Nikiri wazi: Namfahamu shetani

Nikiri wazi: Namfahamu shetani

Mshana Jr

Platinum Member
Joined
Aug 19, 2012
Posts
371,517
Reaction score
860,565
1472991879467.jpg


Kwa wale wachangiaji wa kukurupuka watofautishe kati ya kujua na kufahamu
Nakiri wazi kabisa kuwa namjua shetani...huyu kiumbe mbaya kabisa mwenye kutisha na kuogofya hasa.

Kwa mara ya kwanza nilimfahamu shetani kupitia maandiko na simulizi kwenye imani yangu...nikasoma na kusimuliwa vizuri tu kuhusu hiki kiumbe na jinsi lilivyokaa kimvuto (japo kinatisha sana kwa baadhi ya picha)nikamfahamu shetani kwa njia hiyo
Kilichofuatia ni kumjua shetani...nimekuwa mshirika wake kwa miaka mingi tumefanya naye kazi pamoja, tuneshirikiana kwenye mengi na nimegundua ni mtu wa aina gani...shetani ni shetani tuu hata awe na sura nzuri ya kuvutia kama malaika hata akupe kila kitu..sio mwema kwako na daima anania maovu.

Hii ni siku ya mapumziko na ya ibada kwa wengine lakini wengi muda huu wako kazini wakishiriana kufanya kazi na shetani..cha kushangaza ukiwaukiza wanaweza kukana kabisa kumjua wala kumfahamu shetani na huu ndio uhalisia wetu UNAFIQUE

1472992577614.jpg


1472993069494.jpg
1472993078464.jpg
 
Duh ama kweli unamjua maana post zako zinazohusu imani unapenda sana kuzungumzia hayo ya shetan!
Funguka zaidi mkuu kuwa ilikwaje time unashirikiana nae?
 
Tatizo shetani nae bwana anamautamu yake hv amaizing ili apate company ya kwenda nayo kuleee.... sasa kwasababu ya ugumu wa mioyo ndo hivyo tena tuko mguu nje mguu ndani kujikana nafsi na kuwachukia baba, mana, watoto, ndugu, n.k sio kazi rahusi mzee
 
kiranga haamini uwepo wa huyu kiumbe,

uliwahi kumwona shetani? kujua kitu lazima uwe umekiona ila unafahamu kitu kwa kusimuliwa
 
Back
Top Bottom