Niliambukizwa HIV na mtu niliyemwamini!

Niliambukizwa HIV na mtu niliyemwamini!

After all u r not the first or the last so be strong

Sent from my BlackBerry 9700 using Jamii Forums
 
Mimi kwenda kupima labda niwe naharisha kama ngisi dhofle hali. Niwe nimishajikubali ila naenda kupima kupata uthibitisho tu. Labda pia nipigwe sindano ya usingizi nikizinduka nipo angaza.
Maisha yenyewe presha tupu, halafu nikijitambua marehemu mtarajiwa hapo chacha!!

E bana hata mie nilikuwa ninawaza hivyo hivyoooo
 
Pole sana kaka. Ila ujue yasiyowezekana kwa wanadamu kwa Mungu yanawezekana. Waweza kumuendea Mungu kwa imani yakuponywa na akakuponya. Yeye anasema je kuna jambo gumu lolote nisiloliweza mimi Mungu? Tatizo sisi wanadamu tumekuwa tukim rate kuwa hili anaweza na hili hawezi na mwisho tunaendelea kuteseka nakubeba mizigo mizito unnecessarily. Nakutia moyo mwendee Mungu kwahitaji lakutaka kuponywa na siyo kutiwa moyo wakuishi na matumaini. Keep faith pray continuously weka agano naye kuwa akikuponya utamfanyia nini then usubirie uaminifu wake. Yeremia 29:11-12.
Ubarikiwe

Heshima kwenu wakuu.

Poleni na majukumu ya kila siku. Hili suala ni gumu kuliko linavyofikirika na jamii na watu ambao hawajapatwa na mikasa migumu. Ndio maana unyanyapaa unaendelea kutawala sana humu nchini na tatizo linazidi kushamiri. Nilikuwa na mchumba ambaye nilimpenda sana na ndiye niliyemuweka kuwa chaguo langu la maisha.

Mwanzoni mwa uhusiano wetu tulikuwa tukifanya mapenzi kwa kutumia condom na baadaye tulikuja kuacha kutumia baada ya kupima several times na kuona tupo vizuri na tulikuwa tumeshakubaliana kuja kuishi pamoja. nilimtambulisha kwa ndugu zangu kama ndiye ndugu yao atakayeongezeka na yeye alinitambulisha kwa baadhi ya ndugu zake.

Miaka ilivyozidi kwenda niliona mabadiliko kwa mwenzangu kitabia kwani kuna wakati alikuwa akinidanganya kwamba amesafiri kumbe yupo na hajaondoka. Kumbe mwenzangu alishaanzisha uhusiano na wazee wa mujini wenye pesa zao hivyo akawa ananipotezea kwani kwa wakati huo ndo nilikuwa namalizia mwaka wangu wa mwisho chuoni.

Hali ilizidi kuwa mbaya zaidi kwani ilifika kipindi akanambia ile mipango tuisitishe. nilipomuuliza kwa nini, hakuwa na jibu la wazi. Ilinichanganya sana lakini nilipata faraja kutoka kwa rafiki zangu na ndugu nikatulia. Baada ya miezi kama sita kupita niliamua kwenda kupima na nikagundulika kwamba niko na maambukizi ya VVU, nilichanganyikiwa sana na niliona kama hakuna haja ya kuishi tena.

Sikumwambia mtu mwingine zaidi ya doctor mmoja na mimi mwenyewe kuugulia maumivu yangu peke yangu ila kuna wakati ndugu na jamaa walikuwa wakiniona nimebadirika ila nawaambia hakuna shida yoyote na nipo kawaida. Nilijitahidi kutokukaa peke yangu kwani mawazo ndo yangenizidia.

Mpaka sasa hivi nipo vizuri na nna afya njema ila napata wakati mgumu sana kwani wasichana wengi wanaonesha dalili za kutaka kuwa na uhusiano na mimi lakini nawaonea huruma sana kwani inaniuma sana nikifikiria kumwambukiza mtu mwingine. Wengi wao nimekuwa nikiwakwepa mpaka wengine wananitangazia kwamba jogoo wangu hawiki, huwa inaniuma sana kwani sitaki wajue na sipendi kuwafanya wawe kama mimi.

Nisiwasumbue sana, naomba nihitimishe kwa kusema; hili tatizo ni gumu sana hasa unapokuwa wewe ndiwe 100%. Tupigeni vita unyanyapaa ili watu wasiwe na mawazo ya kwamba TUFE WENGI. Pia unayemnyanyapaa hujui aliupata vipi kwani si kila mwenye VVU alikuwa kuruka njia. Kuna wengine wameupata kutoka kwa watu wanaowaamini sana! Na wengine miaka ya leo wamezaliwa nao hivyo sio kosa lao kwa hapo walipo.

SAY NO TO STIGMA BUT PROTECT YOURSELF FOR THE BEST OF YOU ALL.
 
Mimi kwenda kupima labda niwe naharisha kama ngisi dhofle hali. Niwe nimishajikubali ila naenda kupima kupata uthibitisho tu. Labda pia nipigwe sindano ya usingizi nikizinduka nipo angaza.
Maisha yenyewe presha tupu, halafu nikijitambua marehemu mtarajiwa hapo chacha!!

Teh teh teh......kupima ni muhimu ili ujitambue kuwa upo kundi gani na uishije!
Kuhusu umarehemu mtarajiwa ni kwa yeyote aliyechini ya jua na ndio maana hata asiyekuwa nao anakufa kwa kitu kingine.
Yatupasa kuishi kana kwamba hatutaiona kesho!!!!!!!!!!
 
wdee imekula kwako.....sie twaendea kugegeda na rain coat zetu bwana...mnataka utamu halisia kazi kwenu

Wee Mzabzab usiseme maneno hayo huu ugonjwa hauna mwenyewe,tena tema mate chini...mwîma lakn?mekumic
 
endelea kuwa mwaminifu kwa Mungu na usali sana i blv in miracles, kuwa hiv positive sio mwisho wa maisha angalia maisha yako baada ya kugundua hiyo hali, pray hard, Mungu ni mwaminifu, anaweza kukupa haki yako, nina testimony ya mama mmoja mpk mume wake anakata roho ndipo alipogundua mumewe alikuwa ni hiv positive, ilikuwa ngumu sana kuamini maana alimwamini sana na walipendana sana. aliumia sana na siku zote alimlilia Mungu mana alijua miaka yote 17 ya ndoa yao alikuwa mwaminifu. alienda kupima akaambiwa bado CD4 zake ni nyingi hivyo hakuanza kutumia dawa ilikuwa 2000, akawa anaenda clinic kuchek mara kwa mara, alianza kila baada ya miezi 3, ikabadilishiwa awe anarudi kuchek baada ya miez 6, akabadilishiwa mwaka, na mda wote huo alikuwa committed na Mungu, hivi naongea na wewe 2011 she was tested and found HIV negative.ni swala la kutubu na kumdai Mungu haki yako, if you believe you may receive your miracle. stay blessed kaka nakusihi kusali na kumwomba mungu bila kukata tamaa.
 
  • Thanks
Reactions: PLL
Glivec hii ya kuvaa gloves inanikera kama nini
halafu unakuta wanakuchika kama vile
uchafu fulani hivi, pengine wengi wa wafanyakazi wa idara ya afya siyo wale wa wito ni wanaotafuta tu mkate wa siku na ndiyo maana wanafanya hivyo.

hii ya gloves hata tukienda kuosha nywele salon wanatuvalia ndo wanatuosha.
huwa natamani nisirudi tena hiyo salon kabisa.

lakini yote kwa yote jipe moyo na maisha yataendelea
Mungu hawezi kukuacha hata siku moja,

Je dada mwenyewe yuko wapi saa hii?
na wewe kuna kitu unakijua zaidi ya hao wengine. haya mambo hakuna anayeyajua kuliko mwingine. ndio maana unaona wafanyakazi wa idara ya afya ndo wanyanyapaaji wakubwa kuliko hata jamii inayotuzunguka. pamoja na wao kuruhusiwa kuvaa gloves wanapomhudumia mgonjwa lakini wananyanyapaa sana wagonjwa wa aina hii.
 
Last edited by a moderator:
Hongera sana kwa ujasiri na moyo wa kujali wengine.
Kuishi na VVU sio kuwa na Upungufu wa Kinga Mwilini, hivyo cha msingi zingatia maelekezo yote ya lishe na lifestyle ili Kinga zisipungue.
Usisononeke sana na kuwazia your status, maana itakudhoofisha na ndio maana sijakupa pole maana inaweza kukufanya mnyonge au mwenye mapungufu fulani.
Kuna kaka mmoja alileta uzi wake na nilimpenda the way alivyoikubali hali na kuishi kwa kujali afya yake; kuishi na VVU sio sawa na mgonjwa wa cancer ou diabetes so cheer up and live normal long loving life.
 
Nawafurahia sana watu wa namna hii hasa waliojitambua na wanaojikubali. Nina bibi zangu wawili nao ni HIV positive mmoja aliambukizwa na mumewe na mwengine alikuwa akifanya uchangudoa zamani sana huko Nairobi. Ni wahamasishaji wazuri sana na wamejitolea kuwa mfano kwa wengine kuwa kuugua sio kufa kwa sababu wana miaka zaidi ya 18. Kwahiyo kaka nakupa hongera sana.
 
Pole sana mkuu....umeandika huu uzi kwa hisia kali sana (linaonekana hilo wakati wa kuusoma). Jitahidi kuendelea kuwaokoa na wengine na kuwa strong all the time..Mungu yu pamoja nawe.
 
Pole sana ndugu pia hongera kwa kua na hofu ya Mungu ndani yako maana hyo ndo ikufanyayo ushndwe kuambukiza watu wengine,na Mungu ni mwaminifu hatokuacha endelea kumuamin na kumuomba,usikate tamaa na endelea kufuata ushauri wa dakta,Mungu unaemuomba na kumuamini hatokuacha atakupa mke mwema mtakaeendana nae na utakua na furaha.
 
Heshima kwenu wakuu.

Poleni na majukumu ya kila siku. Hili suala ni gumu kuliko linavyofikirika na jamii na watu ambao hawajapatwa na mikasa migumu. Ndio maana unyanyapaa unaendelea kutawala sana humu nchini na tatizo linazidi kushamiri. Nilikuwa na mchumba ambaye nilimpenda sana na ndiye niliyemuweka kuwa chaguo langu la maisha.

Mwanzoni mwa uhusiano wetu tulikuwa tukifanya mapenzi kwa kutumia condom na baadaye tulikuja kuacha kutumia baada ya kupima several times na kuona tupo vizuri na tulikuwa tumeshakubaliana kuja kuishi pamoja. nilimtambulisha kwa ndugu zangu kama ndiye ndugu yao atakayeongezeka na yeye alinitambulisha kwa baadhi ya ndugu zake.

Miaka ilivyozidi kwenda niliona mabadiliko kwa mwenzangu kitabia kwani kuna wakati alikuwa akinidanganya kwamba amesafiri kumbe yupo na hajaondoka. Kumbe mwenzangu alishaanzisha uhusiano na wazee wa mujini wenye pesa zao hivyo akawa ananipotezea kwani kwa wakati huo ndo nilikuwa namalizia mwaka wangu wa mwisho chuoni.

Hali ilizidi kuwa mbaya zaidi kwani ilifika kipindi akanambia ile mipango tuisitishe. nilipomuuliza kwa nini, hakuwa na jibu la wazi. Ilinichanganya sana lakini nilipata faraja kutoka kwa rafiki zangu na ndugu nikatulia. Baada ya miezi kama sita kupita niliamua kwenda kupima na nikagundulika kwamba niko na maambukizi ya VVU, nilichanganyikiwa sana na niliona kama hakuna haja ya kuishi tena.

Sikumwambia mtu mwingine zaidi ya doctor mmoja na mimi mwenyewe kuugulia maumivu yangu peke yangu ila kuna wakati ndugu na jamaa walikuwa wakiniona nimebadirika ila nawaambia hakuna shida yoyote na nipo kawaida. Nilijitahidi kutokukaa peke yangu kwani mawazo ndo yangenizidia.

Mpaka sasa hivi nipo vizuri na nna afya njema ila napata wakati mgumu sana kwani wasichana wengi wanaonesha dalili za kutaka kuwa na uhusiano na mimi lakini nawaonea huruma sana kwani inaniuma sana nikifikiria kumwambukiza mtu mwingine. Wengi wao nimekuwa nikiwakwepa mpaka wengine wananitangazia kwamba jogoo wangu hawiki, huwa inaniuma sana kwani sitaki wajue na sipendi kuwafanya wawe kama mimi.

Nisiwasumbue sana, naomba nihitimishe kwa kusema; hili tatizo ni gumu sana hasa unapokuwa wewe ndiwe 100%. Tupigeni vita unyanyapaa ili watu wasiwe na mawazo ya kwamba TUFE WENGI. Pia unayemnyanyapaa hujui aliupata vipi kwani si kila mwenye VVU alikuwa kuruka njia. Kuna wengine wameupata kutoka kwa watu wanaowaamini sana! Na wengine miaka ya leo wamezaliwa nao hivyo sio kosa lao kwa hapo walipo.

SAY NO TO STIGMA BUT PROTECT YOURSELF FOR THE BEST OF YOU ALL.


pole sana ndugu, nakushauri ukaribie kwenye kiti cha rehema cha Mungu, ukaungame dhambi zako na kuokoka kisha udai haki yako ya uzima. kwa Mungu hakuna gumu la kumshinda, amini tu tatizo lako litaisha mara moja zaburi 58.3, 51.5, isaya 1.1-9, ufunuo 21.8, mithali 28.13, zaburi 103.3, luka 1.77, Nakupongeza kwa kupima na kwa uamuzi wako wa busara wa kutoambukiza wengine kwani utalipwa na Mungu kwa tendo lako jema.

Kwa wanawake nawashauri mpunguze tamaa za mafanikio ya pupa, mwisho wake huwa ni kuangamiza nafsi zenu na za wengine. hebu jaribu kufikiria huyo binti atakuwa na wazee wangapi wenye fedha maana si atataka aendeke gari ya kisasa na kuishi katika nyumba ya kisasa hivyo mzee mmoja hataweza kugharimia vyote hivyo. je ni familia ngapi ataziua. ni kama kuna mwanamke mmoja alishuhudia humu kuwa amewaambukiza UKIMWI zaidi ya wanaume 1500. Wanawake jitizameni, kumbukeni kwa maumbile yenu yalivyo ninyi ni rahisi sana kuambukizwa ukimwi na kuwaambukiza wengine, ama kweli tamaa mbele mauti nyuma
 
Heshima kwenu wakuu.

Poleni na majukumu ya kila siku. Hili suala ni gumu kuliko linavyofikirika na jamii na watu ambao hawajapatwa na mikasa migumu. Ndio maana unyanyapaa unaendelea kutawala sana humu nchini na tatizo linazidi kushamiri. Nilikuwa na mchumba ambaye nilimpenda sana na ndiye niliyemuweka kuwa chaguo langu la maisha.

Mwanzoni mwa uhusiano wetu tulikuwa tukifanya mapenzi kwa kutumia condom na baadaye tulikuja kuacha kutumia baada ya kupima several times na kuona tupo vizuri na tulikuwa tumeshakubaliana kuja kuishi pamoja. nilimtambulisha kwa ndugu zangu kama ndiye ndugu yao atakayeongezeka na yeye alinitambulisha kwa baadhi ya ndugu zake.

Miaka ilivyozidi kwenda niliona mabadiliko kwa mwenzangu kitabia kwani kuna wakati alikuwa akinidanganya kwamba amesafiri kumbe yupo na hajaondoka. Kumbe mwenzangu alishaanzisha uhusiano na wazee wa mujini wenye pesa zao hivyo akawa ananipotezea kwani kwa wakati huo ndo nilikuwa namalizia mwaka wangu wa mwisho chuoni.

Hali ilizidi kuwa mbaya zaidi kwani ilifika kipindi akanambia ile mipango tuisitishe. nilipomuuliza kwa nini, hakuwa na jibu la wazi. Ilinichanganya sana lakini nilipata faraja kutoka kwa rafiki zangu na ndugu nikatulia. Baada ya miezi kama sita kupita niliamua kwenda kupima na nikagundulika kwamba niko na maambukizi ya VVU, nilichanganyikiwa sana na niliona kama hakuna haja ya kuishi tena.

Sikumwambia mtu mwingine zaidi ya doctor mmoja na mimi mwenyewe kuugulia maumivu yangu peke yangu ila kuna wakati ndugu na jamaa walikuwa wakiniona nimebadirika ila nawaambia hakuna shida yoyote na nipo kawaida. Nilijitahidi kutokukaa peke yangu kwani mawazo ndo yangenizidia.

Mpaka sasa hivi nipo vizuri na nna afya njema ila napata wakati mgumu sana kwani wasichana wengi wanaonesha dalili za kutaka kuwa na uhusiano na mimi lakini nawaonea huruma sana kwani inaniuma sana nikifikiria kumwambukiza mtu mwingine. Wengi wao nimekuwa nikiwakwepa mpaka wengine wananitangazia kwamba jogoo wangu hawiki, huwa inaniuma sana kwani sitaki wajue na sipendi kuwafanya wawe kama mimi.

Nisiwasumbue sana, naomba nihitimishe kwa kusema; hili tatizo ni gumu sana hasa unapokuwa wewe ndiwe 100%. Tupigeni vita unyanyapaa ili watu wasiwe na mawazo ya kwamba TUFE WENGI. Pia unayemnyanyapaa hujui aliupata vipi kwani si kila mwenye VVU alikuwa kuruka njia. Kuna wengine wameupata kutoka kwa watu wanaowaamini sana! Na wengine miaka ya leo wamezaliwa nao hivyo sio kosa lao kwa hapo walipo.

SAY NO TO STIGMA BUT PROTECT YOURSELF FOR THE BEST OF YOU ALL.

Bravo meeen,una moyo wa kiuungwana sana maana mwingine angelipizia,kwa hili Muumba wetu yu pamoja nawe daima,ubarikiwa sana.dooooh
 
Heshima kwenu wakuu. Poleni na majukumu ya kila siku. Hili suala ni gumu kuliko linavyofikirika na jamii na watu ambao hawajapatwa na mikasa migumu. Ndio maana unyanyapaa unaendelea kutawala sana humu nchini na tatizo linazidi kushamiri. Nilikuwa na mchumba ambaye nilimpenda sana na ndiye niliyemuweka kuwa chaguo langu la maisha. Mwanzoni mwa uhusiano wetu tulikuwa tukifanya mapenzi kwa kutumia condom na baadaye tulikuja kuacha kutumia baada ya kupima several times na kuona tupo vizuri na tulikuwa tumeshakubaliana kuja kuishi pamoja. nilimtambulisha kwa ndugu zangu kama ndiye ndugu yao atakayeongezeka na yeye alinitambulisha kwa baadhi ya ndugu zake. Miaka ilivyozidi kwenda niliona mabadiliko kwa mwenzangu kitabia kwani kuna wakati alikuwa akinidanganya kwamba amesafiri kumbe yupo na hajaondoka. Kumbe mwenzangu alishaanzisha uhusiano na wazee wa mujini wenye pesa zao hivyo akawa ananipotezea kwani kwa wakati huo ndo nilikuwa namalizia mwaka wangu wa mwisho chuoni. Hali ilizidi kuwa mbaya zaidi kwani ilifika kipindi akanambia ile mipango tuisitishe. nilipomuuliza kwa nini, hakuwa na jibu la wazi. Ilinichanganya sana lakini nilipata faraja kutoka kwa rafiki zangu na ndugu nikatulia. Baada ya miezi kama sita kupita niliamua kwenda kupima na nikagundulika kwamba niko na maambukizi ya VVU, nilichanganyikiwa sana na niliona kama hakuna haja ya kuishi tena. Sikumwambia mtu mwingine zaidi ya doctor mmoja na mimi mwenyewe kuugulia maumivu yangu peke yangu ila kuna wakati ndugu na jamaa walikuwa wakiniona nimebadirika ila nawaambia hakuna shida yoyote na nipo kawaida. Nilijitahidi kutokukaa peke yangu kwani mawazo ndo yangenizidia. Mpaka sasa hivi nipo vizuri na nna afya njema ila napata wakati mgumu sana kwani wasichana wengi wanaonesha dalili za kutaka kuwa na uhusiano na mimi lakini nawaonea huruma sana kwani inaniuma sana nikifikiria kumwambukiza mtu mwingine. Wengi wao nimekuwa nikiwakwepa mpaka wengine wananitangazia kwamba jogoo wangu hawiki, huwa inaniuma sana kwani sitaki wajue na sipendi kuwafanya wawe kama mimi. Nisiwasumbue sana, naomba nihitimishe kwa kusema; hili tatizo ni gumu sana hasa unapokuwa wewe ndiwe 100%. Tupigeni vita unyanyapaa ili watu wasiwe na mawazo ya kwamba TUFE WENGI. Pia unayemnyanyapaa hujui aliupata vipi kwani si kila mwenye VVU alikuwa kuruka njia. Kuna wengine wameupata kutoka kwa watu wanaowaamini sana! Na wengine miaka ya leo wamezaliwa nao hivyo sio kosa lao kwa hapo walipo. SAY NO TO STIGMA BUT PROTECT YOURSELF FOR THE BEST OF YOU ALL.
pole sana ndugu yangu kweli inasikitisha sana lakini huo sio mwisho wa maisha.duh tumejifunza kitu!!
 
pima ili ujue afya yako uchague namna ya kuishi.

kaka nikupe hongera kwa kupima ila kitu ambacho haujakijua ni kuwa unadahan ukiwa na ngoma utakufa kesho ,si kweli. Pia nakupongeza kwa kuwa na ujasiri ila mim sijawai kupima uwa naishi nikijua kuwa na mimi ni mgonjwa mtarajiwa na kamwe sijaruhusu wala kuruhusu kuwa kuwa mwenye virusi kunazuia chochote ktk maisha yangu. Sitapima na sina mpango wa kupima. Jipe moyo utashinda.
 
Mmmmh..... Umeicopy mahli hii..! Kwa nini usituwekee source basi!!!
 
Mimi kwenda kupima labda niwe naharisha kama ngisi dhofle hali. Niwe nimishajikubali ila naenda kupima kupata uthibitisho tu. Labda pia nipigwe sindano ya usingizi nikizinduka nipo angaza.
Maisha yenyewe presha tupu, halafu nikijitambua marehemu mtarajiwa hapo chacha!!

Hahahha mkuu hili Si Jambo la kucheka ila umefanikiwa kunichekesha sana.
 
Back
Top Bottom