Mr. Wise
JF-Expert Member
- Jul 23, 2012
- 7,733
- 6,469
Dunia ina mambo........
Na mengine ni yakusikia tu............
Kuna jamaa yangu alikuwa anatafuta nyumba ya kuishi[kupanga],alinijulisha hili jambo na tulisaidiana kutafuta kuepuka usumbufu wa madalali na gharama zao
Hatimae wiki moja iliyopita alifanikiwa kupata nyumba eneo la Nyakato Buzuruga,hapa jijini Mwanza,na alihamia siku hiyo hiyo.Ilikuwa ni nyumba nzuri sana na iko kwenye hali nzuri tu
Siku 4 baada ya kuhamia yeye na mkewe na watoto wao wawili jamaa alinipigia simu akiniomba jioni baada ya mihangaiko yetu niende nyumbani kwake kuna mambo hayaelewi kidogo kuhusiana na nyumba ile
Jioni nilikwenda na aliniambia kuwa mara nyingi nyakati za usiku wakati amelala na mkewe huwa wanarushiwa matonge ya ugali kitandani na wakati mwingine kumwagiwa mchanga,na kila yalipokuwa yanatokea hayoi matukio huwa anawasha taa ili kuona labda ndani kuna mtu lakini huwa kunakuwa hakuna tofauti ya yeye na mkewe,na akirudi tena yanarudia yaleyale,na kali zaidi usiku wa kuamkia siku niliyokwenda mkewe aliingiliwa kingono na mtu ambae alikuwa hamuoni na alipojaribu kupiga kelele ili mumewe aamke alikuwa anashindwa,hivyo alikuwa anaomba nimshauri cha kufanya
Nilikaa kimya kwanza nikitafakari haya aliyoniambia,baada ya kimya cha kama dakika 2 hivi nilimuuliza kuhusu lolote analojua kuhusiana na uchawi akaniambia hana analojua zaidi za kusikia story tu mitaani,pia nilimuuliza kuhusu uhalisi wa hayo na alinihakikishia ni kweli kabisa,kiukweli nilishindwa kukubali au kuataa na nilimuambia anipe muda wa kutafakari kidogo
Ndipo leo nikiwa nipo nyumbani na kwakuwa leo sijaenda kwenye shughuli zangu kwa kuwa sijisikii vyema na wakati huohuo sijui cha kumwambia huyu rafiki yangu kutokana na mambo yake kutokuwa na ushahidi na uhakika alinipigia simu niende kumsaidia kupaki vitu kwenye gari kwani anahama nyumba ile.[alikuwa anajua kuhusu kuwepo kwangu home leo]
Nilistuka kidogo,lakini nikajisemea wacha niende nikamuulize kulikoni hukohuko.
Nilifika na kumkuta mkewe pamoja na wanae wakiwa katika harakati hizo za kuhama,nikaamua nitamuuliza baada ya kumaliza harakati hizo maana inaonekana kama kuna jambo kubwa sana lililomfanya ahame ghafla hivyo
Ndipo wakati wa kuhamisha vitu hivyo ndipo kilipotokea kioja kilichonistua sana.
Tulikuwa chumbani tukifungua kitanda mimi na huyu rafiki yangu ili kipakiwe kwenye gari,mule ndani kulikuwa na sofa la kumtosha mtu mmoja na juu yake lilikuwa limewekwa begi kubwa la nguo na mule ndani hakukuwa na mtu zaidi ya mimi na yule rafiki yangu tuliekuwa tumezama kwenye kukifungua kitanda na huku akiniambia baadhi ya vituko vya pale
Unajua kuna vitu mtu huwezi kumuambia na mtu akakuelewa labda tu awe amevishuhudia,na ndio kama hiki changu,kwani ghafla tulisikia harufu ya kitu kinaungua na wote wawili mimi na na rafiki yangu huyu tulitazamana na kisha tukageukia kule tulokokuwa tunahisi kunaungua na ndipo tulipoona moto ukiwaka pale lilipokuwa limewekwa lile begi,yaani kwenye sofa
Nilipigwa pumbuwazi kwanza kwa sababu sofa lile halikuwa mlangoni tungesema labda kuna mtu aliingia kwa kificho na akawasha moto kisha kutoweka wakati sisi tukiwa tumezama kwenye kufungua kitanda,lakini sivyo,sofa lilikuwa nyuma yetu na mlango ulikuwa mbele yetu yaani mtu ili aingie ni lazima tungemuona tu
Ilibidi tuanzishe harakati za kuuzima ule moto lakini cha kushangaza ilionekana ule moto ulikuwa umewaka muda mrefu sana bila sisi kusikia na ulikuwa umeshaliunguza lile begi robo tatu na moto ulikuwa umeanza kushika kwenye sofa
Kwa taharuki tuliuzima ule moto na kufanikiwa na tulilitoa nje lile sofa huku kila mmoja akiwa na maswali mengi sana kichwani
Tulishindwa hata kuuliza maana mazingira tu ya kuwaka moto ule yalifanya tukose ujasiri wa kuuliza kama kuna mtu aliingia mule ndani na kuuwasha ule moto
Yaani mtu aingie ndani na kuwasha moto mpaka begi liungue uwe hujasikia?Ni ngumu sana kueleweka,mkewe rafiki yangu alipouliza kulikoni begi limeungua na sofa tulimwambia tutamueleza kazi ya kuhama ikiisha!
Tulimaliza na tumeahidiana na rafiki yangu kuwa tutakutana kesho jioni ili tuongee zaidi kwani nyumba aliyokuwa anahamia ilitakiwa aifanyie marekebisho kidogo hivyo alihitaji muda kwaajili ya hilo
Nilirudi nyumbani majira ya saa 6 hivi huku nikiwa na maswali mengi sana kuhusiana na ule moto,hadi sasa sijui ni nani aliuwasha na uliwakaje na kwanini
Matukio haya nilikuwa nasimuliwa tu na nilikuwa nahisi labda mengine ni story tu ila leo nimeshuhudia live mimi mwenyewe,sina majibu hadi sasa!
Sina ham kwakweli!
Kuna haja ya kuwa makini na hizi nyumba tunazoishi
Unaweza kwenda kuishi mahali pa ajabu sana!
Mkuu dunia inatumikiwa na nguvu mbili, moja yatoka kwa yule muovu ibilisi na Nyingine kwa Mungu....haya mambo yapo tena kuna makubwa zaidi ya hayo, na hata ya ki Mungu pia yapo yanayompatia sifa Mungu, ila mara nyingi ni ugumu wa mioyo ya wanadamu wa kutokuamini vitu ambavyo hawajavishuhudia kwa macho.