Nilichokishuhudia leo...!

Nilichokishuhudia leo...!

dah hiyo ni ngumu kumesa aiseh,,,,,,,,,,mwambie awakomalie hakuna kuipangisha hadi mkataba wake utakapoisha la sivyo mpangaji atakayeingia amrudishie pesa pesa maana hiyo ndio njia pekee atakayoweza kurecover pesa yake.
 
Ni bora kujitutumua kujenga yako Mkuu, Naafikiana nawe kabisa hizi nyumba baadhi zina vitu vya ajabu sana na vinaweza kutokea wakati wowote ule usiku na mchana pia.

Me ndo maana siafiki hili swala la kununua nyumba,maana zina mengi sana
 
Ni kweli
Huyu jama yangu alikuwa ni moja kati ya wale watu waliokuwa wabishi sana kwenye mambo haya,lakini sasa atakuwa ameipata fresh na sasa atajua kuwa kuna ulimwengu mwingine ambao hatuuoni na ki ukweli ni wa ajabu sana
Yaani ibilisi akikutanaga na watu wasiomjua Mungu huwaonea sana. Huwa nina hasira nae sana na mtaani kwetu tumemfurumusha kabisa. Mahala nilipojenga kibanda changu pia kulikua na watu wazito kwenye mambo ya giza napo tulipohamia tu tulihakikisha wafuasi wa ibilisi wanafunga virago au wanaacha kazi ya ibilisi. Kulikua na waganga wengi ndugu yangu wote walihama mmoja baada ya mwingine tulihakikisha mtu haruki na ungo usiku. Haya yote alitushindia Yesu hivyo sifa na utukufu apewe yeye. Nadhani huyo ndugu hii kitu itamsaidia kuamini kwa sababu ibilisi hataacha kumchezea ni mpaka atakapoamua kumtimua kwa hili jina lipitalo kila jina "YESU"
 
Dah!!!! Hii inatisha sana!!! Bora ilikuwa ni nyumba ya kupanga, fikiria kama jamaa ndio alikuwa ameinunua hiyo nyumba kwa mamilioni chungu nzima!!!....ingekula kwake.
Hahahahahaha hapo lazima ingempasa aamini hii nguvu nyingine iliyo juu ya vyote. Pia ni ngumu kukuta eneo safi kabisa halina mauza uza . Kikubwa ni kuwa na imani tu na kugangamala mpaka kieleweke. Kumbuka kuna watakaokuzunguka nao huwajui background yao na wanasema ni rahisi kuchagua rafiki lkn jirani huwezi kuchagua .
 
dah hiyo ni ngumu kumesa aiseh,,,,,,,,,,mwambie awakomalie hakuna kuipangisha hadi mkataba wake utakapoisha la sivyo mpangaji atakayeingia amrudishie pesa pesa maana hiyo ndio njia pekee atakayoweza kurecover pesa yake.
Kama mwenye nyumba hakuonyesha kujali walipomueleza matatizo wanayoyapata sasa huenda anatumia ujanja huo kujipatia pesa. Anafanya kusudi kuwafanyia wapangaji mauza uza ili waache kodi zao na maisha yanasonga. Wakimdai atawatembelea huko huko waliko mbona watajuta hata kudai hizo pesa, safari hii waweza kujikuta wako njia panda wamechapa usingizi. Unajua wasingehama wangewatafuta watu wenye imani wafanye huduma mahala pale na mambo yangekua shwari.
 
Maji ya baraka ni jibu la yote,,,

kuna nyumba moja ipo manzese,,,,hiyo nyumba kila anapokuja mgeni ,,asubuhi saa kumi na moja lazima aniamshe anataka kuondoka,,,,anadai nyumba haifai kutokana na vituko alivyofanyiwa usiku,,hasa hasa wageni wangu wa kike,,lakini mimi nalala poa tu,,haya mambo yapo sana tu,,,
 
Yaani ibilisi akikutanaga na watu wasiomjua Mungu huwaonea sana. Huwa nina hasira nae sana na mtaani kwetu tumemfurumusha kabisa. Mahala nilipojenga kibanda changu pia kulikua na watu wazito kwenye mambo ya giza napo tulipohamia tu tulihakikisha wafuasi wa ibilisi wanafunga virago au wanaacha kazi ya ibilisi. Kulikua na waganga wengi ndugu yangu wote walihama mmoja baada ya mwingine tulihakikisha mtu haruki na ungo usiku. Haya yote alitushindia Yesu hivyo sifa na utukufu apewe yeye. Nadhani huyo ndugu hii kitu itamsaidia kuamini kwa sababu ibilisi hataacha kumchezea ni mpaka atakapoamua kumtimua kwa hili jina lipitalo kila jina "YESU"

Asante sana mama!
Ki kwetu tunasema "aika mae"
Au "wabheja"
 
......hahahaha, popobawa?!
Halafu ndio miezi yake hii mwisho wa mwaka!

Hivi ndio huyo huyo anaesababishaga na ajali za nyakati hizi?
 
mi naona ni style ya mwenye nyumba kuchkua kodi na kukufkuza then aje mwingine hivyo hivyo.. hao ndio wazee wacheza bao huku pesa inaingia.. 18

 
maji ya maiti ni dili sana hasa kwa waganga ambao wanataka kuwarudisha watu kazini waliofukuzwa , vile vile fimbo ya kipofu , kucha za mwehu nk , yaani ni majanga tu


uvugizi umesahau na mwiko wa gereza!! acha kabisa, ukiupata huo hoteli yako itauzaje? huu uzi kiboko!!
 
Mwenye nyumba atakuwa ameweka mavitu yake. Rafiki yangu alipata nyumba yake ilikuwa balaa ukienda toilet usiku wa manane mlango haufunguki alf pesa hazikai ukiingia na pesa ndani ya nyumba kama ni 102000 basi utabakiziwa 2000 pata picha unakaa mwenyewe kumbe mwenyenyumba anajipatia mapato kirahisi. Bahati nzuri rafiki yangu mtoto wa mjini alimfata mwenyenyumba na panga mbona alitoa pesa yote ya kodi msela akahama.

Haya mambo yapo sana kabla hujaamia kwenye nyumba unatakiwa uchunguze na ujue huo mtaa bahati mbaya watu wapo busy na kazi ndio maana utaenda kichwa kichwa tu
 
Kazi ndogo sana hiyo! hata isinekugarimu hata buku 50, Tafuta Padri/shekhe apige maombi ya kufa mtu! kama huamini katika dini tafuta mganga akuwekee TEGO, mtu akitia mguu kesho unamkuta mlangoni uchi!

Kwa kifupi, ni wenye nyumba wengi wanafanya hivo kuapata hela ya haraka haraka, ila wakikutanaga na mtu ambae anaijua hela vizuri ndio huwa wanakomaga! manake baada ya aibu kila mtu atakuwa anapitia njia yake

kwa yote poleni sana! ila ndio vizuri mjenge na nyie kila siku kupanga tu aaaahhhh!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom