapo wanaweza kuvuta abiria hata kutoka nchi jirani badala ya mentality ya Kitanzania ambapo jirani yako akifungua genge la nyanya mtaani kwenu na wewe unaenda kufungua genge la kuuza nyanya pembeni yake badala ya kuuza bidhaa ambayo wale wanaonunua nyanya kwa jirani yako wataitaka kwako!

Niliwaambia ATC kwamba wafikirie route kama kwenda China kupitia Hong Kong, au Mumbai, au Delhi au Bangalore badala ya kufuata mkumbo wa kila shirika linaloenda China kupitia Bangkok. Hatuhitaji kuuza nyanya kwa kuwa jirani anauza nyanya. Tuuze vitunguu na chumvi.

Wakienda China kupitia Hongkong, Bangalore, Delhi kwa mfano, unaweza kukuta wanavuta abiria kutoka nchi kama Kenya, Uganda, Rwanda Zambia nk ambazo watapeleka regional flight kwa ajili ya hiyo connection, na kupata pia abiria wanaoenda huko ambao labda inabidi waende hadi South Africa au Addis Ababa kupata hiyo connection.

ATC kwenda China kupitia Bangkok unajiweka katika wigo wa kukosa abiria pale Bangkok kwa kuwa wana options nyingi sana. Jiulize, kwa nini abiria watumie ATC na sio Kenya Airways au Ethiopian Airways? Anzisha route kwa namna ambayo unawa-compel abiria kutumia ATC, sio unawapa ATC kama option nyingine kati ya nyingi zilizopo.
Unatoa ushauri kama nani kwanza? Jitambulishe wewe ni nani kujiona una maarifa kuliko staff nzima ya ATCL
 
Tatizo la watanzania tumekuwa makambale tumeota sharubu! Hata mambo ambayo wahusika wakuu wapo mtu anachukua kisimu chake cha toch anaanza kubwabwaja!
 
Unatoa ushauri kama nani kwanza? Jitambulishe wewe ni nani kujiona una maarifa kuliko staff nzima ya ATCL
Sawa Mkuu. Nina connection na wizara inayohusika na ATCL na nina background na mambo ya transport na aviation management. Yangu yalikuwa mawazo tu, haina maana nina maarifa kuliko staff nzima ya ATCL. Lakini pia haina maana ili niwe na wazo zuri kwa ATCL lazima na mimi niwe staff wa ATCL. Hili ni shirika linanihusu kama madau Mtanzania.
 
Sawa Mkuu. Nina connection na wizara inayohusika na ATCL na nina background na mambo ya transport na aviation management. Yangu yalikuwa mawazo tu, haina maana nina maarifa kuliko staff nzima ya ATCL. Lakini pia haina maana ili niwe na wazo zuri kwa ATCL lazima na mimi niwe staff wa ATCL. Hili ni shirika linanihusu kama madau Mtanzania.
ATCL imekuwa inashambuliwa na watu wasioitakia mema nchi wengi wao wakitaka kudidimiza juhudi za Rais za kufufua shirika letu! Nadhani ushauri wako kama ungeutoa kwa kufuata proper channel ungewafikia wahusika na kuuchukulia uzito unaostahili kuliko njia hii ambayo inachukuliwa katika mtizamo hasi!
 
Tatizo la watanzania tumekuwa makambale tumeota sharubu! Hata mambo ambayo wahusika wakuu wapo mtu anachukua kisimu chake cha toch anaanza kubwabwaja!
Hiyo ni mentality kwamba raisi kwa kuwa yeye ni raisi basi ana akili na anajua mambo kuliko Watanzania wote hawezi kukosea wala hapaswi kukosolewa. Waziri naye hivyo hivyo katika mambo ya Wizara yake.

Mkurugenzi wa ATCL hivyo hivyo, na watu tulioko nje ya ATCL hatupaswi kusema kitu kwa kuwa chochote tukachosema hakina maaan wao ndio wanajua kila kitu na ndio maana wako ATCL na sisi hatuko ATCL. Very illiterate kind of thinking.
 
Unatoa ushauri kama nani kwanza? Jitambulishe wewe ni nani kujiona una maarifa kuliko staff nzima ya ATCL

Kuna mtu amekumbushia kuwa sio mara ya kwanza natoa ushauri kwa ATCL kama mdau, kwa nia nzuri tu kwa kuwa nimesomea mambo hayo. Angalia hapa chini.

Naipongeza serikali kwa jitihada ya kuokoa fedha za walipa kodi nchini kwa kuamua kuipaka rangi ndege ya Fooker iliyokuwa ya serikali hapa hapa nchini kwa kutumia mafundi wetu.

Hata hivyo, tusije tukawa tumechukua mafundi rangi wa Gerezani ili kuokoa gharama. Upakaji rangi ndege unapaswa kufanywa kwa makini na watu wanaojua masuala ya ndege. Wasipoangalia huo upakaji tutaishia na yale yale ya ndege kuanguka kwa kuwa sensor fulani zilikuwa hazifanyi kazi baada ya kuzibwa na rangi!

Sijui kama upakaji huu wa rangi ulizingatia factor kama nozzle pressure ya sprayer wakati wa kuipaka. Huko nje kuna vyumba maalum vya kupakia rangi ambavyo sehemu kubwa ya ndege hupakwa kwa low pressure spray. Kuna ndege ya Air France ilianguka kwa sababu tu ilioshwa kienyeji na zile pampu za kurusha maji kwa nguvu zinazotumika car-wash!

Kwa mfano vitu kama pua na leading edge, wamepaka rangi wakizingatia masuala ya friction kati ya ndege na hewa na athari zake kwa rangi kwa jinsi ilivyochanganywa au kutengenezwa kwa mambo ya mawasiliano, rada, static charge, lightining strikes (radi) na mengineyo? Huo upakaji rangi wa pua ya ndege unakubalika? Ndege sio gari, kuna factors kidogo tu usipokuwa makini Magufuli atakuwa anatuma salamu za rambirambi. Fokker ni ndege ya zamani, na pua yake ina mambo tofauti kabisa na ndege za kisasa, huwezi tu ukaipaka rangi kienyeji. Unaweza kukuta pilots hawapati radio signal kutoka aircaft control au rada wakaishia kugongana na ndege nyingine, au kuingia kwenye storm clouds kwa kuwa rada haikuziona!

Nawashauri serikali/ATC wawasiliane na Fokker juu ya hii kazi ya kupaka rangi iliyofanyika nchini.

Nose of an aircraft which we technically call radome contains radar antenna. In civil aircrafts radar serves to dodge thunderstorms. One desirable property of this radome is it must be non metallic and non reflecting surface to minimise the reflection of the transmitted signal from the radome back to the antenna which might damage the receiver crystal. So the radomes use to be composite fibre. But why black? Black serves as anti glare which prevented sun light reflection into the pilot's eyes.
 
Unatoa ushauri kama nani kwanza? Jitambulishe wewe ni nani kujiona una maarifa kuliko staff nzima ya ATCL
Hapana mdau.
Tusijenge utamaduni wa kukataa ushauri bila kuutathimini sababu aliye toa ushauri sio wa kundi lenu.
Ushauri unapokelewa na kufanyiwa uchunguzi wa kinakujiridhisha manufaa yake au hasara zake.
 
Back
Top Bottom