Dah!!!! Hii inatisha sana!!! Bora ilikuwa ni nyumba ya kupanga, fikiria kama jamaa ndio alikuwa ameinunua hiyo nyumba kwa mamilioni chungu nzima!!!....ingekula kwake.
Eiyer poleni sana kwa yaliyowakuta , umenikumbusha niliwahi kuishi mtaa flani hapa bongo na ndio kwanza tulikua tumefunga pingu za maisha. Basi kumbe mtaa tuliopanga wamama walikua kila atakaeshika ujauzito alikua hapati mtoto i.e ilikua lazima atajifungua bahati mbaya tu. Na niliwahi tembelewa mara kadhaa na vigogo wa mtaa ule. Tuliamua kutohama mtaa ule na nilisema wa kwangu atazaliwa na atakua tu. Ngoja nifupishe habari , mara baada ya kuutambua vituko vya mtaa ule tulifanya maombi na tulipata ushindi . HAkuna madhara yoyote yaliyotupata maana Bwana alitupa ulinzi tosha. Sasa huyo ndugu yako mfahamishe kuwa uchawi haujawahi kuizidi nguvu ya Mungu cha msingi ni kufanya maombi na kukemea nguvu za yule muovu.
kuna jamaa yangu alipata nyumba ila akaambiwa haruhusiwi kwenda chooni mida ya jioni kuanzai saa 12:00 mpaka saa 1:00
Mimi maeneo ya Kijitonyama kwa Ali Maua nilionyeshwa nyumba ambayo masharti yake ni kuwa ni Marufuku kabisa kuleta Kitimoto pale hata kama nikila kitimoto baa siku hiyo niwe makini nihakikishe nimenawa na maji ya moto na Sabuni. Baada ya kuambiwa hivyo mimi huyo nikasepa!!!
Mkuu si hua wanasema eti kitimoto ni kiboko ya wachawi?
Sijui labda ! Kwani huyu mzee alikuwa kama sikosei Mjumbe wa nyumba kumi lakini masharti yake ambayo yalikuwa yameandikwa / chapishwa vizuri tu na bei ilikuwa nafuu kidogo ukilinganisha na nyumba nyingine za maeneo hayo.
Mkuu huyu nadhani kilichomfanya akafanya hivyo labda ni imani ya kidini!!!!!!
Kwenye nyumba za kupanga usiache kwenda na mfupa au pisi la kitimoto
Baba paroko vipi tena nilitegemea ungepambana nao kwa jina la Bwana wa majeshi nawe ukakimbia hahahaha,kuna jamaa pia alijenga nyumba nzuri mahali fulani wataalamu wakaitenda mambo wapangaji wakiingia wanaona mara nyumba inatimuka vumbi kila namna ya mikasa,wapangaji wakaiogopa ikakaa miaka kadha akatokea jamaa mmoja mlokole wakamueleza juu ya utata wa nyumba yeye akasema hamna shida atatinga,akaenda kumuona mwenye nyumba akamwambia wewe ukiweza kukaa kakae tu hata kodi usilipe....kajamaaa na upako kakatinga full kukemea kwa jina Yesu usiku mpaka maruweruwe yakaisha yule mwenye nyumba alipoona kajamaa kapo tu siku zinasonga kanadunda akaamua kukadai kodi hahahaha.
hata mim nilishawahi sikia hvyo....tena wanasema ukipata ile pua yake ndo nzuri zaidi.....ila yote ya yote.....YESU KRISTO ndo kiboko yao...Mkuu si hua wanasema eti kitimoto ni kiboko ya wachawi?
jaribu kuangalia hii post imeletwa lini ....Tukio limetokea leo maana hujaenda kazini ukimsaidia rafikio kuhama.
Ila umerudi kwako SAA SITA.
SAA HIZI NI SAA TANO.
Maelezo yako hayaeleweki.
Tukio limetokea leo maana hujaenda kazini ukimsaidia rafikio kuhama.
Ila umerudi kwako SAA SITA.
SAA HIZI NI SAA TANO.
Maelezo yako hayaeleweki.