Nilichokishuhudia leo...!

Nilichokishuhudia leo...!

Dunia ina mambo........
Na mengine ni yakusikia tu............

Kuna jamaa yangu alikuwa anatafuta nyumba ya kuishi[kupanga],alinijulisha hili jambo na tulisaidiana kutafuta kuepuka usumbufu wa madalali na gharama zao

Hatimae wiki moja iliyopita alifanikiwa kupata nyumba eneo la Nyakato Buzuruga,hapa jijini Mwanza,na alihamia siku hiyo hiyo.Ilikuwa ni nyumba nzuri sana na iko kwenye hali nzuri tu

Siku 4 baada ya kuhamia yeye na mkewe na watoto wao wawili jamaa alinipigia simu akiniomba jioni baada ya mihangaiko yetu niende nyumbani kwake kuna mambo hayaelewi kidogo kuhusiana na nyumba ile

Jioni nilikwenda na aliniambia kuwa mara nyingi nyakati za usiku wakati amelala na mkewe huwa wanarushiwa matonge ya ugali kitandani na wakati mwingine kumwagiwa mchanga,na kila yalipokuwa yanatokea hayoi matukio huwa anawasha taa ili kuona labda ndani kuna mtu lakini huwa kunakuwa hakuna tofauti ya yeye na mkewe,na akirudi tena yanarudia yaleyale,na kali zaidi usiku wa kuamkia siku niliyokwenda mkewe aliingiliwa kingono na mtu ambae alikuwa hamuoni na alipojaribu kupiga kelele ili mumewe aamke alikuwa anashindwa,hivyo alikuwa anaomba nimshauri cha kufanya

Nilikaa kimya kwanza nikitafakari haya aliyoniambia,baada ya kimya cha kama dakika 2 hivi nilimuuliza kuhusu lolote analojua kuhusiana na uchawi akaniambia hana analojua zaidi za kusikia story tu mitaani,pia nilimuuliza kuhusu uhalisi wa hayo na alinihakikishia ni kweli kabisa,kiukweli nilishindwa kukubali au kuataa na nilimuambia anipe muda wa kutafakari kidogo

Ndipo leo nikiwa nipo nyumbani na kwakuwa leo sijaenda kwenye shughuli zangu kwa kuwa sijisikii vyema na wakati huohuo sijui cha kumwambia huyu rafiki yangu kutokana na mambo yake kutokuwa na ushahidi na uhakika alinipigia simu niende kumsaidia kupaki vitu kwenye gari kwani anahama nyumba ile.[alikuwa anajua kuhusu kuwepo kwangu home leo]

Nilistuka kidogo,lakini nikajisemea wacha niende nikamuulize kulikoni hukohuko.

Nilifika na kumkuta mkewe pamoja na wanae wakiwa katika harakati hizo za kuhama,nikaamua nitamuuliza baada ya kumaliza harakati hizo maana inaonekana kama kuna jambo kubwa sana lililomfanya ahame ghafla hivyo

Ndipo wakati wa kuhamisha vitu hivyo ndipo kilipotokea kioja kilichonistua sana.
Tulikuwa chumbani tukifungua kitanda mimi na huyu rafiki yangu ili kipakiwe kwenye gari,mule ndani kulikuwa na sofa la kumtosha mtu mmoja na juu yake lilikuwa limewekwa begi kubwa la nguo na mule ndani hakukuwa na mtu zaidi ya mimi na yule rafiki yangu tuliekuwa tumezama kwenye kukifungua kitanda na huku akiniambia baadhi ya vituko vya pale

Unajua kuna vitu mtu huwezi kumuambia na mtu akakuelewa labda tu awe amevishuhudia,na ndio kama hiki changu,kwani ghafla tulisikia harufu ya kitu kinaungua na wote wawili mimi na na rafiki yangu huyu tulitazamana na kisha tukageukia kule tulokokuwa tunahisi kunaungua na ndipo tulipoona moto ukiwaka pale lilipokuwa limewekwa lile begi,yaani kwenye sofa

Nilipigwa pumbuwazi kwanza kwa sababu sofa lile halikuwa mlangoni tungesema labda kuna mtu aliingia kwa kificho na akawasha moto kisha kutoweka wakati sisi tukiwa tumezama kwenye kufungua kitanda,lakini sivyo,sofa lilikuwa nyuma yetu na mlango ulikuwa mbele yetu yaani mtu ili aingie ni lazima tungemuona tu

Ilibidi tuanzishe harakati za kuuzima ule moto lakini cha kushangaza ilionekana ule moto ulikuwa umewaka muda mrefu sana bila sisi kusikia na ulikuwa umeshaliunguza lile begi robo tatu na moto ulikuwa umeanza kushika kwenye sofa

Kwa taharuki tuliuzima ule moto na kufanikiwa na tulilitoa nje lile sofa huku kila mmoja akiwa na maswali mengi sana kichwani

Tulishindwa hata kuuliza maana mazingira tu ya kuwaka moto ule yalifanya tukose ujasiri wa kuuliza kama kuna mtu aliingia mule ndani na kuuwasha ule moto

Yaani mtu aingie ndani na kuwasha moto mpaka begi liungue uwe hujasikia?Ni ngumu sana kueleweka,mkewe rafiki yangu alipouliza kulikoni begi limeungua na sofa tulimwambia tutamueleza kazi ya kuhama ikiisha!

Tulimaliza na tumeahidiana na rafiki yangu kuwa tutakutana kesho jioni ili tuongee zaidi kwani nyumba aliyokuwa anahamia ilitakiwa aifanyie marekebisho kidogo hivyo alihitaji muda kwaajili ya hilo

Nilirudi nyumbani majira ya saa 6 hivi huku nikiwa na maswali mengi sana kuhusiana na ule moto,hadi sasa sijui ni nani aliuwasha na uliwakaje na kwanini

Matukio haya nilikuwa nasimuliwa tu na nilikuwa nahisi labda mengine ni story tu ila leo nimeshuhudia live mimi mwenyewe,sina majibu hadi sasa!

Sina ham kwakweli!

Kuna haja ya kuwa makini na hizi nyumba tunazoishi
Unaweza kwenda kuishi mahali pa ajabu sana!

Mkuu dunia inatumikiwa na nguvu mbili, moja yatoka kwa yule muovu ibilisi na Nyingine kwa Mungu....haya mambo yapo tena kuna makubwa zaidi ya hayo, na hata ya ki Mungu pia yapo yanayompatia sifa Mungu, ila mara nyingi ni ugumu wa mioyo ya wanadamu wa kutokuamini vitu ambavyo hawajavishuhudia kwa macho.
 
Ndugu poleni, kweli mlifikwa sawasawa. Naomba nikuambie, nyumba kama hizo mpelekeni MLOKOLE wa kwelii. Atakaa humo, bila shida na mwisho wa yote mwenye nyumba atashika adabu.
Pale K/koo kuna mwuza nyama mmoja aliipata fresh. Alimhonga nyama mlokole akidhani jioni ni kwenda tu kumgegeda. We, amefika kaambiwa, fedha nilikupa ukazitupa, sikuziokota nemda kaziokote pale buchani kwako. Mimi na Yesu baasi. Mwuza nyama akadhani ni mchezo, alipotuma majitu yake, we, yakamrudi mwenyewe. Mpemba kapiga yowe, Naliwa kibog jamanii.
Natamani kama nyumba hiyo ingekuwa karibu ningeenda leo kuikaa
 
Mkuu hata ukijenga kwako unatakiwa kufanya maombi/sala kubwa sana ya kutakatisha hiyo ardhi uliyojenga maana huwezi kujua huyo aliyekuuzia huo uwanja alikuwa amezindika nini hapo. Wakati mwingine hata mafundi wanaojenga wanatumia nguvu na imani za kishirikina ambazo zinaweza kuathiri maisha yako na familia yako

Hakika mkuu
 
Uchawi upo mbna mkuu

Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums
 
Kaka Eiyer kuna watu wanaitwa wenye nyumba simply kwa kuwa walitangulia kufika mjini ila bila hata kugoogle ni wazi kabisa kuna namna zao wanajua ambazo wametumia kujipatia fedha/mali zilizopelekea kujenga nyumba zinzzowafanya wawe tittled wenye nyuma!

Makafara yametembea sana na manuizo ya ajabu ajabu kwenye nyumba tunazoishi mjini! Just imagine mtu anaishi kwenye banda lisilopigwa walau plaster nje ya mji ilihali mjini ana flats alizojaza wapangaji,kwa nini usitazame mafanikio yake kwa jicho la tatu!

Binafsi nimejiwekea dhamiri juu ya hizi nyumba za kununua ambazo hujui waliojenga waliweka maagano gani na mizimu(naexclude wanaojenga kwa minajili ya real estate) Ni mara mia kujitafutia kajisehemu kako ukajenga kwa kuunga unga huku ukiomba yasikufike makuu kuliko kuingia kwenye haya majanga!

Mkuu kwani ukitafuta pa kujenga hicho kiwanja unajua anaekuuzia alikipataje na aliweka maagano gani?
 
Ukisikia 'Utamu wa Yesu' ndo kwenye matukio kama hayo, ukiwa na Yesu walaaa,,utayasikia tu!!
 
Hata huyu jamaa yangu hakudai kodi
Unadhani ujasiri wa kudai kodi utautoa wapi?


Halafu unadhani ni Bugando tu?
Hii makitu ya kuuza maji ya maiti niliwahi kukutana nayo mahili kwingi sana na mikoa tofauti tofauti!
maji ya maiti ni dili sana hasa kwa waganga ambao wanataka kuwarudisha watu kazini waliofukuzwa , vile vile fimbo ya kipofu , kucha za mwehu nk , yaani ni majanga tu
 
bora wewe ulikuta na ukaona mauza uza kama hayo , kigoma ujiji kulikuwa na nyumba kama hiyo ikifika usiku mnachapwa fimbo na wanao wachapa hamuwaoni na kelele hazisikiki mnazopiga, yaani ilikuwa kila siku watu wanahama na kuingia , sijui ilikuwa wanaogopa kuambiana . dawa ni kumpata mchungaji kama ni mkiristo kufanya maombi , na kama muislam dua na mafusho inaweza kukimbiza hizo roho chafu
 
Yaani hivi vituko ni vingi sana
Unaweza kuhamia kisha ukaambiwa wanaume humo huliwa kibog sijui inakuwaje aisee!!!!!!

hii sasa kali aisee...unaweza jikuta umelala huku umevaa jinzi kama nane kuhofia kugeuzwa rostmaini!!!
 
Mwenye jukumu la kufanya hayo si mwenye nyumba mkuu?
Sasa wapangaji watahusikaje?

Inawezekana kwa aina moja au nyingine mwenye nyumba anahusika au anapenda hali hiyo kwa wapangaji wake!
Kama angekuwa hapendi angekuwa amechukua hatua!

Je huyo rafiki yako aliwasiliana na mwenye nyumba wake na kumweleza hayo matatizo?
 
maji ya maiti ni dili sana hasa kwa waganga ambao wanataka kuwarudisha watu kazini waliofukuzwa , vile vile fimbo ya kipofu , kucha za mwehu nk , yaani ni majanga tu

.....hehehe, "mtaalamu!" Wewe!
 
Mnahamiaje nyumba mpya bila kufanya dua ama maombi? Mdogo wangu eiyer, huyo mana tayari keshaingiwa jini mahaba. Hawana ujanja hapo, kama ni wakristo ama waislamu ni muhimu waende kwa ajili ya maombi/dua.

Bwana asipoulinda mji wakeshao wafanya kazi bure.
 
Eiyer poleni sana kwa yaliyowakuta , umenikumbusha niliwahi kuishi mtaa flani hapa bongo na ndio kwanza tulikua tumefunga pingu za maisha. Basi kumbe mtaa tuliopanga wamama walikua kila atakaeshika ujauzito alikua hapati mtoto i.e ilikua lazima atajifungua bahati mbaya tu. Na niliwahi tembelewa mara kadhaa na vigogo wa mtaa ule. Tuliamua kutohama mtaa ule na nilisema wa kwangu atazaliwa na atakua tu. Ngoja nifupishe habari , mara baada ya kuutambua vituko vya mtaa ule tulifanya maombi na tulipata ushindi . HAkuna madhara yoyote yaliyotupata maana Bwana alitupa ulinzi tosha. Sasa huyo ndugu yako mfahamishe kuwa uchawi haujawahi kuizidi nguvu ya Mungu cha msingi ni kufanya maombi na kukemea nguvu za yule muovu.
 
Last edited by a moderator:
Dah!!!! Hii inatisha sana!!! Bora ilikuwa ni nyumba ya kupanga, fikiria kama jamaa ndio alikuwa ameinunua hiyo nyumba kwa mamilioni chungu nzima!!!....ingekula kwake.
 
Hivi vitu mbona hata ulaya vipo sana. Angalieni au m download vipindi vya Haunted vinarushwa na channel ya Investigation Discovery!! Ni noooooma aisee. Sasa si unajua wenzetu ni wabishi wana chunguzaga mpaka kieleweke, ila wao wenyewe wanachemsha na science. Kichekini kina sisimua!

Kweli kaka. Naona nchi ambayo naishi hivi sasa, watu wanapotea kiajabu ajabu nyumba baadhi zina vibweka vya kufa mtu, lkn Kama ulivyosema, kwa vile wenzetu wabishi wanaamua kuzama kwenye uchunguzi lkn juu ya hilo bado wanaambulia patupu. Mwisho wake nao wanarudi kwenye Kalumanzira wao. Dunia hii tunayoishi ina mambo sana.
 
Dunia ina mambo........
Na mengine ni yakusikia tu............

Kuna jamaa yangu alikuwa anatafuta nyumba ya kuishi[kupanga],alinijulisha hili jambo na tulisaidiana kutafuta kuepuka usumbufu wa madalali na gharama zao

Hatimae wiki moja iliyopita alifanikiwa kupata nyumba eneo la Nyakato Buzuruga,hapa jijini Mwanza,na alihamia siku hiyo hiyo.Ilikuwa ni nyumba nzuri sana na iko kwenye hali nzuri tu

Siku 4 baada ya kuhamia yeye na mkewe na watoto wao wawili jamaa alinipigia simu akiniomba jioni baada ya mihangaiko yetu niende nyumbani kwake kuna mambo hayaelewi kidogo kuhusiana na nyumba ile

Jioni nilikwenda na aliniambia kuwa mara nyingi nyakati za usiku wakati amelala na mkewe huwa wanarushiwa matonge ya ugali kitandani na wakati mwingine kumwagiwa mchanga,na kila yalipokuwa yanatokea hayoi matukio huwa anawasha taa ili kuona labda ndani kuna mtu lakini huwa kunakuwa hakuna tofauti ya yeye na mkewe,na akirudi tena yanarudia yaleyale,na kali zaidi usiku wa kuamkia siku niliyokwenda mkewe aliingiliwa kingono na mtu ambae alikuwa hamuoni na alipojaribu kupiga kelele ili mumewe aamke alikuwa anashindwa,hivyo alikuwa anaomba nimshauri cha kufanya

Nilikaa kimya kwanza nikitafakari haya aliyoniambia,baada ya kimya cha kama dakika 2 hivi nilimuuliza kuhusu lolote analojua kuhusiana na uchawi akaniambia hana analojua zaidi za kusikia story tu mitaani,pia nilimuuliza kuhusu uhalisi wa hayo na alinihakikishia ni kweli kabisa,kiukweli nilishindwa kukubali au kuataa na nilimuambia anipe muda wa kutafakari kidogo

Ndipo leo nikiwa nipo nyumbani na kwakuwa leo sijaenda kwenye shughuli zangu kwa kuwa sijisikii vyema na wakati huohuo sijui cha kumwambia huyu rafiki yangu kutokana na mambo yake kutokuwa na ushahidi na uhakika alinipigia simu niende kumsaidia kupaki vitu kwenye gari kwani anahama nyumba ile.[alikuwa anajua kuhusu kuwepo kwangu home leo]

Nilistuka kidogo,lakini nikajisemea wacha niende nikamuulize kulikoni hukohuko.

Nilifika na kumkuta mkewe pamoja na wanae wakiwa katika harakati hizo za kuhama,nikaamua nitamuuliza baada ya kumaliza harakati hizo maana inaonekana kama kuna jambo kubwa sana lililomfanya ahame ghafla hivyo

Ndipo wakati wa kuhamisha vitu hivyo ndipo kilipotokea kioja kilichonistua sana.
Tulikuwa chumbani tukifungua kitanda mimi na huyu rafiki yangu ili kipakiwe kwenye gari,mule ndani kulikuwa na sofa la kumtosha mtu mmoja na juu yake lilikuwa limewekwa begi kubwa la nguo na mule ndani hakukuwa na mtu zaidi ya mimi na yule rafiki yangu tuliekuwa tumezama kwenye kukifungua kitanda na huku akiniambia baadhi ya vituko vya pale

Unajua kuna vitu mtu huwezi kumuambia na mtu akakuelewa labda tu awe amevishuhudia,na ndio kama hiki changu,kwani ghafla tulisikia harufu ya kitu kinaungua na wote wawili mimi na na rafiki yangu huyu tulitazamana na kisha tukageukia kule tulokokuwa tunahisi kunaungua na ndipo tulipoona moto ukiwaka pale lilipokuwa limewekwa lile begi,yaani kwenye sofa

Nilipigwa pumbuwazi kwanza kwa sababu sofa lile halikuwa mlangoni tungesema labda kuna mtu aliingia kwa kificho na akawasha moto kisha kutoweka wakati sisi tukiwa tumezama kwenye kufungua kitanda,lakini sivyo,sofa lilikuwa nyuma yetu na mlango ulikuwa mbele yetu yaani mtu ili aingie ni lazima tungemuona tu

Ilibidi tuanzishe harakati za kuuzima ule moto lakini cha kushangaza ilionekana ule moto ulikuwa umewaka muda mrefu sana bila sisi kusikia na ulikuwa umeshaliunguza lile begi robo tatu na moto ulikuwa umeanza kushika kwenye sofa

Kwa taharuki tuliuzima ule moto na kufanikiwa na tulilitoa nje lile sofa huku kila mmoja akiwa na maswali mengi sana kichwani

Tulishindwa hata kuuliza maana mazingira tu ya kuwaka moto ule yalifanya tukose ujasiri wa kuuliza kama kuna mtu aliingia mule ndani na kuuwasha ule moto

Yaani mtu aingie ndani na kuwasha moto mpaka begi liungue uwe hujasikia?Ni ngumu sana kueleweka,mkewe rafiki yangu alipouliza kulikoni begi limeungua na sofa tulimwambia tutamueleza kazi ya kuhama ikiisha!

Tulimaliza na tumeahidiana na rafiki yangu kuwa tutakutana kesho jioni ili tuongee zaidi kwani nyumba aliyokuwa anahamia ilitakiwa aifanyie marekebisho kidogo hivyo alihitaji muda kwaajili ya hilo

Nilirudi nyumbani majira ya saa 6 hivi huku nikiwa na maswali mengi sana kuhusiana na ule moto,hadi sasa sijui ni nani aliuwasha na uliwakaje na kwanini

Matukio haya nilikuwa nasimuliwa tu na nilikuwa nahisi labda mengine ni story tu ila leo nimeshuhudia live mimi mwenyewe,sina majibu hadi sasa!

Sina ham kwakweli!

Kuna haja ya kuwa makini na hizi nyumba tunazoishi
Unaweza kwenda kuishi mahali pa ajabu sana!
dawa ni yesu tu mwaminini alafu tumia jina la yesu kukemea uchawi soma biblia yatakusaidia bila yesu popote utayakuta coz wachaw wapo kila sehemu na wanaweza kukufuata popote mi usiku wa leo walimbana mtoto wangu nilizani anaumwa toka saa 5 mpaka saa 8 mtoto analia bembeleza wapi ndipo niliposikia omba nikawakemea kwa jina la yesu wakatoweka mtoto palepale akalala mpaka asubuh hii bado kalala jina la yesu lina magic power
 
Mara nyingi wanapatwa na hayo huwa wanajihusisha nayo kwa nmna moja au nyingine.
 
Dah!!!! Hii inatisha sana!!! Bora ilikuwa ni nyumba ya kupanga, fikiria kama jamaa ndio alikuwa ameinunua hiyo nyumba kwa mamilioni chungu nzima!!!....ingekula kwake.
Me ndo maana siafiki hili swala la kununua nyumba,maana zina mengi sana
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom