Niliambukizwa HIV na mtu niliyemwamini!

Niliambukizwa HIV na mtu niliyemwamini!

wdee imekula kwako.....sie twaendea kugegeda na rain coat zetu bwana...mnataka utamu halisia kazi kwenu
usifurahi mwenzako anapoanguka, maana kifo tumeumbiwa wote, huwezi jua nawe waweza kujikwaa hata kwa kansa ya koo kwa ajiri ya uvinza au kwa ajali ukavujika kiuno utabaki kuponyeza kizenji tu
 
Pole sana kaka. Maisha ni zaidi ya kuwa VVU. Fanya kazi zako na majukumu yako kama kawaida Mungu aendelee kukutia nguvu.
 
Dah inatia uchungu sana ukijitunza halafu akakuletea. Be strong
 
Pole sana ndugu kwa kweli inasikitisha sana. Ila there is still hope. na maisha yanasonga, usikate tamaa. Hongera kwa kuwa mwaminifu kwa muumba wako na kwa jamii nzima. Hakika Mungu atakulipa hata kama si hapa ni huko tuendako sote..
 
Mimi kwenda kupima labda niwe naharisha kama ngisi dhofle hali. Niwe nimishajikubali ila naenda kupima kupata uthibitisho tu. Labda pia nipigwe sindano ya usingizi nikizinduka nipo angaza.
Maisha yenyewe presha tupu, halafu nikijitambua marehemu mtarajiwa hapo chacha!!


kapime uokoe wengine.

Glivec pole sana ,na hongera kwa moyo wako wa huruma.... unachoweza kufanya ni kumtafuta mwanamke ambaye yupo wazi na anamaambukizi mkubaliane na mfanye mahusiano na hatimaye kama ni ndoa mkikubalia mfunge.
 
Last edited by a moderator:
Nimeisoma post yako mara kadhaa, nashindwa nikwambieje zaidi ya kukupa POLE.
Pia nakupongeza kama hutabadili mawazo SIKU MOJA na kusema "NGOJA TUFE WENGI maana hata mimi nililetewa".
Jitahidi upate vyakula vya kutosha na mwili wako utakuwa vizuri.
POLE SANA.
 
Mmmmh..... Umeicopy mahli hii..! Kwa nini usituwekee source basi!!!

hakuna mahali unaweza kucopy na watu wasijue ndugu yangu. ukiona hakuna anayetoa source basi ujue ni mimi mwenyewe
 
Pole sana ndugu kwa kweli inasikitisha sana. Ila there is still hope. na maisha yanasonga, usikate tamaa. Hongera kwa kuwa mwaminifu kwa muumba wako na kwa jamii nzima. Hakika Mungu atakulipa hata kama si hapa ni huko tuendako sote..

sijakata tamaa na nipo kimaendeleo zaidi. najua kwamba sitakufa leo wala kesho ila kufa kupo.
 
Glivec hii ya kuvaa gloves inanikera kama nini
halafu unakuta wanakuchika kama vile
uchafu fulani hivi, pengine wengi wa wafanyakazi wa idara ya afya siyo wale wa wito ni wanaotafuta tu mkate wa siku na ndiyo maana wanafanya hivyo.

hii ya gloves hata tukienda kuosha nywele salon wanatuvalia ndo wanatuosha.
huwa natamani nisirudi tena hiyo salon kabisa.

lakini yote kwa yote jipe moyo na maisha yataendelea
Mungu hawezi kukuacha hata siku moja,

Je dada mwenyewe yuko wapi saa hii?
inabidi wakati mwingine tukubaliane tu na ukweli dada yangu. tuwalinde na wengine. mi ukinishika na gloves sitamind kwa sababu unajilinda na wewe lakini usinishike kwa kinyaa. kuna hepatitis B na C ambazo ni hatari zaidi ya VVU. Tukikubali hali zetu tutakubali kujilinda na kuwalinda wengine. imagine huyo anayekuosha nywele awe na kidonda mkononi na wewe kichwani, si mtaambukizana? Huyo dada kwa kweli sijui yuko wapi kwa sasa hivi. sikuwa na hamu ya kumtafuta kabisaaaa.
 
It is not a death sentence! Mbona watu mmetiririka kama vile jamaa hana maisha tena.
Tumeona watu wamepona kabisa hio kitu. Kinachowapeleka wengi ni stress na mawazo baada ya kujua. Ukiweza kabiliana na hilo basi!
Dawa ipo tafuta tu.
 
yani mtu unakwenda unapima naye, unamuamini mpo salama, halafu anakuja tena kukuambukiza! haya mapenzi jamani
 
Kaka kama umeanza tumia dawa ni bora zaidi.....kula vizur na acha kuwaza mengi. .ndio maisha kaka....
........kwa wale wasiojua afya zao waende kupima.........
kuna dawa ambazo huzuia maambukiz punde unapokutana na muathirika.....inaitwa PEP....unatumia kwa mwez mmoja.......Combivir+Aluviar....hata kwa wanaobakwa hutumia hiyo
 
Hii ni kwa wale wote wanaoishi na maambukizi ya VVU. Anza kliniki za wagonjwa wa VVU ili ufuatiliwe afya yako kwa ukaribu. Ugonjwa wa UKIMWI sasa si hatarishi, dawa zimeufanya kuwa moja ya magonjwa sugu.
 
Glivec, Kwa Neema ya Mungu Utayashinda yote

Usiumie kwa maneno na matendo ya watu, Tazama na usonge mbele,

Unyanyapaa mbaya sana ni ule wa wewe mwenyewe kushindwa kwenda na hali yako

Mungu akutangulie ktk Yote
 
Last edited by a moderator:
Nami nikwambie pole zaidi ya wengine. ww kweli ni msomi jasiri. ulichokosea ni kufanya mapenzi nje ya ndoa na inawezekana huyo mwenza wko hukumfanyia uchunguzi kwa kina juu ya tabia yake.

Lakini yote hayo tuckulaumu xana kwani kila mtu anaweza kuchelea kma hivyo. bado nafac ya kuwa na mwenza unayo lakina hakikisha mwenza wko awe muathirika ili kuepusha kueneza kwa wengine, pia uishi chini ya ushauri wa afya kwa waathirika.
Ucsahau kurejea kwa muumba.
 
Back
Top Bottom