Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,777
- 41,066
Nimeona tulizungumzie hili leo na kama kawaida nimelizungumza kwa kina.
Hivi umewahi kujiuliza inakuwaje watu wasomi waliobobea, na watu ambao walikuwa viongozi wazuri sana wakiwa ngazi za chini lakini mara baada ya kuingia katika Chama au kupata nafasi za juu wamegeuka kuwa butu? Hivi umewahi kujiuliza inakuwaje mtu mwenye mawazo tofauti katika CCM anaonekana "si mmoja wao"? Watu kama kina Jumbe, Seif, Njelu, Horace, Salim, Mrema, nk imekuwaje wajikute wako nje ya "mfumo"?
Jibu ni rahisi. Ni lile dudu lililoshika hatamu ya chama, liitwalo "Nidhamu ya Chama". Ni tatizo kubwa kwani viongozi wetu wana utii mkubwa kwa CCM kuliko Nchi yao na wako tayari kutetea na kulinda Katiba na Ilani ya CCM kuliko kutetea na kulinda Katiba na Sheria za Jamhuri ya Muungano! Ni utii wenye kuogofya kwani wabunge, madiwani, na viongozi wengine ambao hawafurahishwi na mambo fulani ndani ya CCM hawawezi kusema chochote kwa kuogopa hilo jinamizi la Nidhamu ya Chama! Kila kitu ndani ya CCM lazima kiende kwenye vikao, na nje ya vikao uko kwenye matata! Pia hili dudu "nidhamu ya chama" halisamehi! Kama Ngawaiya, Masumbuko n.k walidhani wakirudi CCM watafurahiwa sana, wamejidanganya!!!!
Wabunge wa CCM hawawezi kupiga kelele kuikoromea serikali. Na zaidi hawa wabunge wa kuteuliwa ambao hata chamba hawawezi kuikosoa serikali bila kujikuta wakiung'ata mkono unaowalisha! Bila ya shaka wanaweza kuguna na kukohoa kidogo Bungeni (kuonyesha kuwa wapo) lakini hawawezi kamwe kupinga kwa dhati sera zisizo na manufaa, au kuhoji kwa kina mipango mibovu ya serikali wasije wakaonekana wapindani "ndani ya CCM". Imefikia wakati sasa wabunge wa CCM wenye hoja nzuri wanazungumza na wabunge wa upinzani pembeni ili wabunge wa upinzani ndo wazungumzie hoja hizo!! Hebu fuatilia hili suala la Mikataba ya Madini na hiyo mingine utaelewa ninachosema ni nini. Wako wapi kina C. Mzindakaya? Leo wananyamazishwa kiufundi na kina Juma Akukweti!
Huu utii kwa chama, ni utii hatari, unaovuruga utendaji kazi, na unaowatia watu hofu (Mhe. Spika samahani kwa kutumia neno "kutia"). Ni utii ambao unakigeuza chama kuwa kama kikundi cha Kimafia (La Cosa Nostra) ambapo wale wote walioko ndani hawana budi kujipanga mstari, kufuata kifimbo cha kwaya master! Ni utii unaotaka wacheza ngoma kucheza pale tu CCM ikipiga ngoma kwani wachezaji hawatakiwi hata kupiga filimbi zao isipokuwa zile wanazopewa na Chama! Ni ngoma ya kitumwa! na ya kusukumwa!
Huu ni udhaifu mkubwa wa CCM na hiki ndicho kitakachowaangusha CCM. Wanaweza kutawala kwa miaka 70 au hata mia moja lakini kama wakiendelea hivi, wataanguka "anguko kuu" kama vyama vingine ambavyo vilijidhania kuwa "vimetumwa toka mbinguni". CCM lazima ibadilike, lazime iwape uhuru wanachama wake kupingana kwa hoja na wakubwa bila kutengwa au kunyanyaswa! Ni lazima wanachama ambao hawakubaliani na sera fulani wawe huru kuzipinga bila kufukuzwa au kuitishwa kwenye vikao vya "nidhamu ya chama!" Wakati umefika wabunge waweze kuleta miswada yao ambayo ni tofauti na ile ya serikali ili ijadiliwe Bungeni, miswada mizuri ishinde na CCM iendelee kuwa imara!!
Hata hivyo, ni lazima nikiri kuwa hii nidhamu ya chama ndiyo imekifanya CCM kuwa chama kikongwe, kilichobobea, na chenye umoja (au angalau kuwa na hisia za umoja) kuliko chama kingine chochote nchini. Lakini, niseme pia kuwa umoja huu ni wa kusadikika na si wa kuaminika. Sote tunajua kuna makundi ndani ya CCM, kuna wana Mtandao, kuna watu wa BWM, kuna watu wa JSM n.k. Licha ya jitihada za viongozi mbalimbali kuitisha kuvunjwa kwa makundi hayo, makundi hayo bado yanaendelea! Hata hivyo sitashangaa baadhi ya viongozi mashuhuru wakijikuta wanafukuzwa au kuondolewa katika uongozi pale rungu la Nidhamu ya Chama litakapowapitia.
Kwa yeyote mpenda demokrasia, na anayekipenda chama cha mapinduzi na mtu yule ambaye anaipenda Tanzania, basi CCM ni lazima ibadilike na iende na wakati ili watu wasiogope kuwa viongozi ndani yake kwani kila siku watakuwa wanajiangalia mgongoni kuona kama kuna mtu anawafuata au la! CCM lazima ijifunze kulifunga kamba hili jinamizi na ikibidi iliue kwani maisha ya chama chenyewe yako hatarini. Kwani hili jinamizi likimaliza kule walioko nje, litageukia ndani, na njaa yake haitulizwi! Vinginevyo, tumeanza kuona kuinuka na kuanguka kwa Chama cha Mapinduzi!!
Kigumu chama cha Mapinduzi ! Kigumu ! lakini Kidumu? Kidumu - kikiwa na mabadiliko
Hivi umewahi kujiuliza inakuwaje watu wasomi waliobobea, na watu ambao walikuwa viongozi wazuri sana wakiwa ngazi za chini lakini mara baada ya kuingia katika Chama au kupata nafasi za juu wamegeuka kuwa butu? Hivi umewahi kujiuliza inakuwaje mtu mwenye mawazo tofauti katika CCM anaonekana "si mmoja wao"? Watu kama kina Jumbe, Seif, Njelu, Horace, Salim, Mrema, nk imekuwaje wajikute wako nje ya "mfumo"?
Jibu ni rahisi. Ni lile dudu lililoshika hatamu ya chama, liitwalo "Nidhamu ya Chama". Ni tatizo kubwa kwani viongozi wetu wana utii mkubwa kwa CCM kuliko Nchi yao na wako tayari kutetea na kulinda Katiba na Ilani ya CCM kuliko kutetea na kulinda Katiba na Sheria za Jamhuri ya Muungano! Ni utii wenye kuogofya kwani wabunge, madiwani, na viongozi wengine ambao hawafurahishwi na mambo fulani ndani ya CCM hawawezi kusema chochote kwa kuogopa hilo jinamizi la Nidhamu ya Chama! Kila kitu ndani ya CCM lazima kiende kwenye vikao, na nje ya vikao uko kwenye matata! Pia hili dudu "nidhamu ya chama" halisamehi! Kama Ngawaiya, Masumbuko n.k walidhani wakirudi CCM watafurahiwa sana, wamejidanganya!!!!
Wabunge wa CCM hawawezi kupiga kelele kuikoromea serikali. Na zaidi hawa wabunge wa kuteuliwa ambao hata chamba hawawezi kuikosoa serikali bila kujikuta wakiung'ata mkono unaowalisha! Bila ya shaka wanaweza kuguna na kukohoa kidogo Bungeni (kuonyesha kuwa wapo) lakini hawawezi kamwe kupinga kwa dhati sera zisizo na manufaa, au kuhoji kwa kina mipango mibovu ya serikali wasije wakaonekana wapindani "ndani ya CCM". Imefikia wakati sasa wabunge wa CCM wenye hoja nzuri wanazungumza na wabunge wa upinzani pembeni ili wabunge wa upinzani ndo wazungumzie hoja hizo!! Hebu fuatilia hili suala la Mikataba ya Madini na hiyo mingine utaelewa ninachosema ni nini. Wako wapi kina C. Mzindakaya? Leo wananyamazishwa kiufundi na kina Juma Akukweti!
Huu utii kwa chama, ni utii hatari, unaovuruga utendaji kazi, na unaowatia watu hofu (Mhe. Spika samahani kwa kutumia neno "kutia"). Ni utii ambao unakigeuza chama kuwa kama kikundi cha Kimafia (La Cosa Nostra) ambapo wale wote walioko ndani hawana budi kujipanga mstari, kufuata kifimbo cha kwaya master! Ni utii unaotaka wacheza ngoma kucheza pale tu CCM ikipiga ngoma kwani wachezaji hawatakiwi hata kupiga filimbi zao isipokuwa zile wanazopewa na Chama! Ni ngoma ya kitumwa! na ya kusukumwa!
Huu ni udhaifu mkubwa wa CCM na hiki ndicho kitakachowaangusha CCM. Wanaweza kutawala kwa miaka 70 au hata mia moja lakini kama wakiendelea hivi, wataanguka "anguko kuu" kama vyama vingine ambavyo vilijidhania kuwa "vimetumwa toka mbinguni". CCM lazima ibadilike, lazime iwape uhuru wanachama wake kupingana kwa hoja na wakubwa bila kutengwa au kunyanyaswa! Ni lazima wanachama ambao hawakubaliani na sera fulani wawe huru kuzipinga bila kufukuzwa au kuitishwa kwenye vikao vya "nidhamu ya chama!" Wakati umefika wabunge waweze kuleta miswada yao ambayo ni tofauti na ile ya serikali ili ijadiliwe Bungeni, miswada mizuri ishinde na CCM iendelee kuwa imara!!
Hata hivyo, ni lazima nikiri kuwa hii nidhamu ya chama ndiyo imekifanya CCM kuwa chama kikongwe, kilichobobea, na chenye umoja (au angalau kuwa na hisia za umoja) kuliko chama kingine chochote nchini. Lakini, niseme pia kuwa umoja huu ni wa kusadikika na si wa kuaminika. Sote tunajua kuna makundi ndani ya CCM, kuna wana Mtandao, kuna watu wa BWM, kuna watu wa JSM n.k. Licha ya jitihada za viongozi mbalimbali kuitisha kuvunjwa kwa makundi hayo, makundi hayo bado yanaendelea! Hata hivyo sitashangaa baadhi ya viongozi mashuhuru wakijikuta wanafukuzwa au kuondolewa katika uongozi pale rungu la Nidhamu ya Chama litakapowapitia.
Kwa yeyote mpenda demokrasia, na anayekipenda chama cha mapinduzi na mtu yule ambaye anaipenda Tanzania, basi CCM ni lazima ibadilike na iende na wakati ili watu wasiogope kuwa viongozi ndani yake kwani kila siku watakuwa wanajiangalia mgongoni kuona kama kuna mtu anawafuata au la! CCM lazima ijifunze kulifunga kamba hili jinamizi na ikibidi iliue kwani maisha ya chama chenyewe yako hatarini. Kwani hili jinamizi likimaliza kule walioko nje, litageukia ndani, na njaa yake haitulizwi! Vinginevyo, tumeanza kuona kuinuka na kuanguka kwa Chama cha Mapinduzi!!
Kigumu chama cha Mapinduzi ! Kigumu ! lakini Kidumu? Kidumu - kikiwa na mabadiliko