Nia ya kuwapiga Houth ilikuwepo kitambo. Ziara ya mwisho ya Blinken mashariki ya kati ilikuwa ni kuyakokota mataifa 4 vitani. Yote yalimkatalia

Webabu

JF-Expert Member
Apr 29, 2010
7,183
10,921
Kibri cha Marekani na Uiengereza kuyaona mataifa mengine duniani hasa mashariki ya kati yanakaliwa na watu wajinga kinazidi kupata vikwazo katika awamu hizi.

Juhudi za kuwashawishi viongozi wa mataifa hayo ya mashariki ya kati kuwapokea wapalestina wa Gaza zilikwama mapema sana.Juhudi hizo ziliambatana na hongo kwa Misri lakini wote kwa pamoja
wakagoma.Mataifa hayo yakaamua wawaachie Israel wenyewe wapambane na Hmas mpaka kieleweke.

Wanamgambo wa Houth nao wamekuwa mwiba kwa mataifa hayo kutokana na wanamgambo hao kuvuruga safari za meli zinazoelekea Israel kupitia mlango wa Suez.

Msimamo wa Houth na vitendo vyao vimeonesha kuwa na athari sana katika kuangusha uchumi na mtindo wa maisha wa waisrael.Jambo hilo limewatia hasira washirika wakubwa wa Israel ambao ni Marekani na Uiengereza.

Hata pamoja na hasira na nia za kuisaidia Israel iliyobanwa na Hamas na Hizbollah lakini bado mataifa hayo daima hayapendi kuingia vitani peke yao.Hupendelea sana kukokota mataifa mengine ili yawe pamoja nao,
Viongozi mbali mbali wa Marekani wamekuwa wakifanya ziara zisizosita mashariki ya kati ili kutafuta uungwaji mkono wa mikakati yake ya kivita na kuipa muda Israel kupiga wapalestina.

Ziara ya mwisho ya Blinken ilianza na Uturuki halafu akaelekea Qattar,Saudi Arabia, UAE na Misri.

Katika mazungumzo yake ilikuwa ni kuwashawishi wajiunge na muungano wa kuilinda bahari ya Red Sea Ili kuwazuia Houth wasizipige meli za Israel.Ombi hilo kama yale ya mwanzo ya kuwahamisha wapalestina nalo lilikataliwa na viongozi wa mataifa hayo.

Kwa vile nia ya kuipiga Houth ilikuwepo zamani,hata baada ya kukataliwa ushirikiano Marekani ikashirikiana na Uiengereza kupiga maeneo kadhaa ya Yemen.Siku moja baada ya mashambulio ya mwanzo Marekani ikazidi kujikashifu nia zake mbaya kwa kufanya mashambulia mara ya pili peke yake bila kuishirikisha Uiengereza.
 
Kibri cha Marekani na Uiengereza kuyaona mataifa mengine duniani hasa mashariki ya kati yanakaliwa na watu wajinga kinazidi kupata vikwazo katika awamu hizi.
Juhudi za kuwashawishi viongozi wa mataifa hayo ya mashariki ya kati kuwapokea wapalestina wa Gaza zilikwama mapema sana.Juhudi hizo ziliambatana na hongo kwa Misri lakini wote kwa pamoja wakagoma.Mataifa hayo yakaamua wawaachie Israel wenyewe wapambane na Hmas mpaka kieleweke.
Wanamgambo wa Houth nao wamekuwa mwiba kwa mataifa hayo kutokana na wanamgambo hao kuvuruga safari za meli zinazoelekea Israel kupitia mlango wa Suez.
Msimamo wa Houth na vitendo vyao vimeonesha kuwa na athari sana katika kuangusha uchumi na mtindo wa maisha wa waisrael.Jambo hilo limewatia hasira washirika wakubwa wa Israel ambao ni Marekani na Uiengereza..
Hata pamoja na hasira na nia za kuisaidia Israel iliyobanwa na Hamas na Hizbollah lakini bado mataifa hayo daima hayapendi kuingia vitani peke yao.Hupendelea sana kukokota mataifa mengine ili yawe pamoja nao,
Viongozi mbali mbali wa Marekani wamekuwa wakifanya ziara zisizosita mashariki ya kati ili kutafuta uungwaji mkono wa mikakati yake ya kivita na kuipa muda Israel kupiga wapalestina.
Ziara ya mwisho ya Blinken ilianza na Uturuki halafu akaelekea Qattar,Saudi Arabia,UAE na Misri.
Katika mazungumzo yake ilikuwa ni kuwashawishi wajiunge na muungano wa kuilinda bahari ya Red Sea Ili kuwazuia Houth wasizipige meli za Israel.Ombi hilo kama yale ya mwanzo ya kuwahamisha wapalestina nalo lilikataliwa na viongozi wa mataifa hayo.
Kwa vile nia ya kuipiga Houth ilikuwepo zamani,hata baada ya kukataliwa ushirikiano Marekani ikashirikiana na Uiengereza kupiga maeneo kadhaa ya Yemen.Siku moja baada ya mashambulio ya mwanzo Marekani ikazidi kujikashifu nia zake mbaya kwa kufanya mashambulia mara ya pili peke yake bila kuishirikisha Uiengereza.
Mtasema yote marekani kasema hicho kipigo kwa wahouthi ni hatua ya mwanzo tu
 
Mtasema yote marekani kasema hicho kipigo kwa wahouthi ni hatua ya mwanzo tu
Hana lolote.Tumemzoea huyo
keshasema mengi huko nyuma na mwishowe hutoa kauli za kuaibika.
Nini alisema Vietnam,na nini alisema Afghanistan na Iraq.
Pale wahouth walipo mapigo ya angani wala hayawatazuia kitu.
Kama angeweza angeteremka chini na hawezi kabisa.Mwisho ni aibu tu.
 
Kibri cha Marekani na Uiengereza kuyaona mataifa mengine duniani hasa mashariki ya kati yanakaliwa na watu wajinga kinazidi kupata vikwazo katika awamu hizi.
Juhudi za kuwashawishi viongozi wa mataifa hayo ya mashariki ya kati kuwapokea wapalestina wa Gaza zilikwama mapema sana.Juhudi hizo ziliambatana na hongo kwa Misri lakini wote kwa pamoja wakagoma.Mataifa hayo yakaamua wawaachie Israel wenyewe wapambane na Hmas mpaka kieleweke.
Wanamgambo wa Houth nao wamekuwa mwiba kwa mataifa hayo kutokana na wanamgambo hao kuvuruga safari za meli zinazoelekea Israel kupitia mlango wa Suez.
Msimamo wa Houth na vitendo vyao vimeonesha kuwa na athari sana katika kuangusha uchumi na mtindo wa maisha wa waisrael.Jambo hilo limewatia hasira washirika wakubwa wa Israel ambao ni Marekani na Uiengereza..
Hata pamoja na hasira na nia za kuisaidia Israel iliyobanwa na Hamas na Hizbollah lakini bado mataifa hayo daima hayapendi kuingia vitani peke yao.Hupendelea sana kukokota mataifa mengine ili yawe pamoja nao,
Viongozi mbali mbali wa Marekani wamekuwa wakifanya ziara zisizosita mashariki ya kati ili kutafuta uungwaji mkono wa mikakati yake ya kivita na kuipa muda Israel kupiga wapalestina.
Ziara ya mwisho ya Blinken ilianza na Uturuki halafu akaelekea Qattar,Saudi Arabia,UAE na Misri.
Katika mazungumzo yake ilikuwa ni kuwashawishi wajiunge na muungano wa kuilinda bahari ya Red Sea Ili kuwazuia Houth wasizipige meli za Israel.Ombi hilo kama yale ya mwanzo ya kuwahamisha wapalestina nalo lilikataliwa na viongozi wa mataifa hayo.
Kwa vile nia ya kuipiga Houth ilikuwepo zamani,hata baada ya kukataliwa ushirikiano Marekani ikashirikiana na Uiengereza kupiga maeneo kadhaa ya Yemen.Siku moja baada ya mashambulio ya mwanzo Marekani ikazidi kujikashifu nia zake mbaya kwa kufanya mashambulia mara ya pili peke yake bila kuishirikisha Uiengereza.
Ujinga wa hao wajinga(HOUTH) wakiachiwa madhara yake ni kwa dunia nzima, lazima wachapwe tu, ni dunia nzima inamuangalia mbabe wetu US!! kwani hata kipindi kile wale mahalamia wa somalia walipoanza ujinga wa kuteka meli, bila US, ingekuwaje?!
 
Nilipoangalia kwenye kioo nimekuona wewe .Kwa hivyo bwege ni wewe. babukijana.
Na kabla ya kuangalia kwenye kioo nilipata picha kwa kuangalia jina lako.
Sawa tuendelee kubishana mabwege wawili
 
Ujinga wa hao wajinga(HOUTH) wakiachiwa madhara yake ni kwa dunia nzima, lazima wachapwe tu, ni dunia nzima inamuangalia mbabe wetu US!! kwani hata kipindi kile wale mahalamia wa somalia walipoanza ujinga wa kuteka meli, bila US, ingekuwaje?!
Americant kuichapa houthi hawezi kama anaweza apeleke jeshi ground tuone atakavyo wachapa houthi

Hakuna hata mtumbwi kuelekea israhell yaaani
 
Kusema ukweli toka moyoni mimi Israel ilinikwanza sana iliporuhusu ushenzi na kuuhalalisha ila katika hili nawa muwazi zaidi.
Houth watapigika vibaya na hakuna rangi wataacha kuona ni muda sasa namuelewa muarabu alivyo fitna na mjinga.
Wakati Israel inahalalisha ushoga sio ajabu hata hukuwa umezaliwa au kufikiriwa kuzaliwa.
 
Back
Top Bottom