kindikinyer leborosier
JF-Expert Member
- Jan 6, 2018
- 492
- 929
Hili jambo linanitafakarisha sana wanajamii!!
Habari!?
Mimi ni kijana wa makamo, natoka familia ya kawaida, baba alikua mtumishi na mama ni mama wa nyumbani tu!
Nina changamoto Moja hivi, naomba kushea mnipe mawazo walau nijue naanzia wapi.
Nina miaka 34 Sasa naelekea 35, Sina familia swala ambalo nilikua na sisitizwa sana na baba (si baba mzazi, mama aliolewa nikiwa nimezaliwa), baba huyu ananipenda sana, hivyo mara kadhaa huniomba ushauri na msaada na mara nyingi namsaidia, ikiwa ni pamoja na kuwasomesha wadogo zangu.
Mwaka Juzi niliachana na mchumba Ambae nilidhani tungeoana, ni mambo ya vijana Kila mtu ana sababu zake. (Ameshaolewa na Wana maisha Yao)
Ilibdi niwaze kumpata mtu Ambae ninafahamiana nae, anatoka maeneo ya nyumbani.
Kuna binti mmoja ni mtoto wa rafiki yake na baba, walikua marafiki sana, huyo binti niliwahi kumtongoza kipindi Cha nyuma, wakati tunasoma aligoma, nikamwacha. Baba yake alifariki na wakati anafariki baba ni kama alikua mwangalizi wa familia hii.
Katika pita zangu juzi nikiwa single nimeachana na aliekuwa mchumba, nikakutana nae, ameachwa na waliekuwa nae na kibaya zaidi ana mtoto mmoja.
Nilimweka karibu kwanza kumchunguza, nilivutiwa nae kwa vingi, mapambano yake na historia mbaya sana aliokuwa akinipa kuhusu baba wa mwanae.
Tulienda muda kidogo tukaanza mahusiano, nikiwa makini sana, aaah huyu dada nilijikuta nampenda sana kama mwanzo, very organized, focused, nk nk, yaan package full, japo Kila nikisoma story za usioe single mother naishiwa pawa.
Anyway juzi hapa nikaona nimwoe, baada ya nyumbani pia kusema ni muda Sasa wa kuwa na mchumba, (baba alikua anajua tyari nilimwambia na alifurahi niwe na mtoto wa rafiki yake)
Nilijipanga nikaenda nyumbani kusema official, walifurahi na binti kwao walifurahi sana maana walikua wakitufahamu Toka tukiwa wadogo.
Shida Sasa ikaanza baada ya Mimi kurudi, nikapigiwa simu na dada mkubwa (ameachana na mume wake) ninaemfuata, akaniambia 'wewe kwanini unataka kupush sana mambo Yako wakati unaona nyumbani sahivi Kuna tukio la ukoo, Babu anataka kufanya jubilei' nilishangaa maana Mimi sikua na hizo taarifa, na kwa maelezo ya baba, mwezi wa 10 mwaka huu nilikua niwe na ndoa.
Nikamwambia asirudie kuniambia hivyo maana mm sijalazimisha chochote! Na nilikua sijui lolote,
Kilichofuata baba aliniambia ataenda kwa wakwe kuanza michakato, nikawa napigwa kalenda sana, mwisho akaniambia tatizo ni pesa nikamtumia, lkn Bado nikawa napigwa kalenda.
Hatimaye siku Moja mama akanipigia simu usiku, akaniambia, wewe...... Huoni Kuna Nini hapa nyumbani, tukio la Babu, na tunataka tutengeneze makaburi ya ukoo, nikamwambia mama mbona hivyo vitu havina gharama na vinaweza kwenda pamoja, akapata kigugumizi akaanza kunipa sababu zingine mwisho nikaanza kuonekana mkosaji Tena.. nikanyamaza.
Week kadhaa siku Moja baba akanipigia simu mchana akaniambia, usiwe unaongea nao sana hao, subiri mwakani hata mwezi wa kumi huko tutafanikisha...
Nilishangaa sana maana mwanzo nilikua nahamasishwa sana lkn sahv yamekuwa hayo...
Nipeni mawazo watu wangu wa maana, nianzie wapi? Nisije jikuta nachelewa zaidi na zaidi!
Habari!?
Mimi ni kijana wa makamo, natoka familia ya kawaida, baba alikua mtumishi na mama ni mama wa nyumbani tu!
Nina changamoto Moja hivi, naomba kushea mnipe mawazo walau nijue naanzia wapi.
Nina miaka 34 Sasa naelekea 35, Sina familia swala ambalo nilikua na sisitizwa sana na baba (si baba mzazi, mama aliolewa nikiwa nimezaliwa), baba huyu ananipenda sana, hivyo mara kadhaa huniomba ushauri na msaada na mara nyingi namsaidia, ikiwa ni pamoja na kuwasomesha wadogo zangu.
Mwaka Juzi niliachana na mchumba Ambae nilidhani tungeoana, ni mambo ya vijana Kila mtu ana sababu zake. (Ameshaolewa na Wana maisha Yao)
Ilibdi niwaze kumpata mtu Ambae ninafahamiana nae, anatoka maeneo ya nyumbani.
Kuna binti mmoja ni mtoto wa rafiki yake na baba, walikua marafiki sana, huyo binti niliwahi kumtongoza kipindi Cha nyuma, wakati tunasoma aligoma, nikamwacha. Baba yake alifariki na wakati anafariki baba ni kama alikua mwangalizi wa familia hii.
Katika pita zangu juzi nikiwa single nimeachana na aliekuwa mchumba, nikakutana nae, ameachwa na waliekuwa nae na kibaya zaidi ana mtoto mmoja.
Nilimweka karibu kwanza kumchunguza, nilivutiwa nae kwa vingi, mapambano yake na historia mbaya sana aliokuwa akinipa kuhusu baba wa mwanae.
Tulienda muda kidogo tukaanza mahusiano, nikiwa makini sana, aaah huyu dada nilijikuta nampenda sana kama mwanzo, very organized, focused, nk nk, yaan package full, japo Kila nikisoma story za usioe single mother naishiwa pawa.
Anyway juzi hapa nikaona nimwoe, baada ya nyumbani pia kusema ni muda Sasa wa kuwa na mchumba, (baba alikua anajua tyari nilimwambia na alifurahi niwe na mtoto wa rafiki yake)
Nilijipanga nikaenda nyumbani kusema official, walifurahi na binti kwao walifurahi sana maana walikua wakitufahamu Toka tukiwa wadogo.
Shida Sasa ikaanza baada ya Mimi kurudi, nikapigiwa simu na dada mkubwa (ameachana na mume wake) ninaemfuata, akaniambia 'wewe kwanini unataka kupush sana mambo Yako wakati unaona nyumbani sahivi Kuna tukio la ukoo, Babu anataka kufanya jubilei' nilishangaa maana Mimi sikua na hizo taarifa, na kwa maelezo ya baba, mwezi wa 10 mwaka huu nilikua niwe na ndoa.
Nikamwambia asirudie kuniambia hivyo maana mm sijalazimisha chochote! Na nilikua sijui lolote,
Kilichofuata baba aliniambia ataenda kwa wakwe kuanza michakato, nikawa napigwa kalenda sana, mwisho akaniambia tatizo ni pesa nikamtumia, lkn Bado nikawa napigwa kalenda.
Hatimaye siku Moja mama akanipigia simu usiku, akaniambia, wewe...... Huoni Kuna Nini hapa nyumbani, tukio la Babu, na tunataka tutengeneze makaburi ya ukoo, nikamwambia mama mbona hivyo vitu havina gharama na vinaweza kwenda pamoja, akapata kigugumizi akaanza kunipa sababu zingine mwisho nikaanza kuonekana mkosaji Tena.. nikanyamaza.
Week kadhaa siku Moja baba akanipigia simu mchana akaniambia, usiwe unaongea nao sana hao, subiri mwakani hata mwezi wa kumi huko tutafanikisha...
Nilishangaa sana maana mwanzo nilikua nahamasishwa sana lkn sahv yamekuwa hayo...
Nipeni mawazo watu wangu wa maana, nianzie wapi? Nisije jikuta nachelewa zaidi na zaidi!