Mr Why
JF-Expert Member
- Nov 27, 2019
- 1,353
- 2,351
Mimi nikijana wa miaka 27 nilishinda betting kiasi kikubwa tu cha pesa lakini sikuwahi kumweleza mwanafamilia yeyote na wala hakuna anayefahamu, nikaamua kujenga nyumba kupitia zile pesa za betting kwahiyo nikawa na nyumba ya ghafla
Sikutaka kumshirikisha ndugu au mwanafamilia kwa haraka
Nikaanza kumshirikisha mama yangu mzazi nikajua atafurahi
Jambo la kushangaza akashtuka sana baada ya muda kidogo kila nikiongea nae ananambia kuna utajiri wa kafara isijekuwa nimejiunga nikadhani labda ameongea tu lakini kila mara anasema maeneno hayo hayo
Kwahiyo leo nagundua kuwa tayari ananiita mchawi
Kuna kaka yangu naye ni mlokole kwa miaka yote na mwamini lakini huwezi kuamini siku anakuja kwangu alipoondoka alianza kunizungumzia habari za kafara
Naona jinsi gani familia yangu nitavunja nao uhusiano kwasababu ya kunipakazia mambo makubwa kiasi hiki
Inawezekanaje mama yako mzazi anathubutu kukutamkia maneno kama haya ni dhahiri nimezaliwa familia yenye laana ya mafanikio
Unathubutuje kumshutumu mtu kuwa ana mali za kafara wakati pesa kapata kupitia betting akiwa kama mtu mzima kwanini asingetulia akaambiwa taratibu badala ya kutapika maneno machafu kama haya
Watu wengi wanasema kuzaliwa bongo ni nuksi kwakweli nimeona
Sikutaka kumshirikisha ndugu au mwanafamilia kwa haraka
Nikaanza kumshirikisha mama yangu mzazi nikajua atafurahi
Jambo la kushangaza akashtuka sana baada ya muda kidogo kila nikiongea nae ananambia kuna utajiri wa kafara isijekuwa nimejiunga nikadhani labda ameongea tu lakini kila mara anasema maeneno hayo hayo
Kwahiyo leo nagundua kuwa tayari ananiita mchawi
Kuna kaka yangu naye ni mlokole kwa miaka yote na mwamini lakini huwezi kuamini siku anakuja kwangu alipoondoka alianza kunizungumzia habari za kafara
Naona jinsi gani familia yangu nitavunja nao uhusiano kwasababu ya kunipakazia mambo makubwa kiasi hiki
Inawezekanaje mama yako mzazi anathubutu kukutamkia maneno kama haya ni dhahiri nimezaliwa familia yenye laana ya mafanikio
Unathubutuje kumshutumu mtu kuwa ana mali za kafara wakati pesa kapata kupitia betting akiwa kama mtu mzima kwanini asingetulia akaambiwa taratibu badala ya kutapika maneno machafu kama haya
Watu wengi wanasema kuzaliwa bongo ni nuksi kwakweli nimeona