CreativityCode
Senior Member
- Aug 8, 2020
- 158
- 653
Huu ni wito kwa Wafanyabiashara na Wadau wote wa Sekta Binafsi. Tafadhali sana ili maisha yenu yarejee kwenye kukuza na kuimarisha biashara zenu muondoeni huyu mtu kwenye sanduku la kura.
Mpigeni za uso ili mumkumbushe kwamba serikali iliyostaraabika duniani kote haimiliki njia za uchumi na pia haifanyi biashara bali inaweka mazingira mazuri ya kufanya biashara.
Kwa miaka yote mitano Rais Magufuli amewaona wafanyabiashara na sekta binafsi kama wezi na adui wa Taifa. KITU AMBACHO SIYO KWELI HATA KIDOGO.
Rais Magufuli haamini kwamba Sekta Binafsi na biashara ni msingi wa uchumi imara.
Mfano mmoja pekee ni namna alivyoua mashirika binafsi ya ndege mfano wa fastJet, ingelikuwa ni Rais mwenye maono asingeliweza kununua midege ya serikali kwa fedha cash za Watanzania bali angetafuta wawekezaji wa uhakika tu wakawekeza kwenye shirika la ATCL ambalo bado lingefanya kazi ileile ya kuitangaza nchi, kuleta watalii n.k.
Fedha alizopeleka kwa anaowaita mabeberu ingeliboresha elimu ambayo tayari haina ubora wowote kwenye soko la ajira hata la Afrika Mashariki achana na soko la ajira la dunia.
NI HAYO TU KWA LEO, NAWATAKIA SIKU NJEMA.
Mpigeni za uso ili mumkumbushe kwamba serikali iliyostaraabika duniani kote haimiliki njia za uchumi na pia haifanyi biashara bali inaweka mazingira mazuri ya kufanya biashara.
Kwa miaka yote mitano Rais Magufuli amewaona wafanyabiashara na sekta binafsi kama wezi na adui wa Taifa. KITU AMBACHO SIYO KWELI HATA KIDOGO.
Rais Magufuli haamini kwamba Sekta Binafsi na biashara ni msingi wa uchumi imara.
Mfano mmoja pekee ni namna alivyoua mashirika binafsi ya ndege mfano wa fastJet, ingelikuwa ni Rais mwenye maono asingeliweza kununua midege ya serikali kwa fedha cash za Watanzania bali angetafuta wawekezaji wa uhakika tu wakawekeza kwenye shirika la ATCL ambalo bado lingefanya kazi ileile ya kuitangaza nchi, kuleta watalii n.k.
Fedha alizopeleka kwa anaowaita mabeberu ingeliboresha elimu ambayo tayari haina ubora wowote kwenye soko la ajira hata la Afrika Mashariki achana na soko la ajira la dunia.
NI HAYO TU KWA LEO, NAWATAKIA SIKU NJEMA.