Kingmairo
JF-Expert Member
- Apr 7, 2012
- 4,936
- 3,548
Utanashati ni muunganiko wa vitu vingi hivyo ni gharama kidogo. Kwanza anza na matunzo ya nywele zako! kila mtu ana kichwa ambacho kinaonekana vizuri au vibaya kulingana na aina fulani ya kunyoa. Tafuta hair dressing tyle inayokufanya utokee presentable (watu wengi kipara hakiwatoi smart). Pili, tafuta mavazi yanavyoendana na structure ya mwili wako (epuka nguo zinazopwaya sana au kubana sana). Mpangilio wa rangi za nguo kulingana na rangi yako unahusika pia, kama wewe mweusi uwe unapenda kuchanga nguo zenye bright colours or strips. Angalia pia aina za strips (vertical or horizontal or diagonal) hasa kwenye nguo ya juu. watu wengi wasio na umbo la unene, vertical strips zinawatoa poa na kuwaonyesha warefu. Pamba zako sio lazima ziwe za bei ghali ila material ya nguo inahusika kwenye ubora wa nguo, mfano t-shirt ya pure cotton sio sawa na ya polyster 75%, hivyo ule uzito wake unaifanya ikae vizuri mwilini. Epuka nguo zinazoonekana kwa macho kuwa zimeanza kuchoka (kuchakaa). Usiache ndevu ziwe msitu
