Niko Dilemma

Niko Dilemma

Wapendwa
Sio mara nyingi nimekuwa nikipost hapa...nimekuwa msomaji mzuri tu wa mabandiko mbalimbali na nimejifunza mengi kupitia post na michango yenu.

Kiukweli niko njia panda ndugu zangu,Niko na historia ya kuumizwa na mzazi mwenzangu mpk ilifika mahala nikamuacha na kuendelea na maisha yangu..

Nilitamani sana kama ningelikuwa na uwezo nibaki single siku zote nisiwe na mahusiano but kama unavyojua tena ujana maji ya moto..Of coz nikisema nitaishi bila dyudyu milele najidanganya...
Niliona kuliko kuangaika ni heri kuwa na mtu mmoja ninayemuamini na kupima ambaye ataendelea kunipoza mpk pale nitakapo amua kuingia katika serious relationship...

Mwanzoni kabisa wakati tunaanza mahusiano nilimwambia msimamo wangu akaniambia ...Mungu ndie mpangaji tuendelee tu nitakufundisha kunipenda..nikaona isiwe tabu tukaendelea na mahusiano yetu ni mwaka sasa.

Kiukweli mwaka umepita...mwanaume ananipenda na kunijali japo hayuko kamili..but sio shida sababu hakuna aliyemkamilifu...shida ni kwamba bado hajaujaza moyo wangu...najitahidi sana kujifunza kumpenda lkn nahisi kuwa naidanganya nafsi yangu ili hali yeye kila siku anazidi kudata na penzi langu na anazidi kunipenda.Imefika mahala mpk na mimi nimeamua kupretend kuwa nampenda ili asiumie.

Mwishoni mwa mwaka jana aliniomba nimpeleke kwa wazazi wangu na kwamba ananipenda sana so anataka kila kitu kiwe formal...nikamjibu kuwa nahitaji muda zaidi kujiridhisha na hayo maamuzi lakini niliona ni mapema sana coz nilishaumizwa na sikutaka kukurupuka tena katika maamuzi

Kiukweli sitoficha sijui ni bahati nzuri au mbaya ila nimekuwa nikitongozwa sana na wanaume katika kipindi hicho kigumu na najua wengi walitaka kutake advantage na situation niliyokuwa nayo but maamuzi ya kuwa kwenye mahusiano yanilisaidia kuendelea kuwa na misimamo yangu....

Lakn kama mnavyojua mapenzi wakati mwingine ni upofu...nimetokea kumpenda mkaka mmoja ambaye ni rafiki yangu tu wa kawaida...na kiukweli alishanitongozaga nikwambia nina mahusiano na kwa vile ni mtu mwenye kuheshimu hisia zangu aliomba tuendelee kuwa marafiki tu kama ilivyozamani..But kila kukicha naona moyo wangu unamwelekea na and I never felt like this before....Kiukweli nimejikuta nashindwa kucontrol hisia zangu kwa huyo mkaka.

Sasa nikija katika vigezo vya husband material kiukweli da first guy anavyo sababu ana Hofu ya Mungu.. ni matured...kashafanya starehe mpk kaamua kuacha...Sio mlevi..Anajali....sio tajiri ila anapambana na maisha kufikia ndoto na malengo yake na amekuwa akinishirikisha kila jambo na pia ameonesha nia dhahiri na kutaka kufunga ndoa na mimi.

About second Guy kiukweli bado anaujana,anakunywa pombe kiasi,kwa tabia siwezi comment sana sababu bado sikumpa nafasi kama mpz ni rafiki yangu tu...so sijapata nafasi kumsoma kiundani zaidi.
Sasa Dilemma inayokuja ni kuwa niolewe na anayenipenda na kunifeel sana nikajifunze kumpenda nikiwa kwenye ndoa au au nisubiri kwanza mpk nijiridhishe na maamuzi yangu coz sitaki kamwe kuchepuka...na me sina haraka sana kusubiri wakati utakaompendeza Mungu but mwenzangu kwa kweli kwa age yake na malengo yake amekuwa akitamani sana tufunge ndoa mwaka huu

Sasa wandugu pamoja ya kuwa niko kwenye maombi nikiendelea kumwomba Mungu anioneshe mwelekeo wa maisha yangu..Natamani mnishauri kama ni sahihi kuendelea mbele na maamuzi ya kuolewa na huyo mkaka au nisubiri..najua ndoa ni kitu chema lkn sitaki kuja kumuumiza mume wangu mtarajiwa kwa kuwa na mahusiano nje ya ndoa na kwa state niliyopo now mpk naanza kufall kwa mwingine inatosha kuonesha danger zone kuwa inawezekana ikatokea kama nikiwa kwenye ndoa

Naomba nieleweke wazi kuwa sina nia ya kuwa na huyo mkaka wa pili na msimamo wangu ni kwamba aendelee kuwa rafiki au ndugu kama walivyo wengine na ameaccept ila kupitia yeye nimeona bado kuna gap katika moyo wangu juu ya huyu niliyenae na hofu yangu ni kuwa sitotaka hilo lije kujirudia katika maisha yangu ya ndoa sababu sitopenda kuisaliti ndoa yangu huko mbele.

Naombeni mnishauri..
Mbarikiwe sana
Jitahidi kumwangalia Hugo ambae moyo wako umefall ili kujiridhisha zaidi pole sana dadaangu
 
Hizi feelings sa nyingine zinadanganya......nakumbuka nami nilikuwa kwenye dilema....nikajidai A nampenda kuliko B .....nikampotezea B .... Baadse nae A akanipotezea....matokeo yake nikapoteza kote....

Bora anayekupenda kuliko huyo unayesema moyo ndo umemdondokea..... Moyo saa nyingine unadanganya.......
 
Hizi feelings sa nyingine zinadanganya......nakumbuka nami nilikuwa kwenye dilema....nikajidai A nampenda kuliko B .....nikampotezea B .... Baadse nae A akanipotezea....matokeo yake nikapoteza kote....

Bora anayekupenda kuliko huyo unayesema moyo ndo umemdondokea..... Moyo saa nyingine unadanganya.......
Ninyi mitetea acheni tabia yenu ya kukimbiza majogoo jamani, acheni majogoo yawakimbize!.... Itakula kwenu, believe me!
 
wewe, mpe mashine apige huyo unae mtamani, dhen ndoa funga na huyu wa kwanza, ila nikushauri kitu muhimu husimuumize mtu maana dhambi ya kumuumiza itakuchoma mbinguni
 
Mmmh! Ndoa ni pana na inachangamoto zake nyingi tu bidada! Mapenzi ni hisia kama umeshindwa kumpenda huyo the first hadi umekuja humu kutaka ushauri naamini hata ufunge ndoa naye hutokaa umpende katu!kwani atakuwa kabadilika nini labda?! Usijidanganye eti utajifunza kumpenda! Wee! Kama unataka kufunga ndoa ili umridhishe huyo jamaa na jamii yako uishi maisha ya kupretend katika maisha yako yote OLEWA!(Hapa ndipo wanawake wengi hukosea)kama unataka kuishi ukiwa na amani moyoni SUBIRI.sikushauri uwe na hako kajamaa kengine !kuna mdada alishakujaga hapa kujuta jinsi gani anavyoteseka moyoni kuolewa na mtu asiyempenda.nilimuelewa alichomaanisha.Subiri!
 
...otherwise maisha ni yako fanya vile akili yako inataka.
 
Rusha roho taratibu hiyo shoga
Angalia usijekuwa story
Usijekuwa mfano
Usijekuwa tukio bidada
Penda unapopendwa utulizane....
You are right my friend rubii hata katika Biblia yenu imeandikwa kuwa mwanamke hupendwa na mwanaume hupenda. Ni hatari mwanamke kupenda. Katika maisha hasa ya ndoa lazima mwanamme apende na mwanamke apendwe. Ukiona mwanamke anapenda jua hiyo ndoa ipo mashakani. Mwenye masikio na asikie
 
U
Hizi feelings sa nyingine zinadanganya......nakumbuka nami nilikuwa kwenye dilema....nikajidai A nampenda kuliko B .....nikampotezea B .... Baadse nae A akanipotezea....matokeo yake nikapoteza kote....

Bora anayekupenda kuliko huyo unayesema moyo ndo umemdondokea..... Moyo saa nyingine unadanganya.......
Up sahihi bora kupendwa kuliko kupenda.
Ni rahisi kuumizwa
 
dear sio rahic kuishi na mtu unayempenda. Nilipita katika wakati kama wako, lkn ckufanya kosa nilimchagua anayenipenda sasa ni mwaka wa 9 ndoa yangu inaamani na furaha, nimejifunza kumpenda mume wangu na sasa nampenda sana. life is not a rehearsal.
Ahsante kwa kunitia moyo dear
 
Yes its possible ..(But its up to her ) .. Some women are very easy to fall in love to the men that are really in love with them .. I am talking this through experience , I have seen before ... Kinachotakiwa ni Honest toward the guy that he loves her .. But we are still different people .. As I said it is up to her.. For her situation asijichanganye aombe sana Mungu na kufunga .. Halafu aache kuwasiliana na huyo so called friends will bring confusion to her mind and soul.. Na kwa sababu the first guy seems patient amuaambie wafunge na kuomba pamoja kwanza kabla ya kufanya chochote ili wasikie Mungu atasema nini juu yao (wakate mawasiliano kwa muda ili kuutafuta uso wa Mungu ) .... Thanks..
ahsante sana mkuu...I will do that
 
Kwa ukweli unaojionyesha kuna mapungufu kwa yule ulienae, kulingana na uzoefu wa mahusiano yako ya awali. Unatafuta the best ya yule ulieachana nae, past experience inakutesa hata ukijiambia hutaki kukumbuka. Olewa na mtu anaekupenda mfundishe na msaidie kuondoa mapungufu aliyonayo
Ahsante Mkuu
 
Unajitafutia tu kuja kujuta baadaye. Unashindwa nini ku stick na mwanaume anayekupenda na kukujali? Huyo brazameni wako atakugharimu.
 
Back
Top Bottom