Nifanyeje ili na mimi nionekane mtanashati?

Nifanyeje ili na mimi nionekane mtanashati?

Mkuu suti NA joto hili...

Nilikuwa sijajua mazingira uliyopo mkuu kwa kua nimeona hapo unapendelea T-shirt na jeans au shirt na jeans na kwa kua unalalamika hazikupendezi basi anza kuvaa suruali za vitambaa, kadeti pamoja na hizo shirt

Ila muhimu vaa nguo unayopenda wewe siyo ambayo ulimuona fulani ameivaa uta-feel more comfortable mkuu
 
Lazima uchunguze ujue nguo zipi zinakupendeza.
Suruali aina gani
Mashati aina gani
Rangi ipi

Na kama mwili wako unakubali, maana wengine miili yao hata uiveshe vipi haipendezi
 
Lazima uchunguze ujue nguo zipi zinakupendeza.
Suruali aina gani
Mashati aina gani
Rangi ipi

Na kama mwili wako unakubali, maana wengine miili yao hata uiveshe vipi haipendezi

asante sana ....napenda sana kuvaa jeans ....sana..
 
Utanashati gharama!
Isije kuwa unashindia kinyelamumo za mtumba a.k.a "mama ntakunyaje"

Kama Kila nguo unayotupia haupendezi,jaribu kutembea uchi kiongozi!!

Kama weupe ungekuwa dili,ubuyu usingepakwa rangi.
 
Utanashati gharama!
Isije kuwa unashindia kinyelamumo za mtumba a.k.a "mama ntakunyaje"

Kama Kila nguo unayotupia haupendezi,jaribu kutembea uchi kiongozi!!

Kama weupe ungekuwa dili,ubuyu usingepakwa rangi.

asante mkuu...
 
mimi napita tu maana mimi ni pure sina cha mtana shati wala mtana blauzi
 
Kuna mwana saikolojia mmoja amewahi kuniambia kuwa hata nguo huondoa Stress sasa naamini hilo.
Kaka hata mie ni black lakini nashukuru mungu huwa nikichagua nguo najua zipi zanipendeza. Nilihangaika sana kutafuta fashion but niligundua jeans, mashati ya mikono mifupi na mipasuo kidogo pembeni, viatu vya kuchomeka ambavyo huvalia hata suruali za kitambaa, t shirt form six za dukani.
Nahizo zote ziwe model na sio fashion nyingine. Hakika utapendeza.
Mie toka nigundue hata siku moja sijawahi kuambiwa hujui kuchagua nguo.
Na mke wangu ndo kwanza anapenda mpaka basi.
Fanya hivyo
 
Utanashati gharama!
Isije kuwa unashindia kinyelamumo za mtumba a.k.a "mama ntakunyaje"

Kama Kila nguo unayotupia haupendezi,jaribu kutembea uchi kiongozi!!

Kama weupe ungekuwa dili,ubuyu usingepakwa rangi.



kuna mdau kachangia vyema.mtoa mada hana wasiwasi na rangi wala uzuri anataka utanashati wengi hamja elewa.


kwanza ndugu vaa size yako kama ni suruali au shati.vaa suruali zisizo na mapana ya kizamani.
mtu mweusi anapendeza na nguo za cream. blue isiyo kolea na nyeupe.angalia aina za viatu ziendame na nguo mfno.mchongoko na surual ya kitambaa.flat mbele jeans na kadet.usivae draft chini na juu.usivae shat na suruali zinazofanana rangi.uwiiiiiii mdogo wangu mengine next time.
 
hongera kwa kutamani kuwa samrt, hao, wanaokubeza ndio uchafu wa akili zao, kikubwa badili muonekano, anza kuvaa suruali za kitambaa model zile, na mashati mikono mirefu au mifupi, pia nguo nunua popote ili mradi nzuri ndugu, si mpaka uone duka limeandikwa classic. mimi uwa navaa nguo za tandika bei buku jero, nikilipeleka kwa fundi nikabana shati, namfunika mpk wa classic shop, kingine jikubali aisee, ukiwa smart raha sana, mimi bado kidogo mzeee 1 anipe mtoto wake church awe mke.
 
Utanashati huwa hautafutwi bali huwa unakuja automatically,wala ckushauri ufanye nn ili uwe mtanashati.Hujawahi kumuona mtu ni super handsome but akivaa huwa yupo normal tu.Usiumize kichwa we jikubali tu jins ulivyo
Habari wakuu,
mimi ni kijana mwenye miaka 25..ni mweusi sana...na mrefu wa wastani....na sio mnene
..ningependa wakuu mnipe hints za kuvaa..ili na mimi nionekane smart...kama vijana wenzangu.
Najitahidi kununua nguo
lakini hazinipendezi.
 
Tafuta hela dogo humuoni Wasira au Pinda ni watanashati si mchezo chezea pesa wewe.Ukivaa sana mwisho utapaka caloright.Pesa a.k.a shekeli ndio habari.
 
hongera kwa kutamani kuwa samrt, hao, wanaokubeza ndio uchafu wa akili zao, kikubwa badili muonekano, anza kuvaa suruali za kitambaa model zile, na mashati mikono mirefu au mifupi, pia nguo nunua popote ili mradi nzuri ndugu, si mpaka uone duka limeandikwa classic. mimi uwa navaa nguo za tandika bei buku jero, nikilipeleka kwa fundi nikabana shati, namfunika mpk wa classic shop, kingine jikubali aisee, ukiwa smart raha sana, mimi bado kidogo mzeee 1 anipe mtoto wake church awe mke.

Duh! Umaridadi huficha umaskini pia. Nimependa hapo ulipotaka kupewa mke
 
Back
Top Bottom