Mkaruka
JF-Expert Member
- Feb 5, 2013
- 19,617
- 34,062
Mkuu hii mijitu CHADEMA ni midikteta mibaya sana isiyo na madaraka tu.Kinachonishangaza kwa CHADEMA ni kumdharau Mdee kama vile ni takataka fulani. Mdee ameumizwa Mara ngapi kwa ajili ya CHADEMA? Hivi hiyo dhambi ya kwenda bungeni imemfanya Mdee kukosa thamani kiasi hicho?
Narudia kusema kwamba kama mnatuaminisha kuwa Mwendazake alikuwa Dikteta, mnayajua yaliyowakuta hao wanawake kabla ya kuapishwa? Wakati huo inasemekana nguvu ya dola ilitumika hata kumtoa mtu gerezani ili aapishwe. Kama ninyi mlivyotuamisha ina maana utawala wa amwendazake ulitumia nguvu ya dola kuhakikisha hawa wanawake wote wanaingia mtegoni.
Ni nguvu hiyo hiyo iliyosababisha wengine watoroke nchi, wengine kujisalimisha kabisa kwa kujiunga na sisiem, wengine kuishia magerezani. Hivi kwa nini hawa wanawake ndiyo waonekane wadhambi zaidi? CHADEMA mna haki kweli ya kuifundisha sisiem hekima? Kwa nini msipambane na mfumo mnaoamini ni kandamizi uliopelekea hao akidada kujisalimisha? Hilo tukio la hao Dada zenu mlioambatana nao siku zote kwenye siasa ya nchi hii na leo kuonekana takataka mbele zenu mkifanikiwa kuwaondoa mtakuwa mumetatua tatizo la nchi hii? Mnataka watoke muweke wake zenu?