Nebuchadneza
JF-Expert Member
- Oct 6, 2023
- 415
- 1,032
Habari zenu,
Ndugu zangu kwenye ukuaji tunapitia hatua mbalimbali za maisha, kipindi nikiwa mdogo nishanusurika kifo zaidi ya mara 3, kusema kweli nilikuwa mtundu sana nisiyesikia chochote,na michezo yangu ilikuwa hatari sana,tena ya kutosha.
Naanza kama hivi. Mara ya kwanza. Kipindi nikiwa na miaka 3 nilishaingiaga kwenye friji nikaka huko zaidi ya dakika 45,wazazi walinitafuta sana wakajua nimepotea au nimeishiwa,maana kipindi kile watoto walikuwa wanaibiwa sana.
Sasa baada ya kunitafuta kwa dakika 45 wakachoka,wakaona waende police kutoa taarifa,sasa kabla hawajaenda baba akaona apate maji ya baridi,ndipo hapo akanikuta kwenye friji baridi limenikolea viungo vyote vimelegea,vidole vishakakama wakaniwaisha hospital ikawa pona yangu.
Mara ya pili. Kipindi tukiwa watoto tulipenda kucheza kombolela, na kipindi kile ukibutua kopo unaonekana shujaa,sasa wakati nakimbia kujificha kumbe jirani alifumua chemba lake la mavi lilikua limejaa,na hakutoa taarifa kwa majirani.
Wakati nakimbia nilijua shimo bado limefunikwa, kipindi nakimbia nilikuwa naangalia nyuma ghafla ile nageuka mbele USO kwa USO shimo lipo mbele yangu, nikaruka kwa nguvu ile nafika ng'ambo ya pili nikakosa BALANCE nikawa narudi kinyume nyume kama mtu aliyesukumwa mlimani.
Sasa wakati narudi kinyume nyume huku nateleza kuelekea shimoni,nikapapasa pembeni nikagusa mawe ya chemba ndiyo yalionisaidia kukishika,huku miguu ikiwa ndani ya mavi mpaka kwenye magoti,wakaja watu kunivuta ndo ikawa pole yangu
Mara ya tatu. Hii ilikuwa moshi,ilikuwa juma Juma tatu ya ubarikio(moshi ubarikio jumapili,sasa Jumatatu waliobarikiwa huenda sokoni kununua vitu kwa ela waliopewa zawadi siku ya ubarikio).
Sasa baada ya kununua zawadi zetu ile tunarudi nyumbani ilikuwa mida ya saa 11 jioni na mpaka kufika nyumbani kuna zaidi ya km 18,kuna pick up ikatupita tukaona tudandie tulikuwa watoto 4,sasa ile chuma ya kuweka miguu ikangooka tukaanza kuburuzwa,kweli tuliburuzwa ile akili inatukaa sawa tukaachia mikono kwenye lile chuma ndo ikawa pole yetu,tulichubuka mapaja,tumbo na kucha za vidole zilingooka.
Maisha ni mapito.
Ndugu zangu kwenye ukuaji tunapitia hatua mbalimbali za maisha, kipindi nikiwa mdogo nishanusurika kifo zaidi ya mara 3, kusema kweli nilikuwa mtundu sana nisiyesikia chochote,na michezo yangu ilikuwa hatari sana,tena ya kutosha.
Naanza kama hivi. Mara ya kwanza. Kipindi nikiwa na miaka 3 nilishaingiaga kwenye friji nikaka huko zaidi ya dakika 45,wazazi walinitafuta sana wakajua nimepotea au nimeishiwa,maana kipindi kile watoto walikuwa wanaibiwa sana.
Sasa baada ya kunitafuta kwa dakika 45 wakachoka,wakaona waende police kutoa taarifa,sasa kabla hawajaenda baba akaona apate maji ya baridi,ndipo hapo akanikuta kwenye friji baridi limenikolea viungo vyote vimelegea,vidole vishakakama wakaniwaisha hospital ikawa pona yangu.
Mara ya pili. Kipindi tukiwa watoto tulipenda kucheza kombolela, na kipindi kile ukibutua kopo unaonekana shujaa,sasa wakati nakimbia kujificha kumbe jirani alifumua chemba lake la mavi lilikua limejaa,na hakutoa taarifa kwa majirani.
Wakati nakimbia nilijua shimo bado limefunikwa, kipindi nakimbia nilikuwa naangalia nyuma ghafla ile nageuka mbele USO kwa USO shimo lipo mbele yangu, nikaruka kwa nguvu ile nafika ng'ambo ya pili nikakosa BALANCE nikawa narudi kinyume nyume kama mtu aliyesukumwa mlimani.
Sasa wakati narudi kinyume nyume huku nateleza kuelekea shimoni,nikapapasa pembeni nikagusa mawe ya chemba ndiyo yalionisaidia kukishika,huku miguu ikiwa ndani ya mavi mpaka kwenye magoti,wakaja watu kunivuta ndo ikawa pole yangu
Mara ya tatu. Hii ilikuwa moshi,ilikuwa juma Juma tatu ya ubarikio(moshi ubarikio jumapili,sasa Jumatatu waliobarikiwa huenda sokoni kununua vitu kwa ela waliopewa zawadi siku ya ubarikio).
Sasa baada ya kununua zawadi zetu ile tunarudi nyumbani ilikuwa mida ya saa 11 jioni na mpaka kufika nyumbani kuna zaidi ya km 18,kuna pick up ikatupita tukaona tudandie tulikuwa watoto 4,sasa ile chuma ya kuweka miguu ikangooka tukaanza kuburuzwa,kweli tuliburuzwa ile akili inatukaa sawa tukaachia mikono kwenye lile chuma ndo ikawa pole yetu,tulichubuka mapaja,tumbo na kucha za vidole zilingooka.
Maisha ni mapito.