Niliapa kutosimulia

Niliapa kutosimulia

story ya uongo hii, umebugi uliposema eti hukusave namba yake alipokutumia vocha kwa simu, hapo ndo ulipoharibu, kwa jinsi ulivyomsifia eti usisave namba? wapi wewe!

mkuu sikusave no..kwanza ni kwasababu alikua mkimya sana kwenye gali so nikajua hayuko interested na mimi kabisa..pili alisema ni mwenyeji wa iringa na dar kaja kwa interview tu so ikanikatisha tamaa, tatu kumsifia ni kwasababu ni mzuri kweli..na niliona muda wa siku tatu maybe usingetosha kumpata mtoto mzuri kama huyu...LAKINI HAIKUA HIVYO MKUU..nilipatikana
 
Kama ni mtu wako wa karibu kwanini usimsimulie yaliyokusibu huko Iringa? Au mwenzetu Shs. milioni 10 kwako si kitu? Halafu kwenye stori yako inaonyesha ulipiga bao moja tu...Sasa Shs milioni 10 ziende kwa bao 1 tu? Na hata huyo taxi driver aliyeitwa na Kalinga alikuwa kapangwa akutishe...Ndio maana akawa anakutisha kwenye taxi !

sikufichi M10 ni pesa nyingi kwa mtu yeyote mkuu...sio mimi tu
 
Nertwork ilianzia kwa babu alokua anamlindia seat,haikua tu coencidence

Ungejua si ungemfaidi huyo cleopatra toka day1 alivyokufikisha tu hotelini, sasa show moko kwa 10M kweli?
 
aisee pole sana ndugu, ila ni vizuri kwenda kupima na VVU mana huenda huyo dada ndo mchezo wake huwezi jua amelala na wangapi
 
Samahani mwenye andiko hili. Nimeyakuza maandishi ili nisome kwa urahisi. Kwa wengine "mnaoposti threads" zenu tafadhali jitahidini kukuza maandishi ili kutusaidia sisi tunaopata shida kusoma maandishi madogo.


"Asubui na mapema naanza safari kutoka mitaa ya tabata kuelekea ubungo, ni mida ya saa kumi na moja, rafiki yangu julius kajitolea kunisindikiza ili niwahi basi la SUMRY la kwanza liendalo mbeya. Ofcoz safari yangu inaishia iringa lakini ni mara yangu ya kwanza kwenda huko so nataka niwahi kufika ili nipate nuda wa kutafuta hotel nzuri ya kufikia.

Nakumbuka jana wakati nakata tiketi niliamua kuchagua makusudi seat no E.2 iliyo koridoni baada ya julius kunipa ushauri kuwa madem wanapenda sana seat za dirishani so nichague ya koridoni ili kutoa nafasi kwa mdada kukaa pembeni yangu. Kimsingi hakutaka niwe bored sana katika hii safari ndefu so akanambia nikikaa na msichana kutakua na vistory vya hapa na pale (sina uhakika kama kweli ndo yalikua malengo yake halisi)

Ni mtu kama wa kumi hivi kuingia ndani ya basi, katika seat E.1 namkuta mzee wa makamo, kwa mbali natabasam,ofcoz moyoni namcheka julius, kachemka na theory zake za kitaa. Namsalimia mzee kisha nakaa. Saa kumi na mbili kamili tunaanza kutoka ubungo, trafiki katika geti la kutoka wanakagua magari so tunasimama kwa muda. Mara mtu anagonga body la basi kwa nje, konda anafungua mlango kwa nyodo, "mnaniacha jamani" sauti nzuri ya kike inalalamika, huku akionyesha tiketi yake. Abilia wote tunaangalia mlangoni kushadadia ni nani huyu aliyachelewa namna hiyo.

Duh, anaingia mtoto mzuri, binti wa makamo mrefu kiasi, kabalikiwa umbo la ile namba maarufu ya kiungo mshambuliaji a.k.a namba nane. Anaangalia juu katika seat namba kuitambua seat yake, tayari basi risharuhusiwa, na tuko mataa ya ubungo. Mara anasimama pembeni yangu na kumuuliza mzee seat no yake ni ngapi. Nashtuka kidogo na kumuomba mzee tiketi yake nipate kumsaidia kuthibitisha!! lahaula mzee kakosea seat, seat yake ni F.1 nyuma yangu. Bila hiyana anampisha mrembo na kuhamia nyuma. Nashindwa kujizuia nacheka kichinichini sababu utabili wa julius umejidhihirisha ingawa kwa kuchelewa.

Dem ananisalimia, kisha anakaa, headphone maskioni hana muda na mengineyo,.Moyoni namsifia kwa uzuri wake huku nikimuangalia kwa kuibia. tunavuka kimara nafumba macho kufidia usingizi wangu niliokatisha.
Mpaka CHALINZE hatujasemeshana neno lolote, Duh huyu dem kauzu, ni muziki tu na yeye.Isiwe taabu napotezea nafumba macho tena.

Morogoro hiyo, napiga moyo konde natoa elfu kumi namuomba aninunulie vocha kwa dirishani, "ya sh ngapi" duh najikuta nasema ya pesa yote. Muuzaji ana moja moja,usumbufu kukwangua nikakataa. Usihofu ngoja nikuhamishie mimi coz nina air time ya kutosha. MMH anaomba no yangu nampa ananihamishia elfu kumi then anabaki na pesa.

namshukuru then namuuliza anaitwa nani, PRISCA na wewe, nikamwambia..then nikamuuliza iringa ni mwenyeji, akanambia ni kwao, alikuja dar kwa interview tu. Ikabidi ni confess ugeni wangu na kumuomba aniambie wapi naweza kufikia(HOTEL). Dem akanambia nisihofu atanisaidia then tukapiga kimya tena. Mpaka KItonga ndo katoa headphone tena.."kaka hii ndo kitonga kama uliwahi kuisikia". NIkachomoza shingo kuchungulia kidogo lahaula kitonga inatisha lakini pia macho pembeni kifuani kwa mrembo kwa juu kidogo naweza kuona bolibo zake zilivyokaa vizuri, mmh huyu dem mzuri.

natamani kitonga iendelee mpaka iringa but ndo tushaivuka ivyo so najiadjust, then safari inaendelea. Kimya mpaka IRINGA tunashuka, Prisca anaita tax ananambia niingie anipeleke kwa hotel coz kuna hotel nzuri jilani na maeneo anayoishi. Mojakwa moja mpaka hotel inaitwa wilolesi.Prisca ananisaidia bag ya laptop na mie nabeba mizigo mingine mpaka reception. napata chumba prisca ananiaga then kaondoka.

Mawazo yangu yote kwa prisca, duuh DAR kuna madem lakini huyu mtoto ni moto!! nimeamua kuagiza msosi chumbani, hii baridi ya iringa sitoki humu chumbani haki ya nani. SAA tatu usiku nakula msosi wangu, mara SMS "mambo vp, umelala" duh hii no kama naijua nimeiona wapi?? "sijalala nakula, sorry nani mwenzangu" mala "mimi prisca kwan nilivyo kuhamishia vocha huku save my no"

Hatari, moyo mbiombio, nikajibu "sikuserve" akanitext "Good night" then kimya.Kesho yake baada ya mizunguko yangu na mwenyeji wangu Mr. Kalinga . nikarudi hotelini. Kama kawaida nikaagiza msosi kwa chumba mida ya tatu kasoro, nimemaliza kula tu mara ko koko.. "karibu" nikijua ni muhudumu ...yallabi tobaaaa..PRISCA huyu apa. kanisalimia na tukajuliana hali then nikamuuliza kulikoni mida hii tena bila taarifa. Dem kaanza kunisuta.."unadhani jana sikukuona ulivyokuwa unaniangalia, ulivyokua unanichungulia maziwa" ofcoz najua nilikuvutia na ukweli hata mie unanivutia sana" duh majanga.. dem kakaa kitandani kanishika mkono, story mbili tatu mara kiss, kanivua shati bado siamini wala kutambua nini kinaendelea kapiga jeans yangu chini, azam Fc a.k.a lambalamba ikaanza..kapiga koni kashuka mpaka nazi zinazoning'inia,..walai prisca kaamia maskioni..nduguyenu nimekata kauli... kanilamba mpaka macho, prisca hatariiiii..katoa nguo zake zote..nikaona isiwe kesi nikamvamia na mimi, ndani ya blanketi ni pump za kutosha,..napiga round ya kwanza ..nakumbuka nimecheza PEKUPEKU. yalaaaah

Prisca akavaa na kunambia "ntakuona kesho" then kaondoka..duh huyu dem jini?? afu nimepiga peku??mbona haongei sana??why kanifanyia haka ka mchezo kirahisi namna hii?? siku yangu ya mwisho kuwa iringa niko na Mr karinga baada ya mambo yetu. Then ananambia kampigia simu wife wake aje kutujoin ili anitambulishe, ni wazo jema so napiga ndovu yangu huku tukimsubili shemeji..DUUH bajaji si Gari.. PRISCA huyuapa, kavaa pete ya ndoa anakuja moja kwa moja na kukaa pembeni ya KARINGA..Bia imenikwama, moyo unanidunda. Natambulishwa na Mr Karinga kwa prisca, ananambia ni juzi tu alienda Dar kufanya interview CRDB. Mwenzenu sina Kauli...Mr. kalinga anaendelea kuongea, ananambia kuna vitu anataka kunionyesha...namuuliza vinahusu biashara tunayoianzisha, ananisogezea simu yake, Mtumeeee..ni picha zangu na prisca ndani ya mahaba pale wilolesi...naanza kutetemeka ..prisca anauliza vipi, Karinga anasema anajua ushenzi tuiofanya, anamuonyesha prisca zile picha, HE ..prisca anaanza kulia kwa chini chini..karinga akasema ili asinichukulie hatua yeyote niondoke kesho na nisikanyage tena iringa..dUH Sijawai kukamatwa ugoni..naomba msamaha..jamaa anaita tax na kuniamuru niondoke..namuuliza vipi kuhusu MILLION 10 zangu tilizolipia jana mashambani, coz hataki kuniona tena iringa. Jamaa akawa mbogo, kasimama katoa bastora..."unataka nikuue kwa kutembea na mke wangu" duh isiwe kesi nikaomba msamaha nikaingia kwa tax aliyoniitia nikaondoka. Njiani dereva anamsifia karinga kuwa ni mnyama hatari, (labda kunitisha) ...

Keshoyake asubui huyo ndani ya sumry mpaka dar...nikaanza kuntafuta rafiki yangu michael aliyenikutanisha na KARINGA na wakanipa mchongo wa biashara hiyo ya iringa..duhhhhhhh michael hayupo kwake, naambiwa kaenda south africa..isiwe taabu... naenda mpaka kwao mbez louis..babayake ananambia michael hakumuaga pia sikuizi haendi hata kumsalimia...nikaamua kumpigia prisca ili nimuulize kama amewahi kumjua michael...duh hapatikani..

Ngoja nimsubili anyway coz michael ni mshikaji wangu wa kitambo.....miez sita ..hakuna mtu..Mpaka leo ni miaka miwili michael hajarudi dar.

SIjui nilitapeliwa (a pre-meditated scum) au ni chain of jinx or ni mshahara wa uovu sijajua ila hata JULIUS sijawahi kumsimulia kisa hiki licha ya kuniuliza mara kwa mara why sijaenda tena kufuatilia biashara zangu za iringa.

Niliapa kutosimulia mtu but lea nimeamua kuiachia"
 
BIA BORA PIC.png




nnakusubiria
 
Back
Top Bottom