Mi nna swali kuhusu uislam
.
Ni nani aliyeipanga Quran, Yani aya hii ianze ile ifate? Na alitumia/walitumia formula ipi au vigezo Gani?
Asante
Swali lako halipo sawa kitaalamu ila nimekuelewa
Kwanza tambua kuwa Kuna Quran na msahafu
Quran
Ni Aya na sura zilizokuwa zinamfikia mtume Moja Kwa Moja kupitia ufunuo
Kwa mfano siku mtume anahama kutoka Maka kuende Madina kulikuwa na maadui wanamsuburi nje akitoka wamshambulia Ili asifanikiwe kufika Madina
Mtume akaambiwa asome surat Yasini kama Kinga yake na akaisoma kuanzia Aya ya kwanza Hadi ya mwisho
Na Kuna siku mtume alimwambia swahaba wake amsomee surat nisaa Yale swahaba akaisoma alipofika Aya Fulani akamwambia basi ishia hapo
Na pia wakati Mtume anaongoza Sara alikuwa anasoma sura tofauti tofauti
So wakati Mtume yupo Quran ilikuwa Ina sura zake na Aya zake
MSAHAFU
Baada ya mtume kufa Abukali ndio alikuwa kiongozi wa waislam akaona ni vyema tukusanye sura zote tuziandike sehemu Moja ndio ukapatikana msahafu
Hizo sura kabla ya msahafu zilikuwa zimeandikwa katika ngozi za wanyama na zingine katika mawe
KUPANGWA KWA MSAHAFU
Ndani ya msahafu Kuna
1) sura ya kwanza Hadi ya mwisho
2) Juzu ya kwanza Hadi ya 30
Haya yamepangwa na wanazuoni Ili kurahisisha kwa watu kujifunza kuisoma Quran na kuhifadhi na ndio maana Ile juzu ya mwisho imewekwa sura nyinyingi fupi fupi Ili watoto wajifunze Kwa urahisi
Sio sawa mtoto mdogo aanze kufundishwa surat bakara Ina Aya zaidi ya 200 na 80 badala yake Kuna sura fupi fupi Zina 7 au 5 ,au 10 ndio anaanza nazo hizo
Na hili la kupangwa sura na juzuu katika uislam halina ulazima wowote kulifuata
Umewekewa sura fupi fupi uanze nazo ukisema Mimi nataka nijifunze Quran kuanzia surat bakara Haina shida wewe tu na uamuzi wako unaweza ukaanzia popote kujifunza au kuisoma