Kibo10
JF-Expert Member
- Aug 20, 2013
- 11,277
- 8,840
Ni vizuri kuelewa jina lako au la mtoto na maana yake, kuna mambo mengi hukutokea kwa uzuri au ubaya lakini yawezekana na jina lako linachangia au asili ya jina lako
Kuna wengi wetu wamepewa majina yao kutoka kwa mababu zao ambao walikua na roho fulani labda ya umasikini, uzinzi, magonjwa n.k. Wengine wamepewa majina kutoka kwa waganga wa kienyeji au mizimu, ndio maana kuna vifungo fulani unavyo kwenye maisha yako.
Jina lako linangangania ubaki pale pale, hakuna kusonga mbele, wewe ni wa hivyo hivyo au unajimilikisha magonjwa fulani kwasababu bibi au babu zako walikua nayo.
Mfano unasema mimi ugonjwa wangu ni kisukari, TB au sie kwetu ndio ugonjwa wetu! nk
Tukatae misingi mibaya ya majina yetu, tusikubali wala usikubali kumpa mtoto wako majina ya laana
Kwa mfano Shida,Matatizo,Makusudi n.k.
Ni vizuri kukubali au kuwapa watoto majina yenye baraka na kibali katika maisha yetu.
Barikiweni sana!
Kuna wengi wetu wamepewa majina yao kutoka kwa mababu zao ambao walikua na roho fulani labda ya umasikini, uzinzi, magonjwa n.k. Wengine wamepewa majina kutoka kwa waganga wa kienyeji au mizimu, ndio maana kuna vifungo fulani unavyo kwenye maisha yako.
Jina lako linangangania ubaki pale pale, hakuna kusonga mbele, wewe ni wa hivyo hivyo au unajimilikisha magonjwa fulani kwasababu bibi au babu zako walikua nayo.
Mfano unasema mimi ugonjwa wangu ni kisukari, TB au sie kwetu ndio ugonjwa wetu! nk
Tukatae misingi mibaya ya majina yetu, tusikubali wala usikubali kumpa mtoto wako majina ya laana
Kwa mfano Shida,Matatizo,Makusudi n.k.
Ni vizuri kukubali au kuwapa watoto majina yenye baraka na kibali katika maisha yetu.
Barikiweni sana!