Karibu sana katika Uislam. Uislam ndio Dini yako ya asili. Unaposilimu unakuwa unarudi katika asili. Uislam ndio Dini ya maumbile yako. Rudi katika maumbile yako halisi. Moyo wako hauna utulivu deep down kwa sababu haupo katika maumbile yako halisi. Ulizaliwa katika Fitrah (maumbile ya asili) ya Uislam, ila wazazi/walezi wakakubadilisha. Tumeumbwa sisi kumuabudu Allah Peke Yake bila ya kumshirikisha na chochote kile (kuwa Waislam).
Mitume (Amani iwe yao) walikuja kuwaongoza watu na kuwarekebisha pale ambapo Fitrah yao ilipochafuliwa, Mitume wakaletwa kuwasafisha na kuwaongoza watu kurudi katika Fitrah yao, warudi kumuabudu Allah Peke Yake bila ya kumshirikisha na chochote.
Yule Aliyeumba kila kitu na ni Muweza juu ya kila kitu Ndiye Anayestahiki Kuabudiwa na Anaabudiwa vile anavyotaka Yeye kwa sababu Yeye Ndio Mjuzi juu ya kila kitu. Ndio maana kaleta Mitume ili wawalinganie watu wao warudi katika Fitrah (maumbile ya asili) yao ya kumuabudu Allah Peke Yake bila ya kumshirikisha na chochote kile na Allah Akawafunulia Mitume hao namna ya kumuabudu Yeye wakawafundisha jamaa zao.
Mitume wote walikuja kuwalingania na kuwaongoza watu wao kurudi katika maumbile ya asili na lengo la kuumbwa kwao wamuabudu Allah Peke Yake bila ya kumshirikisha na chochote.
Kila watu walipopotoka katika maumbile yao halisi na wakaacha mafundisho ya Mitume, Allah Alileta Mtume mwengine mpaka alipokuja Muhammad (Swala na Salamu ziwe juu yake).
Mitume wote ikiwemo Nuh, Ibrahim, Musa, 'Iysa/Yesu na Mtume wa Mwisho Muhammad ambaye alitumwa kwa watu wote kwa zama zote mpaka Qiyama na akawa ni Mtume wa Mwisho na hakuna Mtume wala Nabii baada yake (Swala na Salamu ziwe juu yake na juu ya Mitume wote) walikuja kuwarudisha watu katika lengo la kuumbwa kwao.
Mtume Muhammad (Swala na Salamu ziwe juu yake) ndio Mtume wa mwisho na ndio alikuja na Sheria ya mwisho kutoka kwa Allah, na Sheria hiyo itabaki mpaka Qiyama, na wafuasi wa manabii waliopita wanawajibiwa kumfuata Mtume wa Mwisho pamoja na Sheria aliyokuja nayo kutoka kwa Mola wake.
Hivyo mkuu
nodetz Uislam ndio Haqq na ndio njia ya sawa na ndio ndio Dini ya Manabii na Mitume wote wa Allah (Amani iwe juu yao Manabii na Mitume wote) na ndio Dini yako ya asili.
ayat 64 from Surah Al Imran
﴿قُلْ يَا أَهْلَ الْكِتَابِ تَعَالَوْا إِلَىٰ كَلِمَةٍ سَوَاءٍ بَيْنَنَا وَبَيْنَكُمْ أَلَّا نَعْبُدَ إِلَّا اللَّهَ وَلَا نُشْرِكَ بِهِ شَيْئًا وَلَا يَتَّخِذَ بَعْضُنَا بَعْضًا أَرْبَابًا مِّن دُونِ اللَّهِ ۚ فَإِن تَوَلَّوْا فَقُولُوا اشْهَدُوا بِأَنَّا مُسْلِمُونَ﴾
[ آل عمران: 64]
Sema: Enyi Watu wa Kitabu! Njooni kwenye neno lilio sawa baina yetu na nyinyi: Ya kwamba tusimuabudu yeyote ila Mwenyezi Mungu, wala tusimshirikishe na chochote; wala tusifanyane sisi kwa sisi kuwa Waola Walezi badala ya Mwenyezi Mungu. Na wakigeuka basi semeni: Shuhudieni ya kwamba sisi ni Waislamu.