Herbalist Dr MziziMkavu
JF-Expert Member
- Feb 3, 2009
- 43,037
- 34,742
- Thread starter
- #261
Niliuwa kwa kukusudia-33-
ILIPOISHIA JANA Mbele yake kulikuwa na meza ndogo ambayo kwa juu kulikuwa na bastola ambayo aliwahi kunionesha ofisini kwake. Nikiwa na hasira iliyopita kiwango huku mikono na midomo ikinitetemeka, niliichukua ile bastola na kuielekeza kwa Elhakimu. Lengo lilikuwa ni kumuua hivyo nikaanza kuhesabu; mojaaa...mbilii...tatu.... SASA ENDELEA...
ila kusita nikammiminia kwa hasira risasi kadhaa mwilini mwake. Risasi ya kwanza nilihakikisha inapenya na kuharibu sehemu zake za siri kama adhabu ya kuzitumia sehemu hizo vibaya kutunyanyasa kijinsia mimi na mdogo wangu Inana. Risasi ya pili nilihakikisha inatua katika paji la uso wake nikilenga kuuadabisha ubongo wake kwa kuthubutu kuwaza kutubaka. Baada ya kutekeleza unyama huo, ghafla hasira zangu ziliyeyuka.
Nikaanza kuingiwa na hofu kuu kutokana na mauaji niliyoyafanya ambayo sikuwahi kuyafikiria. Kuna wakati nikiwa nimeishika ile bastola baada ya kumpiga risasi mbili, nilihisi nimefanya maamuzi sahihi hasa baada ya kukumbuka unyama alionifanyia lakini baada ya muda tena nikajiwa na mawazo kwamba nimechukua uamuzi mbaya ambao utaniharibia kabisa maisha yangu. "Potelea mbali," nilijikuta nikitamka maneno hayo na kuitupa ile bastola chini.
Bila kuangalia chini, nilitoka kwa kukimbia kuelekea nje ya nyumba ya Elhakimu ambaye kwa wakati huo nilikuwa na uhakika kuwa tayari ni mmoja kati ya wafu waliopokelewa kuzimu siku hiyo. Kabla sijafika mlangoni, nilijikuta nikiwekwa chini ya ulinzi na askari polisi wakiongozwa na yule mlinzi wa Elhakimu ambaye nilikuwa na uhakika alisikia milio ya risasi wakati namuua bosi wake hivyo kuamua kuniitia polisi.
Kutokana na idadi ya polisi waliofika, sikuwa na ujanja, nilikuwa mpole nikijua fika kuwa hakuna cha kunifanya niwe huru kutokana na tukio lile la mauaji. Siku hiyo kwa mara ya kwanza katika maisha yangu nilipelekwa kituo cha polisi kama mtuhumiwa, mikononi mwangu nikiwa na pingu huku askari wakiwa pembeni na nyuma yangu, wawili wakiwa wameshikilia bastola.
Baada ya kufika kituoni nilichukuliwa maelezo kuhusiana na tukio hilo ambapo nilikataa katakata kuwa sikuua jambo ambalo liliwachukiza polisi wale waliokuwa na uhakika kuwa nilihusika kwa asilimia mia moja na mauaji ya Elhakimu. Bila kupoteza muda waliniingiza ndani ya selo nikiwa navuja jasho huku nikionekana kama niliyechanganyikiwa.
Nililala mpaka siku iliyofuata ambapo mdogo wangu Inana alikuja kuniona na kuniletea chakula. Sikuwahi kumuona Inana akiwa katika hali hiyo kabla kwani uso wake ulikuwa mwekundu ajabu. Macho yake yalikuwa na rangi ya manjano kuonyonesha kwamba alilia kwa muda mrefu kabla ya machozi kukauka.
"Dada, hata siamini! Siyo wewe wamekusingizia tu. Wewe siyo muuaji dada, niamini haya nisemayo," aliniambia mdogo wangu Inana huku akiangua kilio kikubwa palepale kituoni. Bila kujali kwa pamoja tukaanza kulia wote huku nafsi yangu ikinisuta kwa maneno ya mdogo wangu ambaye kwa wakati huo hakuamini kabisa kama ningeweza kufanya unyama ule.
Kilio chetu kilibadilika na kuanza kuwakera mahabusu wenzangu, ikabidi polisi wamtake mdogo wangu aondoke mara moja kituoni hapo jambo ambalo alilifanya japo kwa uzito. Siku moja kabla ya kesi yangu kutajwa, kaka mmoja aliyejitambulisha kama wakili wangu alikuja kunitembelea gerezani na kunitaka nimsimulie kila kitu kilichotokea na uhusika wangu katika mauaji ya Elhakimu.
Kwa kuwa nafsi yangu ilikuwa imeanza kujutia yote niliyoyafanya, nikamuelezea mwanzo hadi mwisho bila kuficha jambo lolote ili yeye ajue kama ni kunisaidia, ananisaidiaje. "Pole sana kwa yaliyokukuta, lakini naomba nikuambie kwamba, usije ukathubutu kukubali kuwa umeua na kusimulia ukweli wote huo mbele ya
hakimu," aliniambia wakili huyo kwa msisitizo na kuahidi kuwa atatumia taaluma yake ya sheria kuhakikisha kuwa siingii hatiani.
"Sawa kaka," nilimjibu wakili huyo, tukaagana na kurudishwa selo. Nikiwa mle selo watuhumiwa wenzangu walikuwa na shauku ya kujua nilikuwa nimefanya kosa gani hadi kufikishwa pale kituoni huku nikiwa binti mdogo. Mmoja wao ambaye alionekana alikuwa na cheo mle selo, aliniita na kuniuliza nilifanya kosa gani lililonifanya niwe pale. Je, alijibu nini?
Usikose kufuatilia simulizi hii kesho jioni .....
ILIPOISHIA JANA Mbele yake kulikuwa na meza ndogo ambayo kwa juu kulikuwa na bastola ambayo aliwahi kunionesha ofisini kwake. Nikiwa na hasira iliyopita kiwango huku mikono na midomo ikinitetemeka, niliichukua ile bastola na kuielekeza kwa Elhakimu. Lengo lilikuwa ni kumuua hivyo nikaanza kuhesabu; mojaaa...mbilii...tatu.... SASA ENDELEA...
ila kusita nikammiminia kwa hasira risasi kadhaa mwilini mwake. Risasi ya kwanza nilihakikisha inapenya na kuharibu sehemu zake za siri kama adhabu ya kuzitumia sehemu hizo vibaya kutunyanyasa kijinsia mimi na mdogo wangu Inana. Risasi ya pili nilihakikisha inatua katika paji la uso wake nikilenga kuuadabisha ubongo wake kwa kuthubutu kuwaza kutubaka. Baada ya kutekeleza unyama huo, ghafla hasira zangu ziliyeyuka.
Nikaanza kuingiwa na hofu kuu kutokana na mauaji niliyoyafanya ambayo sikuwahi kuyafikiria. Kuna wakati nikiwa nimeishika ile bastola baada ya kumpiga risasi mbili, nilihisi nimefanya maamuzi sahihi hasa baada ya kukumbuka unyama alionifanyia lakini baada ya muda tena nikajiwa na mawazo kwamba nimechukua uamuzi mbaya ambao utaniharibia kabisa maisha yangu. "Potelea mbali," nilijikuta nikitamka maneno hayo na kuitupa ile bastola chini.
Bila kuangalia chini, nilitoka kwa kukimbia kuelekea nje ya nyumba ya Elhakimu ambaye kwa wakati huo nilikuwa na uhakika kuwa tayari ni mmoja kati ya wafu waliopokelewa kuzimu siku hiyo. Kabla sijafika mlangoni, nilijikuta nikiwekwa chini ya ulinzi na askari polisi wakiongozwa na yule mlinzi wa Elhakimu ambaye nilikuwa na uhakika alisikia milio ya risasi wakati namuua bosi wake hivyo kuamua kuniitia polisi.
Kutokana na idadi ya polisi waliofika, sikuwa na ujanja, nilikuwa mpole nikijua fika kuwa hakuna cha kunifanya niwe huru kutokana na tukio lile la mauaji. Siku hiyo kwa mara ya kwanza katika maisha yangu nilipelekwa kituo cha polisi kama mtuhumiwa, mikononi mwangu nikiwa na pingu huku askari wakiwa pembeni na nyuma yangu, wawili wakiwa wameshikilia bastola.
Baada ya kufika kituoni nilichukuliwa maelezo kuhusiana na tukio hilo ambapo nilikataa katakata kuwa sikuua jambo ambalo liliwachukiza polisi wale waliokuwa na uhakika kuwa nilihusika kwa asilimia mia moja na mauaji ya Elhakimu. Bila kupoteza muda waliniingiza ndani ya selo nikiwa navuja jasho huku nikionekana kama niliyechanganyikiwa.
Nililala mpaka siku iliyofuata ambapo mdogo wangu Inana alikuja kuniona na kuniletea chakula. Sikuwahi kumuona Inana akiwa katika hali hiyo kabla kwani uso wake ulikuwa mwekundu ajabu. Macho yake yalikuwa na rangi ya manjano kuonyonesha kwamba alilia kwa muda mrefu kabla ya machozi kukauka.
"Dada, hata siamini! Siyo wewe wamekusingizia tu. Wewe siyo muuaji dada, niamini haya nisemayo," aliniambia mdogo wangu Inana huku akiangua kilio kikubwa palepale kituoni. Bila kujali kwa pamoja tukaanza kulia wote huku nafsi yangu ikinisuta kwa maneno ya mdogo wangu ambaye kwa wakati huo hakuamini kabisa kama ningeweza kufanya unyama ule.
Kilio chetu kilibadilika na kuanza kuwakera mahabusu wenzangu, ikabidi polisi wamtake mdogo wangu aondoke mara moja kituoni hapo jambo ambalo alilifanya japo kwa uzito. Siku moja kabla ya kesi yangu kutajwa, kaka mmoja aliyejitambulisha kama wakili wangu alikuja kunitembelea gerezani na kunitaka nimsimulie kila kitu kilichotokea na uhusika wangu katika mauaji ya Elhakimu.
Kwa kuwa nafsi yangu ilikuwa imeanza kujutia yote niliyoyafanya, nikamuelezea mwanzo hadi mwisho bila kuficha jambo lolote ili yeye ajue kama ni kunisaidia, ananisaidiaje. "Pole sana kwa yaliyokukuta, lakini naomba nikuambie kwamba, usije ukathubutu kukubali kuwa umeua na kusimulia ukweli wote huo mbele ya
hakimu," aliniambia wakili huyo kwa msisitizo na kuahidi kuwa atatumia taaluma yake ya sheria kuhakikisha kuwa siingii hatiani.
"Sawa kaka," nilimjibu wakili huyo, tukaagana na kurudishwa selo. Nikiwa mle selo watuhumiwa wenzangu walikuwa na shauku ya kujua nilikuwa nimefanya kosa gani hadi kufikishwa pale kituoni huku nikiwa binti mdogo. Mmoja wao ambaye alionekana alikuwa na cheo mle selo, aliniita na kuniuliza nilifanya kosa gani lililonifanya niwe pale. Je, alijibu nini?
Usikose kufuatilia simulizi hii kesho jioni .....