Niko sawa au ni mawazo yangu ya kishetwain??

Niko sawa au ni mawazo yangu ya kishetwain??

Siku nyingine akikupigia mpe BF wako apokee,kama mbwai mbwai bana,au namna gani vipi pokea alafu lia kama vile mko na jamaa yako sehem sehemu mna DUU, kama atakupigia tena huyo si pastor ni SHETWANI MKUBWA

Kwa urahisi sana, hata kama hajamwambia mama,
Amtishe kwa kumkumbusha kazi yake kama mchungaji, then mwambie Mama/baba ataongea nawe au mkeo kuhusu majukumu ya kanisa na nasi sote,
Atalia na kuanza kusali ili isiwe soo kubwa!
 
Habari yako?
Pole kwa changamoto hiyo iliyokupata kwa huyo mtumishi wa Mungu.
Kwanza, napenda uelewe kuwa hata watumishi wa Mungu katika uanadamu wao wanaweza kuanguka, kwa maana ya kujaribiwa na kutenda uovu kama anavyonia huyo mchg. Sitaki kuzungumzia juu ya uhalisi wa utumishi wake kwa kuwa sifahamu.

Kwakuwa najua unaelewa lengo lake ni lipi, basi huu ni ushauri wangu:
  • Elewa kwamba yeye ni binadamu na anaweza kukuosea kama hivyo, no one is perfect hivyo kuwa tayari kusamehe na kulifuta hilo jambo kwenye priority za mawazo yako. Usipofanya hivyo, utaingia katika mtego wa kutokuwaamini watumishi wote wa Mungu, au ule wa kutokuwaamini wanaume wote.
  • Biblia Takatifu inasema kuwa "Ikimbieni zinaa", kwa msingi huo wa Neno la Mungu, na kwa kuwa unasema wewe ni msomi wa chuo, tumia akili yako kulitii andiko hilo, jiepushe na mazingira yote ambayo wewe unafahamu fika kuwa yanaweza kupelekea wewe kuzini na huyo mtumishi. Tunajua wakati mwingine mtu anaweza kumlaumu mtumishi kuwa kazini naye lakini inafaa kutafakari kuwa mdada mwenyewe alijirahisisha na kushindwa kuzuia jambo hilo ili hali alielewa kabisa kuwa matukio fulanifulani yanaashiria ngono. Jilinde.
  • Kwa namna ya uangalifu, nakushauri uongee na huyo mtumishi. Mueleze wewe umekuwa ukimchukuliaje yeye na familia yake, mshukuru kwa malezi aliyochangia kwako na familia yenu, mweleze kuwa unaelewa hizo sms na calls zake zinaashiria nini, mueleze kuwa jambo analotaka kulifanya ni ovu, kinyume na amri za Mungu, kinyume na hata mahubiri ambayo huwa anahubiri Kanisani (mi simfahamu mtumishi huyo). Mueleze kuwa kwa msingi wa maagizo ya Mungu kamwe hutaridhia kufanya kitendo hicho kwa namna yoyote.
  • Mwambie aache kabisa tabia hiyo kwako na hata kwa wasichana wengine na asirudie kabisa. Muonye kuwa la sivyo utapasua jipu kwa kuwaeleza wanafamilia wote. Muonye vikali. Mwambie kuwa hili siyo ombi bali ni amri kwani ndiyo utaratibu wa maisha yako kwa mujibu wa Neno la Mungu analolihubiri.
  • Muahidi kuwa akitii hilo utaendelea kumheshimu kwa nafasi yake, na siyo vinginevyo.
  • Mwambie kwa kuwa yeye ni mtumishi wa Mungu, unaamini kuwa atamwomba Mungu msamaha kwa ajili ya hilo kama anavyohubiri kwa watu.
  • Kumwelezea msimamo wako huu, pengine ni vyema kumwandikia barua umpe asome (kwa kuzingatia kuwa, pengine ukiwa naye ana kwa ana anaweza asikupe nafasi ya kuyaeleza haya yote, na pia pengine yanaweza yakawa mazingira hatarishi, kwani mtu huyu unapaswa kumkwepa sasa, nimeshasema tumia usomi wako vizuri.)
  • Mtake atamke (kwa namna yoyote) kutokuyarudia hayo.
  • Baada ya kufanya hivyo, act kwa mujibu wa response yake.
  • Hiyo ndio dunia, UWE MAKINI SIKU ZOTE.
  • Kama nilivyosema, huu ni ushauri wangu tuu, tafakari zaidi mwenyewe uone jinsi ya ku-act. Nadhani utaifaa jamii kwa ujumla pia kuhusu yale ambayo tunayona huku mitaani mwetu.
  • **Napenda ieleweke kuwa mimi simfahamu mtumishi huyo (wala sihitaji kumfahamu), kwahiyo nimeongea in a general term.
Kama utadhani (au yeyote) utahitaji ushauri zaidi , email: thekingdomnews@yahoo.com
 
unasema ingekuwa ni mtu wa kawaida ungesha mchana..

Mi naona tena huyo mchungaji ndo wa kumchana mpaka aone rangi zote za rainbow.
yeye ni mtumishi wa Mungu, Ana mke kama ulivyosema , familia yako wanamwamini sana
na we unamwita baba..

Ingepeza zaidi kama ungemfumulia hayo yote ,
Na umwambie aheshimu na kutimiza amri za MUngu kama anavyofundisha waumini wake .

Amen.

Na ukimuona huwezi hata kumdhania ndo mana hata mi nasita nkihisi labda mie ndo namtafsiri vibaya
 
Siku nyingine akikupigia mpe BF wako apokee,kama mbwai mbwai bana,au namna gani vipi pokea alafu lia kama vile mko na jamaa yako sehem sehemu mna DUU, kama atakupigia tena huyo si pastor ni SHETWANI MKUBWA
kwani anaye BF!!!
 
Zama sio rahisi kivile kumchana mtu mzima tena unaemuheshim sana besids haniambii direct ili iwe rahis kumjibu direct bt anafungafunga lkn mtu mzima una uwezo wa kusoma intention ya mtu
basi kama hakuambii live muhimize aisema hiyo nia yake then wewe hapo ndo umchane live!unajua wanaume ni kama mchwa hujaribu kula kitu chochote mbele yao!mchwa hujaribu kula jiwe,ukiendelea kummezea upuuzi wake one day anaweza kufanikisha anacho taka maana ataongeza bidii akisaidiwa na shetani na wewe ukiwa na imani haba mchungaji anabembea!!
 
Na ukimuona huwezi hata kumdhania ndo mana hata mi nasita nkihisi labda mie ndo namtafsiri vibaya

come on now..
Hebu we fikiri Mume gani wa mtu anakupigia simu zaidi ya mara tatu kwa siku
halafu anakwambia mnayoongea ni kati yenu tu . Haileti maana kwa nini mfanye
siri kama maongezi ni ya heri?.... fikiri hilo.
 
kwani anaye BF!!!

Inavoonesha hana,

Chamuhimu ajilinde sana na huyu mtumishi yawezekana ni mbwa mwitu ila ana ngozi ya kondoo,
Lakini ikiwezekana ndo ivo akimpigia amtishe kuwa mama anajua na ataongea naye zaidi, akimwambia ni jambo bayaa wala hakutegemea,
Ikiwezekana ajipange vizuri kumwambia mambo kama yaliyosemwa na Savedlema, Nawe ukimsaidia na kupotoka kwake utabarikiwa, ila akikosea ataingia katika tabu na majuto ya maisha
 
Habari yako?
Pole kwa changamoto hiyo iliyokupata kwa huyo mtumishi wa Mungu.
Kwanza, napenda uelewe kuwa hata watumishi wa Mungu katika uanadamu wao wanaweza kuanguka, kwa maana ya kujaribiwa na kutenda uovu kama anavyonia huyo mchg. Sitaki kuzungumzia juu ya uhalisi wa utumishi wake kwa kuwa sifahamu.

Kwakuwa najua unaelewa lengo lake ni lipi, basi huu ni ushauri wangu:
  • Elewa kwamba yeye ni binadamu na anaweza kukuosea kama hivyo, no one is perfect hivyo kuwa tayari kusamehe na kulifuta hilo jambo kwenye priority za mawazo yako. Usipofanya hivyo, utaingia katika mtego wa kutokuwaamini watumishi wote wa Mungu, au ule wa kutokuwaamini wanaume wote.
  • Biblia Takatifu inasema kuwa "Ikimbieni zinaa", kwa msingi huo wa Neno la Mungu, na kwa kuwa unasema wewe ni msomi wa chuo, tumia akili yako kulitii andiko hilo, jiepushe na mazingira yote ambayo wewe unafahamu fika kuwa yanaweza kupelekea wewe kuzini na huyo mtumishi. Tunajua wakati mwingine mtu anaweza kumlaumu mtumishi kuwa kazini naye lakini inafaa kutafakari kuwa mdada mwenyewe alijirahisisha na kushindwa kuzuia jambo hilo ili hali alielewa kabisa kuwa matukio fulanifulani yanaashiria ngono. Jilinde.
  • Kwa namna ya uangalifu, nakushauri uongee na huyo mtumishi. Mueleze wewe umekuwa ukimchukuliaje yeye na familia yake, mshukuru kwa malezi aliyochangia kwako na familia yenu, mweleze kuwa unaelewa hizo sms na calls zake zinaashiria nini, mueleze kuwa jambo analotaka kulifanya ni ovu, kinyume na amri za Mungu, kinyume na hata mahubiri ambayo huwa anahubiri Kanisani (mi simfahamu mtumishi huyo). Mueleze kuwa kwa msingi wa maagizo ya Mungu kamwe hutaridhia kufanya kitendo hicho kwa namna yoyote.
  • Mwambie aache kabisa tabia hiyo kwako na hata kwa wasichana wengine na asirudie kabisa. Muonye kuwa la sivyo utapasua jipu kwa kuwaeleza wanafamilia wote. Muonye vikali. Mwambie kuwa hili siyo ombi bali ni amri kwani ndiyo utaratibu wa maisha yako kwa mujibu wa Neno la Mungu analolihubiri.
  • Muahidi kuwa akitii hilo utaendelea kumheshimu kwa nafasi yake, na siyo vinginevyo.
  • Mwambie kwa kuwa yeye ni mtumishi wa Mungu, unaamini kuwa atamwomba Mungu msamaha kwa ajili ya hilo kama anavyohubiri kwa watu.
  • Kumwelezea msimamo wako huu, pengine ni vyema kumwandikia barua umpe asome (kwa kuzingatia kuwa, pengine ukiwa naye ana kwa ana anaweza asikupe nafasi ya kuyaeleza haya yote, na pia pengine yanaweza yakawa mazingira hatarishi, kwani mtu huyu unapaswa kumkwepa sasa, nimeshasema tumia usomi wako vizuri.)
  • Mtake atamke (kwa namna yoyote) kutokuyarudia hayo.
  • Baada ya kufanya hivyo, act kwa mujibu wa response yake.
  • Hiyo ndio dunia, UWE MAKINI SIKU ZOTE.
  • Kama nilivyosema, huu ni ushauri wangu tuu, tafakari zaidi mwenyewe uone jinsi ya ku-act. Nadhani utaifaa jamii kwa ujumla pia kuhusu yale ambayo tunayona huku mitaani mwetu.
  • **Napenda ieleweke kuwa mimi simfahamu mtumishi huyo (wala sihitaji kumfahamu), kwahiyo nimeongea in a general term.
Kama utadhani (au yeyote) utahitaji ushauri zaidi , email: thekingdomnews@yahoo.com

Asnt sana savedlema its such a wisdom way...ingawa plan yangu ni kutoreply msg zake ever hata hiyo ya asnt baba nastop...pili simu napokea moja tuu natoa salam na nkiona mazungumzo yanaenda way too far namwambia nna kazi nakata,mimi sitakaa nipige labda kwa mkewe coz sijui kama anayajua haya and no more vochaa ili asione namuentertain na zawadi
 
Na yeye ana moyo wa nyama si wa chuma hivyo ana hisia ingawa ni mchungaji.
Kama unamkatalia just mkatalie just like unavyowakatalia wnaume wengine ambao hawakuvutii na kama unamkubalia just mkubalie tuu.
 
Huu ni mtego mbaya. Sababu kubwa ni kuwa unamheshimu kama kiongozi wako wa kiroho. Kumbuka akigundua kuwa mchezo huu utamuathiri, anaweza kugeuza kibao wewe ukaonekana ndo mkosaji.(mtoto huyu hana adabu/amekuwa mhuni nk) Huyu ni mchungaji na watu waumini wake watamuamini zaidi yako na wewe kuonekana mwenye tabia mbaya. anaweza kusema alikuwa nataka kukupa malezi kwa ukaribu wewe ukatafsiri mapenzi! hapa atakuwa anataka kujikwamua na kudhalilika, na hatajari amekuumbua kiasi gani, ili mradi abaki na uchungaji wake.
Ushauri wangu;
Nenda kwenye simu yako, block namba yake kabisa. Hatakuwa na uwwezo wa kukupigia akiuliza mwambie simu yako mbovu. Kwa kuwa ameisha kukwaza kiimani, sali kanisa jingine ili asipate nafasi ya kukuona na wewe uwe huru kusali kwa amani. Kwa njia hii utamfuta kwenye mawazo yako na yeye atagundua makosa yake. Kila la kheri.
 
Huu ni mtego mbaya. Sababu kubwa ni kuwa unamheshimu kama kiongozi wako wa kiroho. Kumbuka akigundua kuwa mchezo huu utamuathiri, anaweza kugeuza kibao wewe ukaonekana ndo mkosaji.(mtoto huyu hana adabu/amekuwa mhuni nk) Huyu ni mchungaji na watu waumini wake watamuamini zaidi yako na wewe kuonekana mwenye tabia mbaya. anaweza kusema alikuwa nataka kukupa malezi kwa ukaribu wewe ukatafsiri mapenzi! hapa atakuwa anataka kujikwamua na kudhalilika, na hatajari amekuumbua kiasi gani, ili mradi abaki na uchungaji wake.
Ushauri wangu;
Nenda kwenye simu yako, block namba yake kabisa. Hatakuwa na uwwezo wa kukupigia akiuliza mwambie simu yako mbovu. Kwa kuwa ameisha kukwaza kiimani, sali kanisa jingine ili asipate nafasi ya kukuona na wewe uwe huru kusali kwa amani. Kwa njia hii utamfuta kwenye mawazo yako na yeye atagundua makosa yake. Kila la kheri.

Yan wewe umenielewa vilivyo,,,watu wana akiliii nisipojipanga aibu itanirudia mimi na kwa protocal yake mie ndo naeza kuonekana shetani namseduce pastor
 
Ni sawa, ila kumbuka wanaume siye wajanja bwana!
Zingatia maonyo ya watu wengine hapa.
 
Mchane live,mwambie haupendezwa na tabia yake ya kuku call mara kwa mara.mwambie wewe uwezi kuwa mfariji wake.mfariji wake ni yesu na mungu wake.kama vp unaweza ku mblack list.
 
Toria pole sana

Jambo la muhimu tambua kwanza huyo Mchungaji ni binadamu (kuwa kwake mchungaji hakuondoi mapungufu yake ya kibinadamu)

Pili, tambua kwamba watumishi wa Mungu au watu wanaomwamini Mungu huwa wanakutana na majaribu ya kila aina yakiwepo ya namna hii.

Play ya part, kama umemaliza chuo naamin una upeo kiasi fulani. Mwambie akuheshimu wewe kama binti yake, na asikuletee hizo habari kabisa. Mtishe kuwa akiendelea utamshtaki kwa wazazi wako na hizo sms zitakuwa ndio uthibitisho. All the best. .


Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums
 
Last edited by a moderator:
HONGERA SANA MDADA KWA KUMSHTUKIA HUYO MCHUNGAJI MWOVU,WALA ASIKUPOFUSHE NA HUO UCHUNGAJI WAKE FEKI NA WALA HUJAMHISI VIBAYA WALA NINI KWANI UNATAKIWA KUFAHAMU MCHUNGAJI PIA NI MTU KAMA WENGINE NA HIVYO UWEZEKANO WA KUKOSEA KWAKE UPO TENA MKUBWA TU,UAMUZI ULIOUCHUKUA SAA HIVI ENDELEA NAO HIVYOHVYO NI KUMCHUNIA KWA KWENDA MBELE ASITAKE KUTUMIA CHEO CHAKE KUKUHARIBU NA KUFICHA MDHAMBI ZAKE,BIG UP MDADA UNAFAA.:cheer2:BRAVOOOOOOOOOOO.
 
Kama anatabia hiyo na yeye ni kiongozi wa dini, hii ni Hatari kabisa, La muhimu usimjibu vibaya, usipokee simu yake tenaaaaa na wala usijubu sms zake pindi atakapokuwa anakuandikia, atafahamu kuwa umechukia kutokana na maneno yake pamoja na sms, alizokuwa anakuandikia. ila kikutana naye pritent kama hakuna kitu, msalimu, na mchangamkie kama kawaida, akikuuliza kwa nn hupokei simu yake wala hujibu sms zake mwambie zijaziona. yeye mwenyewe ataelewa ni nn unamwambia. Usiwaambie wazazi maana unaweza leta mtafaruku katika jamii. wewe umeshakuwa unatakiwa kusolve matatizo kama hayo mwenyewe. Na ndipo atashika adabu yake na atakuheshimu mwanzo mwisho.

MUUNGWANA NI VITENDO, UKIPIGA KELELE WATU WATAKUDHARAU

Zingatia haya ya Lisa utakuwa salama
 
Huu ni mtego mbaya. Sababu kubwa ni kuwa unamheshimu kama kiongozi wako wa kiroho. Kumbuka akigundua kuwa mchezo huu utamuathiri, anaweza kugeuza kibao wewe ukaonekana ndo mkosaji.(mtoto huyu hana adabu/amekuwa mhuni nk) Huyu ni mchungaji na watu waumini wake watamuamini zaidi yako na wewe kuonekana mwenye tabia mbaya. anaweza kusema alikuwa nataka kukupa malezi kwa ukaribu wewe ukatafsiri mapenzi! hapa atakuwa anataka kujikwamua na kudhalilika, na hatajari amekuumbua kiasi gani, ili mradi abaki na uchungaji wake.
Ushauri wangu;
Nenda kwenye simu yako, block namba yake kabisa. Hatakuwa na uwwezo wa kukupigia akiuliza mwambie simu yako mbovu. Kwa kuwa ameisha kukwaza kiimani, sali kanisa jingine ili asipate nafasi ya kukuona na wewe uwe huru kusali kwa amani. Kwa njia hii utamfuta kwenye mawazo yako na yeye atagundua makosa yake. Kila la kheri.

Well speak sambu
 
Toria pole sana

Jambo la muhimu tambua kwanza huyo Mchungaji ni binadamu (kuwa kwake mchungaji hakuondoi mapungufu yake ya kibinadamu)

Pili, tambua kwamba watumishi wa Mungu au watu wanaomwamini Mungu huwa wanakutana na majaribu ya kila aina yakiwepo ya namna hii.

Play ya part, kama umemaliza chuo naamin una upeo kiasi fulani. Mwambie akuheshimu wewe kama binti yake, na asikuletee hizo habari kabisa. Mtishe kuwa akiendelea utamshtaki kwa wazazi wako na hizo sms zitakuwa ndio uthibitisho. All the best. .


Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums
Asnt kwa ushauri
 
Last edited by a moderator:
HONGERA SANA MDADA KWA KUMSHTUKIA HUYO MCHUNGAJI MWOVU,WALA ASIKUPOFUSHE NA HUO UCHUNGAJI WAKE FEKI NA WALA HUJAMHISI VIBAYA WALA NINI KWANI UNATAKIWA KUFAHAMU MCHUNGAJI PIA NI MTU KAMA WENGINE NA HIVYO UWEZEKANO WA KUKOSEA KWAKE UPO TENA MKUBWA TU,UAMUZI ULIOUCHUKUA SAA HIVI ENDELEA NAO HIVYOHVYO NI KUMCHUNIA KWA KWENDA MBELE ASITAKE KUTUMIA CHEO CHAKE KUKUHARIBU NA KUFICHA MDHAMBI ZAKE,BIG UP MDADA UNAFAA.:cheer2:BRAVOOOOOOOOOOO.

Asnt blue g
 
Back
Top Bottom