Niipi nafasi ya Dua na maombezi katika uponyaji wa maradhi ?

SONDR

JF-Expert Member
Apr 18, 2019
271
643
Wanajamvi kuna hili swala la watu wenye changamoto mbalimbali za kiafya namaanisha waogonjwa kupelekwa kusomewa Dua au kwenye maombi ili kutatua changamoto zao za kiafya.

Swali ninalojiuliza moja kama kweli Dua na Maombezi vinaponya Maradhi kwanini wasoma Dua na waombeaji hawendi kwenye vituo vya kutolea huduma za afya kama Dhahanati na mahospitalini kuponya wagonjwa?

Pili Kama Dua na maombezi haviponyi maradhi nilini Serikali itaingilia kati kwa kutengeneza sheria za kukataza wagonjwa kupelekwa kwenye Dua na Maombezi ili kupunguza matokeo hasi ya ugonjwa kama ulemavu wa kudumu na vifo.

Tatu kama Dua na Maombezi vinatibu na kuponya maradhi nilini wizara ya afya itaajiri wasoma Dua na waombeaji kwenye ngazi zote za kutelea huduma za afya.
 
Back
Top Bottom