Niite jina lolote ila ndivyo nilivyo

Niite jina lolote ila ndivyo nilivyo

The Evil Genius

JF-Expert Member
Joined
Mar 21, 2014
Posts
6,151
Reaction score
20,076
Niite msaliti,mwizi,sio mzalendo au vyovyote ila haya yafuatayo siyafanyi.

1. Silipi kodi.
Sitalipa na huwa silipi kodi ya moja kwa moja au wanaita direct tax. Huo ni utaratibu wangu,silipi na huwa nafanya kadri niwezavyo kuikwepa,nikiuza au kununua sidai lisit,hata nikibanwa sana bora nikubaliane na afsa kodi tuigawane ila isiende serikalini.

2. Siwataji na sitawataja wala rushwa na wakwepa kodi
Hata kama ntamjua mtu anaehujumu uchumi sitamtaja kwa wahusika na wala sina mpango huo isipokua tu waovu kama majambazi.

3. Mimi sio mzalendo.
Kuwa mzalendo maana yake ni kua uwaheshimu viongozi walioko madarakani(profesa shivji). Hivyo basi mimi sio mzalendo na wala sina huo mpango.

4. Sipigi kura na wala sina huo mpango.
Sina mpango wa kuja kupiga kura nchi hii hadi pale ntakapokua nimejiridhisha mwenyewe.

5. Kuwasaidia watu wanaotaka kukwepa kulipa kodi.
Kwa kua nimefanya kazi na watu wa mapato kwa muda,ukijumlisha na kua mimi ni mtu wa mahesabu najua wapi kuna udhaifu wa kukusaidia kutolipa au kukwepa kodi,ntamsaidia watu kadri niwezavyo wakwepe kulipa kodi.

Hayo matano tu. Unaweza kuniitaje?au unaweza kusema nikoje?

Sababu nimegundua ni sawa na kugawa hela kwa mafisadi wa nchi hii. Jadili
 
  • Thanks
Reactions: SIM
jina zuri linalokufaa Mwanakombo
 
Acha kujidanganya wewe kenge maji. Kw kifupi kodi unalipa kila siku. Mf mahitaji yako ya kila siku yote unalipa kodi nukta.
 
Nakuunga mkono asilimia mia tano!
Kwa nchi yenye viongozi wezi kama Tanzania kuna sababu gani za kulipa kodi au kuwa mzalendo? Nchi ambayo inasamehe kodi wageni na kuwasukumia mzigo wote wazawa kwa kisingizio cha uwekezaji!!
Na mimi silipi kodi na nitaiba kila nipatapo fursa! nawasihi na ninyi wananchi mnaosubiri maisha bora toka serikalini mtoke kwenye mawazo hayo,

Serikali haina mpango wowote wa kurahisisha maisha ya Mtanzania zaidi ya tuliowapa madaraka kujijali wao na familia zao na kuzidi kututisha tu kila uchao.
Nakusihi kulipa kodi kwa sasa hasa hapa Tz ni ufala, na nakusihi usiilazie macho kila fursa mbele yako eti kwa kujifanya mzalendo, kibongo utakuwa unatafuta kufa maskini tu!!

Pana kulipa kodi na iba kila nafasi nzuri ijitokezapo.
 
Mie nataka kuacha ajira kabisa ili niweke kodi ya kichwa. Nifanye biashara niweke kodi kuliko wahindi. Hii habari kuwa wafanyakazi wote paye waliyokatwa ni sawa ni excemption zilizotolewa imenikata stimu haswaa
 
hii post yenyewe ulipoi-post tu umeshalipa kodi kubwa tu kama hujui... nami pia ninapo-post hii nalipa kodi kubwa tu.
 
Kumbe uko kama mimi.Nikienda kununua bidhaa kwa mfanyabiashara mwenye EFD.Tunakubaliana kushusha thaman ya bidhaa
 
Mie nataka kuacha ajira kabisa ili niweke kodi ya kichwa. Nifanye biashara niweke kodi kuliko wahindi. Hii habari kuwa wafanyakazi wote paye waliyokatwa ni sawa ni excemption zilizotolewa imenikata stimu haswaa

Unafanya kazi kwa kutoil sana alafu unakatwa kodi wajinga wanaila kiulaini,unalipa mafao serikali inachukua yote ukistaafu unakosa cha kukupiga jeki. Angalia mifuko ya kijamii imefilisika wastaafu wanalia njaa. Sifanyi huo ujinga.
 
Back
Top Bottom