Mkuu sijui ni jamaa wapi unaoongelea hata hivyo naomba nichangie hoja zako
1. Kuhusu mfumo ni nini, hili swali anauliza Barbarosa kila wakati. tuliwahi kuandika maelezo tukitaraji angeelewa. Kila mara anarudia, hivyo tunakaa kimya hatuna uwezo mwingine wa kumsaidia. Tunafahamu pia ni njia anayotumia kuhamisha mjadala
2. Kuna vitu viwili katika maoni yako.
Moja, kuna mfumo ambao upo wa chama kimoja, na miaka 50 umetufikisha katika 'utamaduni' wa ufisadi Kwamba, ni wakati tuangalie mfumo mzima kwanza
Pili, kuna CCM unaowasema. Mfumo ni kitu na humilikiwa na watu.
Kwa miaka 50 CCM ndio watawala wakitumikia mfumo huo.
Licha ya kelele za wananchi, bado wanaamini ni mzuri tu kwavile unawafaidisha binafsi
3. Kwavile CCM ndio kikwazo katika kufumua mfumo huu waliouasisi , kuna uhusiano wa moja kwa moja, wa mfumo, CCM na matokeo yake kama ufisadi.
Mfano,Rais anatumbua majipu, wanaopaswa kumsaidia wanachukua rusha, i.e Wabunge wa CCM. Hii inaeleza wanavyoujua mfumo na kuutumia bila woga kwasababu tu ndio 'wamiliki' wa mfumo. Wanajua wao na serikali lazima watii mfumo unaonedesha na CCM
Wala rushwa wanatetewa na Spika badala ya kuchukuliwa hatua kwa mujibu wa sharia.
Spika anawabadilisha kamati ili kupooza habari ionekane ni jambo dogo.
Anajua kutumia mfumo uliopo kulinda wala rushwa kama wabunge-CCM
4. Hiki mnachosikia kutumbua majipu kwa vijana wadogo ni kitu cha kipekee sana.
Kwa watu waliokula chuimvi kiasi na hapa niwaalike
Mzee Mwanakijiji Mag3 JokaKuu Jasusi Andrew Nyerere kwa uchache wa kuwataja wanakumbuka Tumbua majipu ifuatayo
a) Wahujumu uchumi na walanguzi wakati wa Sokoine hadi vipindi vya mikingamo
B)Usipo wajika utakumbwa na fagio la chuma wakati wa Mwinyi
Kwasababu hatukuwa na mfumo endelevu kazi yote ikaisha tumerudi kwa kasi , ari mpya na nguvu mpya katika ufisadi kuliko wakati mwingine toka uhuru
Tunachosema ni kuwa, kama CAG, TISS wanatakiwa kuangaliwa kimfumo, isiishie hapo
Lazima tujiulize DPP, DCI, IGP, Bunge, BoT, Hazina, serikali n.k zipo katika nzuri?
Tunakumbuka mtifuano wa PCCB ya Hosea na DPP.
Tujiulize, tatizo ni hawa watu peke yao? Je walikwama wapi?
Iweje Magufuli anapata habari za wakati wa JK leo hii?
Kwa jicho pana, hakuna kilichokuwa hakijulikani. Mfumo wetu ndio iliokwamisha kila j
DPP hana uwezo hadi Rais aseme, DCI hana uwezo mbele ya Rais, IGP anawajibika kwa Rais, BoT inaendeshwa kisiasa-ya Kagoda. DCI hana uhuru wa kutekeleza majukumu
Orodha ni ndefu sana. Haiwezekani CAG na TISS tu. Mfumo ni kitu 'intertwining'
Badala ya kuangalia tulipojikwa, tupo bize kuangalia tumeangukia wapi
Baada ya miaka 5 anakuja mpasua matambazi, miaka 5 anakuja mwingine kupaka GV vipele, miaka 5 mingine anakuja mwingine kuondoa fungus! No hatufiki